Uchaguzi 2020 Jemadari hodari hutambuliwa vitani. Dkt. Magufuli, Mungu anakupa miaka mitano tena kwa kwa kutushindisha vita dhidi ya Coronavirus

Uchaguzi 2020 Jemadari hodari hutambuliwa vitani. Dkt. Magufuli, Mungu anakupa miaka mitano tena kwa kwa kutushindisha vita dhidi ya Coronavirus

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,902
Reaction score
52,001
Vita ya Corona dunia nzima inawasumbua kote kuliko na majeshi yenye nguvu na teknlojia ya hali ya juu na wenye huduma za afya bora duniani zenye madaktari bingwa wazuri duniani ikiwemo Ubelgiji wako hoi kusumbuliwa na Corona.

Nchi zenye elimu bora na waongea kiingereza kizuri ikiwemo kenya na marekani kwa marafiki wa Lisu hali ngumu Corona muziki mzito kwao.

Sisi Tanzania chini ya jemadari wetu hodari kwa vita hii ya corona ya dunia tumeishinda na kuwa taifa LA kwanza duniani kuikimbiza Corona chini ya jemadari mkuu Mungu ambaye Jemadari wetu aliiomba tumwuombe

Mungu atakupa miaka mitano tena Jemadari wetu uendelee utuvushe vita zingine mbele.

Relax Mungu yu pamoja nawe kukushindia uchaguzi huu. Na sisi tuko pamoja nawe hatutalala hadi tuhakikishe unakanyaga Ikulu ndipo tutalala baada ya kumaliza kazi.
 
Lissu alisema Corona inaua wa-TZ kama kawaida yake akiwa Nairobi. Akapewa sifa ya kushambulia serikali, naye akavimba kichwa. Mbona kaingia kampeni havai barakoa na akijichanganya kwenye makundi. Sifa za kijinga.
 
Amejitahidi sana ,Elimu bure kama hivi...
IMG-20200924-WA0010.jpg
 
LIssu alisema Corona inaua wa-TZ mbona havai barakoa?
Katusaidia kujianika kwa wazungu kuwadhibitishia kuwa yeye muongo

Tulikuwa kabla tukiwaambia huyu Lisu wenu msanii na muongo walikuwa wakibisha sasa wanajionea live uongo wake hawamuamini tena taarifa zake hata apeleke picha za mafuriko wanajua kapika tu
 
Vita ya Corona dunia nzima inawasumbua note kuliko na majeshi yenye nguvu na teknlojia ya hali ya juu na wenye huduma za afya bora duniani zenye madaktari bingwa wazuri duniani ikiwemo ubelgiji wako hoi kusumbuliwa na Corona...
Sijui mnatetea kitu gani! Kati ya nchi zilizochukulia janga la corona kihovyo ni Tanzania, kuliko nchi yoyote ile duniani. Tumehangaika na midawa ya kienyeji kutoka Madagascar kwa kutumia fedha za walipa kodi leo hii ile dawa hata kuiongelea tu utafungwa.

Tumewaweka wananchi wetu rehani kwa ugonjwa tusioujua vizuri bila tahadhari zozote halafu leo tunajisifia kwa uzembe huu! Watu wamezikwa usiku kwa siri hadi imekuwa aibu kubwa kwa serikali, hadi leo watu wanafariki kimya kimya na haisemwi ni kwa corona halafu tunasifu.

Waliochukua hatua systematically sio wajinga, hao ndio tunaowaomba misaada kila siku ndio walio mbele kisayansi na tunanunua technolojia ya utabibu kutoka kwao.

Kama husikii vifo vya corona ni kwasababu vimezuiliwa kutangazwa, ni sawa tu na kutosikia Lissu kwamba yupo Chato leo kwasababu vyombo vya habari vimeamua tu kukaa kimya, lakini yupo Chato na anapolewa kifalme kule pia.
 
Magufuli alipigana vita akiwa kajificha nyumbani. Sasa sijui yeye au wewe uliyekuwa mtaani ni nani anastahili kuitwa Jemadari
 
Magufuli alipigana vita akiwa kajificha nyumbani. Sasa sijui yeye au wewe uliyekuwa mtaani ni nani anastahili kuitwa Jemadari
Alikuwa nyumbani akisali ulitaka atuombee akiwa anazunguka mabarabarani? Alifunga na viongozi wa dini wakafunga kuomba ili sisi wachacharikaji tusidondoke na Corona mabarabani kwenye mihangaiko yetu

Na Mungu katunusuru kwa sala zake
 
Vita ya Corona dunia nzima inawasumbua kote kuliko na majeshi yenye nguvu na teknlojia ya hali ya juu na wenye huduma za afya bora duniani zenye madaktari bingwa wazuri duniani ikiwemo ubelgiji wako hoi kusumbuliwa na Corona...

Unachekesha..
 
Kwa hiyo JPM anamtumia Mungu kama msaidizi wa kampeni zake?

Mungu kaponya Corona ili kuokoa watu wake na siyo iwe sehemu ya kampeni za Magufuli.
 
Wakati wa Corona Jiwe alikimbia Dodoma na kwenda kujificha kijijini kwao Chato.

Ananikumbusha Iddi Amini ambaye wakati wa vita vya Uganda alilikimbia jiji la Kampala na kwenda kujificha kijijini alikozaliwa Koboko.
 
Unachekesha..

Wataalam wa afya Tanzania tafadhalini tuelimisheni kuhusu HERD IMMUNITY na athari zake!!! Inaelekea huyu JIWE ametuingiza Chaka kuamini kuwa sisi peke yetu dunia nzima ndio tunasikilizwa na MUNGU!!!
 
Back
Top Bottom