Salaam Tanzania, Natumai ni wazima
Jumapili ya Agosti 25, 2019 ni siku mbaya sana wa sisi
Wanasimba kindakindaki kwa matokeo mabaya ya kufurushwa kwenye mashindano ya kimataifa ya Klabu Bingwa Afrika.
Ndugu zangu Wanasimba Jenga Morali kwa wachezaji wetu
Simba SC, Wekundu wa Msimbazi, tuwaunge mkono, si wakati wa kutupa lawama kwa viongozi na wachezaji pamoja na benchi la ufundi, kawaida ya mpira unatoa matokeo pengine hayatarajiwi pamoja na kujiandaa kwa asilimia
99%, maana naona wengine wameanza kuwataja akina Emmanuel Okwi, jamani kwa style hiyo hatuwezi kusonga mbele na madhara yake ni kuwavunja moyo wachezaji wengine, ni sawa kuwakumbuka akina Kibadeni na Mwameja ambapo muda wao tayari umepita.
Jamani tusisahau vilevile mpira kuna bahati, na siku ya Jumapili haikuwa bahati yetu Wanasimba, hatujafungwa lakini tumeondoshwa kwa kanuni, kwahivyo jambo muhimu kwa sasa tuangalie patashika nyingine VPL, na ASFC kwani tuna timu bora kabisa kwenye ukanda huu, soka la
Simba SC ni level ya juu iliyothibitishwa na Shirikisho la Kandanda Afrika CAF.
Kwa upande wa pili, kutoka kuanza kwa michuano hii 2019, tulijitahidi sana kuwa wazalendo kupitia kwenye Tv, Radio na baadhi ya mitandao ya kijamii, lakini mmekosa busara, lakini tunasema tutalipa ili mjifunze.
Na hapo nilifarijika mno baada ya kusoma historia ya Klabu ya Zesco United nimegundua kumbe Ndugu yangu mimi
Ghazwat wa damu kabisa yupo Zambia, na baba yake amewahi kuchezea Zesco United, kwahivyo Wanasimba kwa niaba Ndugu yangu, Zesco watatufurahisha mno,
Unyama Unyamani NguvuMoja.View attachment 1191147View attachment 1191148