Jela kwa kukataa chanjo

Jela kwa kukataa chanjo

Wameonewa tu labda kuwe na kosa jingine lakini kugomea chanjo sio kosa.
 
Watu saba wote Wakazi wa Kijiji cha Kalambo Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa, wamehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja Jela kila mmoja na Mahakama ya mwanzo Wilaya ya Kalambo baada ya kugoma Watoto wao wenye umri kati ya miezi 9 hadi 59 wasipewe chanjo ya ugonjwa wa Surua na Rubela wakidai chanjo sio maagizo ya Mungu.

Hukumu hiyo imetolewa February 26,2024 na Mahakimu wa Mahakama hiyo Elis Mkama na Suzy Mkinga kwa Washtakiwa hao ambao ni Abiniel Isaya (27), Misheck Simon (28), Isack Simon (26), Yona Simon (30), Efeso Peter (28), Job Simon (36) na Joshua Meshack (40)

Akitoa taarifa kuhusu hukumu hiyo leo February 27, 2024, RPC wa Rukwa, Shadrack Masija amesema chanjo hiyo ilikuwa ikitolewa na Wizara ya afya katika Kijiji hicho February 18, 2024, ambapo sababu ya kugomea ni imani ya dini yao ya Kanisa la Watchtower kwamba chanjo sio maagizo ya Mungu.

RPC Masija mesema “Kugomea chanjo inayoelekezwa na Serikali ni kufifisha juhudi za Serikali za kupambana na maradhi hivyo amewahimiza Wananchi wazingatie maagizo na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Serikali na wazitii Mamlaka za Serikali kwani zimewekwa na Mungu ambaye ndiye wote tunamwabudu”

CREDIT: MILLARD AYO

View attachment 2918605
Waacheni watu na watoto wao. Hizo chanjo Ulaya hawachanji, ziko kwenye majaribio na zina madhara makubwa sana kwenye maisha ya baadaye ya mtoto aliyechanjwa
 
Kuna maamuzi binafsi lakini ogopa kufanya maamuzi juu ya mtu mwingine mfano kuzuia mtoto asipate chanjo kitu ambacho ni hatari kwa Maisha yake mtoto ni kuyaweka Maisha ya mtoto hatarini
Kama mzazi hana maamuzi juu ya nini mwanawe afanyiwe au nini asifanyiwe huyo mtu baki hata ikiwa ni serikali mamlaka hayo anayapata wapi?
 
Kesi ya Mauaji ya watoto wadogo
Watoto hawajagoma bali wao watu wazima wanazuia haki ya mtoto kuishi kwa kuchanjwa kuzuia asipate maradhi ya kumuua ndio wanashinikiza watoto wasichanjwe ili wafe
Huyo hakimu kawapa adhabu ndogo sana Serikali ikate rufaa wapewe hukumu kubwa zaidi
Wonders shall never end! Mkuu, hivi hata wewe mwenyewe umeelewa ulichoandika? [emoji23]
 
Kama mzazi hana maamuzi juu ya nini mwanawe afanyiwe au nini asifanyiwe huyo mtu baki hata ikiwa ni serikali mamlaka hayo anayapata wapi?
Mamlaka ya serikali ni pamoja na kulinda afya za raia wake huwezi singizia kujisaidia hovyo hovyo barbarians kueneza kipindu pindu serikali ikikukamata useme mamlaka ya kukuzuia usijisaidie haja kubwa hovyohovyo serikali inatoa wapi inazuia rain wake wasiugue kipindupindu

Watoto ni Raia wa serikali inayo mamlaka kamili kulinda afya zao kwa chanjo
 
Mamlaka ya serikali ni pamoja na kulinda afya za raia wake huwezi singizia kujisaidia hovyo hovyo barbarians kueneza kipindu pindu serikali ikikukamata useme mamlaka ya kukuzuia usijisaidie haja kubwa hovyohovyo serikali inatoa wapi inazuia rain wake wasiugue kipindupindu

Watoto ni Raia wa serikali inayo mamlaka kamili kulinda afya zao kwa chanjo
Ushawahi kuona au kusikia mtu ameenda kukamatwa na kufungwa kisa ana tb au kansa au kisukari kwakuwa amekataa kwenda kutibiwa? Kwanini mtu akikataa chanjo iwe nongwa! mbona hatujasikia watu wakikamatwa na kufungwa kwa kukataa chanjo ya Covid 19 au chanjo ya homa ya ini au magonjwa hayo hayauwi? Halafu nitajie hiko kifungu cha sheria walichokiuka hao watu.
 
Nakubaliana nawe, ni njia ya kutisha watu wasiwe na uhuru wa Imani zao kama ilivyoainishwa na katiba.

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
Uhuru wa kuabudu upon ila uhuru wa kutoa uhai haupo

Mfano ukijifungia ndani ya Hengoed la ibadan ukasema mnajilipua moto muwahi kwa Mungu serikali itavamia hilo jengo na kuwatia nguvuni na kawashitaki kwa kutaka kujiua.Kujiua ni kosa na kuua mtu ni kosa

Watoto wakikosa chanjo ni hatari kwa Marshall yao hicho kitu serikali haiwezi kubali Maisha ya watoto yawe hatarini
 
Ushawahi kuona au kusikia mtu ameenda kukamatwa na kufungwa kisa ana tb au kansa au kisukari kwakuwa amekataa kwenda kutibiwa? Kwanini mtu akikataa chanjo iwe nongwa! mbona hatujasikia watu wakikamatwa na kufungwa kwa kukataa chanjo ya Covid 19 au chanjo ya homa ya ini au magonjwa hayo hayauwi? Halafu nitajie hiko kifungu cha sheria walichokiuka hao watu.
Uhuru wa kibinafsi kwa mtu mzima upo wa kukataa upo lakini huwezi tumia uhuru huo kukataa kwa niaba ya mtu mwingine kuwa mimi yule sitaki apewe dawa au chanjo awe mkubwa au mtoto
 
Uhuru wa kuabudu upon ila uhuru wa kutoa uhai haupo

Mfano ukijifungia ndani ya Hengoed la ibadan ukasema mnajilipua moto muwahi kwa Mungu serikali itavamia hilo jengo na kuwatia nguvuni na kawashitaki kwa kutaka kujiua.Kujiua ni kosa na kuua mtu ni kosa

Watoto wakikosa chanjo ni hatari kwa Marshall yao hicho kitu serikali haiwezi kubali Maisha ya watoto yawe hatarini
Ni kifungu gani hicho cha sheria kinasema hivyo Au ni mawazo yako tu?
 
Watu saba wote Wakazi wa Kijiji cha Kalambo Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa, wamehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja Jela kila mmoja na Mahakama ya mwanzo Wilaya ya Kalambo baada ya kugoma Watoto wao wenye umri kati ya miezi 9 hadi 59 wasipewe chanjo ya ugonjwa wa Surua na Rubela wakidai chanjo sio maagizo ya Mungu.

Hukumu hiyo imetolewa February 26,2024 na Mahakimu wa Mahakama hiyo Elis Mkama na Suzy Mkinga kwa Washtakiwa hao ambao ni Abiniel Isaya (27), Misheck Simon (28), Isack Simon (26), Yona Simon (30), Efeso Peter (28), Job Simon (36) na Joshua Meshack (40)

Akitoa taarifa kuhusu hukumu hiyo leo February 27, 2024, RPC wa Rukwa, Shadrack Masija amesema chanjo hiyo ilikuwa ikitolewa na Wizara ya afya katika Kijiji hicho February 18, 2024, ambapo sababu ya kugomea ni imani ya dini yao ya Kanisa la Watchtower kwamba chanjo sio maagizo ya Mungu.

RPC Masija mesema “Kugomea chanjo inayoelekezwa na Serikali ni kufifisha juhudi za Serikali za kupambana na maradhi hivyo amewahimiza Wananchi wazingatie maagizo na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Serikali na wazitii Mamlaka za Serikali kwani zimewekwa na Mungu ambaye ndiye wote tunamwabudu”

CREDIT: MILLARD AYO

View attachment 2918605
Hii hukumu si nzuri hata kidogo, na kwa kipindi hicho ambapo watakuwa ndani, serikali ichukue jukumu la kuwaangalia familia zinazotegemewa na hao waliyohukumiwa hicho kifungo. Chanjo zina faida na hasara pia, leo kuna idadi kubwa ya watoto waliyopatwa na maradhi ya usonji, ikiaminika kuwa sababu kubwa ni hizi chanjo wanazopewa watoto. Ni kweli hakuna utafiti uliyotolewa hadharani kwa kuwa litaharibu soko kubwa la chanjo hizo, tuliona tu hapa jinsi chanjo za Uviko zilivyoshikiwa bango na kuwalazimisha watu kuchomwa chanjo hizo, hivyo serikali lazima wajue jinsi ya kuwandea raia zake kuhusu mambo ya lazima kwenye afya zao. Hii kesi ifutwe na waachiwe watu waendelee na maisha yao.
 
Upumbavu wa kidini ukiruhusiwa kuingia kwenye jamii kwa sheria ya kila mtu ana haki ya kuamini anavyoamini italeta taharuki kubwa sana.
 
Upumbavu wa kidini ukiruhusiwa kuingia kwenye jamii kwa sheria ya kila mtu ana haki ya kuamini anavyoamini italeta taharuki kubwa sana.
Kuamini mtu aamini kivyake ila sio kwa niaba ya mwingine

Katiba inatambua kuwa dini ni swala la kibinafsi humwaminii mwingine kwa niaba yake

Tatizo linakuja mtu hataki tiba halafu anashinikiza na mwingine asipewe hapo ndipo tatizo lilipo kwa hao wayehova
 
Kuamini mtu aamini kivyake ila sio kwa niaba ya mwingine

Katiba inatambua kuwa dini ni swala la kibinafsi humwaminii mwingine kwa niaba yake

Tatizo linakuja mtu hataki tiba halafu anashinikiza na mwingine asipewe hapo ndipo tatizo lilipo kwa hao wayehova
Kabisa .
 
Back
Top Bottom