Jenerali Mirisho Sarakikya: Niliteuliwa kuwa Mkuu wa Majeshi nikiwa na umri wa miaka 30

Jenerali Mirisho Sarakikya: Niliteuliwa kuwa Mkuu wa Majeshi nikiwa na umri wa miaka 30

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
07 January 2022

Mkuu wa Majeshi wa Kwanza JENERALI SARAKIKYA, Asimulia Alivyoshiriki Kuliunda Jeshi



Katika interview hii maalum mhitimu wa chuo tajwa kabisa cha kijeshi duniani cha Sandhurst huko Uingereza, Jenerali mstaafu Mirisho Sam Hagai Sarakikya anaelezea alivyojiunga jeshi mwaka 1959 ambapo aliwakuta David Musuguri na Mwita Waitara wakiwa na vyeo vya juu vya nyota ya kitambaa siyo ya chuma mabegani ....pia undani wa maasi ya mwaka 1964 na utumishi wake jeshi hadi anastaafu jeshi mwaka 2002.

Kapteni Mirisho Sam Hagai Sarakikya kwa mstuko mkuu akiwa afisa kijana umri miaka 30 tu mwaka 1964 aliteuliwa na Rais Julius Nyerere kuwa Mkuu wa Majeshi.

Hii ni kufuatia maasi ya jeshi la KRA mwaka 1964 na serikali kuamua kuwatimua waasi wote kutoka jeshini kutokana na kukosa uzalendo, hivyo kuanza upya kuunda jeshi litakalokuwa na uzalendo kwa Taifa.

Hivyo akapandishwa cheo kuwa Brigedia kwa wakati huo Brig. Mirisho Sam Hagai Sarakakya kwa kuwaongoza maafisa wenzake na kwa bahati nzuri hakukuwa na afisa yoyote aliyeshiriki katika maasi hayo yaliyokuja kuzimwa na Jeshi la Uingereza lililoombwa kuzima maasi ya askari ... walishughulika kuunda upya jeshi lililo na mtizamo wa kulitumikia Taifa na wananchi hivyo kuwa JWTZ .

Hivyo chini ya uongozi wake Jenerali Sarakikya walipewa jukumu la kupatikana Jeshi la nchi kavu infantry, jeshi la majini navy, jeshi la anga, na kufuatiwa na kuanzisha pia shule za wapiganaji shule za maofisa, staff college, vyuo vya maofisa.

Jenerali Sam Hagai Sarakikya sasa ni mstaafu kwa miaka inayozidi 10 anajisikia fahari kuazimishwa kwa miaka 60 ya uhuru pia kuundwa upya jeshi la kizalendo hadi kuwa la kisasa na operesheni mbalimbali JWTZ ilizoshiriki Seychelles, Comoros, Mozambique, South Sudan, DR Congo n.k
Source : Ulinzi Channel


Habari za ziada :

TPDF / JWTZ December 2021



Video courtesy of Wasafi Media


Kamandi ya Jeshi la anga la Tanzania


Video courtesy of the Boss tv

Kamandi ya Jeshi la Wanamaji Tanzania NAVY


Rear Admiral Michael Mumanga mkuu wa kamandi ya jeshi la wanamaji - Navy
Video courtesy of Ulinzi Channel
 
Aendelee kuishi miaka mingi, long live gallant officer, a true legend among statesmen
 
07 January 2022

Mkuu wa Majeshi wa Kwanza JENERALI SARAKIKYA, Asimulia Alivyoshiriki Kuliunda Jeshi



Katika interview hii maalum mhitimu wa chuo tajwa kabisa cha kijeshi duniani cha Sandhurst huko Uingereza, Jenerali mstaafu Mirisho Sam Hagai Sarakikya anaelezea alivyojiunga jeshi mwaka 1959 pia undani wa maasi ya mwaka 1964 na utumishi wake jeshi hadi anastaafu jeshi mwaka 2002.

Kapteni Mirisho Sam Hagai Sarakikya kwa mstuko mkuu akiwa afisa kijana umri miaka 30 tu mwaka 1964 aliteuliwa na Rais Julius Nyerere kuwa Mkuu wa Majeshi.

Hii ni kufuatia maasi ya jeshi la KRA mwaka 1964 na serikali kuamua kuwatimua waasi wote kutoka jeshini kutokana na kukosa uzalendo, hivyo kuanza upya kuunda jeshi litakalokuwa na uzalendo kwa Taifa.

Hivyo akapandishwa cheo kuwa Brigedia kwa wakati huo Brig. Mirisho Sam Hagai Sarakakya kwa kuwaongoza maafisa wenzake na kwa bahati nzuri hakukuwa na afisa yoyote aliyeshiriki katika maasi hayo yaliyokuja kuzimwa na Jeshi la Uingereza lililoombwa kuzima maasi ya askari ... walishughulika kuunda upya jeshi lililo na mtizamo wa kulitumikia Taifa na wananchi hivyo kuwa JWTZ .

Hivyo chini ya uongozi wake Jenerali Sarakikya walipewa jukumu la kupatikana Jeshi la nchi kavu infantry, jeshi la majini navy, jeshi la anga, na kufuatiwa na kuanzisha pia shule za wapiganaji shule za maofisa, staff college, vyuo vya maofisa.

Jenerali Sam Hagai Sarakikya sasa ni mstaafu kwa miaka inayozidi 10 anajisikia fahari kuazimishwa kwa miaka 60 ya uhuru pia kuundwa upya jeshi la kizalendo hadi kuwa la kisasa na operesheni mbalimbali JWTZ ilizoshiriki Seychelles, Comoros, Mozambique, South Sudan, DR Congo n.k
Source : Ulinzi Channel


Habari za ziada :

TPDF / JWTZ December 2021



Video courtesy of Wasafi Media


Kamandi ya Jeshi la anga la Tanzania


Video courtesy of the Boss tv

Kamandi ya Jeshi la Wanamaji Tanzania NAVY


Video courtesy of Ulinzi Channel

Kikwete alipeleka barua kwa Nyerere, kumsimanga Sarakikya, Nyerere akampa Sarakikya barua ile alipomtembelea ikulu.

Baada ya hapo uanajeshi wa Kikwete ukakoma rasmi, yeye Mwenyewe akajiondoa, Tena kwa adhabu kubwa akitembea kwa miguu kutoka Monduli Hadi Arusha
 
Kikwete alipeleka barua kwa Nyerere, kumsimanga Sarakikya, Nyerere akampa Sarakikya barua ile alipomtembelea ikulu.

Baada ya hapo uanajeshi wa Kikwete ukakoma rasmi, yeye Mwenyewe akajiondoa, Tena kwa adhabu kubwa akitembea kwa miguu kutoka Monduli Hadi Arusha

..hii habari umeipata wapi?

..Sarakikya aliondoka jeshini mwaka 1974.

..wakati huo Kikwete alikuwa masomoni Udsm.
 
Kikwete alipeleka barua kwa Nyerere, kumsimanga Sarakikya, Nyerere akampa Sarakikya barua ile alipomtembelea ikulu.

Baada ya hapo uanajeshi wa Kikwete ukakoma rasmi, yeye Mwenyewe akajiondoa, Tena kwa adhabu kubwa akitembea kwa miguu kutoka Monduli Hadi Arusha
Siyo Sarakikya. Ni Sayole aliyekuwa mkuu wa chuo Monduli Tanzania Military Academy.
 
Kikwete alipeleka barua kwa Nyerere, kumsimanga Sarakikya, Nyerere akampa Sarakikya barua ile alipomtembelea ikulu.

Baada ya hapo uanajeshi wa Kikwete ukakoma rasmi, yeye Mwenyewe akajiondoa, Tena kwa adhabu kubwa akitembea kwa miguu kutoka Monduli Hadi Arush

Na ujanja wote ule kumbe ndo alipoishia.
 
Kikwete alipeleka barua kwa Nyerere, kumsimanga Sarakikya, Nyerere akampa Sarakikya barua ile alipomtembelea ikulu.

Baada ya hapo uanajeshi wa Kikwete ukakoma rasmi, yeye Mwenyewe akajiondoa, Tena kwa adhabu kubwa akitembea kwa miguu kutoka Monduli Hadi Arusha
Kamba hii..
 
..alikuwa na utamaduni wa kupanda mlima Kilimanjaro kila mwaka.

..huenda anashikilia rekodi ya kupanda mlima huo mara nyingi zaidi, sina uhakika lakini.
Zamani wasomi walikuwa wachache sana au vijana waliaminika?

Mfano Mwl Nyerere alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika akiwa 'under 40'.....tena aliongoza harakati za Uhuru akiwa kwenye early 30's tu.

Mstaafu Sarakikya alikuwa mkuu wa majeshi akiwa na miaka 30 tu.

Mstaafu Dr Salim Ahmed Salim alikuwa balozi wa Tz huko Misri akiwa kwenye early 20's.

Vijana wa zamani walikuwa na kipi tofauti na sisi mpaka kupata madaraka makubwa wakiwa na umri mdogo?....sisi wa Leo tunakwama wapi? ....
 
Zamani wasomi walikuwa wachache sana au vijana waliaminika?

Mfano Mwl Nyerere alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika akiwa 'under 40'.....tena aliongoza harakati za Uhuru akiwa kwenye early 30's tu.

Mstaafu Sarakikya alikuwa mkuu wa majeshi akiwa na miaka 30 tu.

Mstaafu Dr Salim Ahmed Salim alikuwa balozi wa Tz huko Misri akiwa kwenye early 20's.

Vijana wa zamani walikuwa na kipi tofauti na sisi mpaka kupata madaraka makubwa wakiwa na umri mdogo?....sisi wa Leo tunakwama wapi? ....
Utajipa teuzi?
 
  • Kicheko
Reactions: Pep
Zamani wasomi walikuwa wachache sana au vijana waliaminika?

Mfano Mwl Nyerere alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika akiwa 'under 40'.....tena aliongoza harakati za Uhuru akiwa kwenye early 30's tu.

Mstaafu Sarakikya alikuwa mkuu wa majeshi akiwa na miaka 30 tu.

Mstaafu Dr Salim Ahmed Salim alikuwa balozi wa Tz huko Misri akiwa kwenye early 20's.

Vijana wa zamani walikuwa na kipi tofauti na sisi mpaka kupata madaraka makubwa wakiwa na umri mdogo?....sisi wa Leo tunakwama wapi? ....

..Ni kwasababu wasomi walikuwa wachache.

..zama hizi huwezi kuwa balozi ukiwa na miaka 20.
 
Zamani wasomi walikuwa wachache sana au vijana waliaminika?

Mfano Mwl Nyerere alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika akiwa 'under 40'.....tena aliongoza harakati za Uhuru akiwa kwenye early 30's tu.

Mstaafu Sarakikya alikuwa mkuu wa majeshi akiwa na miaka 30 tu.

Mstaafu Dr Salim Ahmed Salim alikuwa balozi wa Tz huko Misri akiwa kwenye early 20's.

Vijana wa zamani walikuwa na kipi tofauti na sisi mpaka kupata madaraka makubwa wakiwa na umri mdogo?....sisi wa Leo tunakwama wapi? ....
Wazee wao hawakuwa na hila, waliwaamini vijana wenye uwezo!

Wazee wa siku hizi wanapalilia watoto wao tu ndio wawe viongozi hata kama hawana akili, hawana uzalendo na ni wezi.
 
Kikwete alipeleka barua kwa Nyerere, kumsimanga Sarakikya, Nyerere akampa Sarakikya barua ile alipomtembelea ikulu.

Baada ya hapo uanajeshi wa Kikwete ukakoma rasmi, yeye Mwenyewe akajiondoa, Tena kwa adhabu kubwa akitembea kwa miguu kutoka Monduli Hadi Arusha
Nafikiri ilikuwa barua kwa Sayore na sio Sarakikya
 
Kikwete alipeleka barua kwa Nyerere, kumsimanga Sarakikya, Nyerere akampa Sarakikya barua ile alipomtembelea ikulu.

Baada ya hapo uanajeshi wa Kikwete ukakoma rasmi, yeye Mwenyewe akajiondoa, Tena kwa adhabu kubwa akitembea kwa miguu kutoka Monduli Hadi Arusha

HUU uzee ni tabu, kumbukumbu zangu zinanisuta kuwa aliyeshitakiwa na Jakaya ni Sayore( aliyekuwa mkuu wa chuo cha kijeshi cha Monduli) na "SI" sarakikya. Sarakikya hajawahi kuwa boss wa Jakaya. iLA inaonesha mpeleka mashitaka alikuwa na lake jambo
 
Back
Top Bottom