KERO Jengo la Wilaya ya Tanganyika lililopo Manispaa ya Mpanda linaharibu taswira ya Mji kwa uchafu

KERO Jengo la Wilaya ya Tanganyika lililopo Manispaa ya Mpanda linaharibu taswira ya Mji kwa uchafu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Torra Siabba

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
243
Reaction score
287
WhatsApp Image 2024-11-26 at 11.01.16_b30b0f69.jpg

WhatsApp Image 2024-11-26 at 11.00.53_f01a6923.jpg
Hili ni moja ya majengo yanayomilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika zamani Mpanda DC yaliyopo Manispaa ya Mpanda, Jambo la ajabu jengo hili limetelekezwa kwa sababu mazingira yake yanaonekana machafu sana.

Ni aibu kubwa mazingira ya jengo hili kuwa machafu ili hali liko katikati ya Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Uchafu huo unaharibu taswira ya mji na kuufanya kuonekana mchafu na kuibua maswali mengi kwamba inamaana watu wenye mamlaka hawaoni uchafu huo?

Natoa wito kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika kuhakikisha ukarabati na usafi ili kudhibiti magonjwa ya mlipuko yanayosababishwa na uchafu, kama hivi karibuni Katibu Tawala Mkoa wa Katavi alivyoripoti kipindupindu.

Nashauri kwa kuwa jengo hilo liko Manispaa ya Mpanda ni vema sasa Wilaya ya Tanganyika ikalimilikisha jengo hilo kwa Manispaa hiyo kwani itakuwa rahisi kwa jengo hilo kukarabatiwa na mazingira yake kufanywa kuwa safi.

Kwa sasa jengo hilo linatumika hususani wakati wa mitihani ya Wanafunzi, ndio huwaga tunaona wanakwenda hapo na limefanywa kuwa kama bohari ya kutunzia mitihani.
WhatsApp Image 2024-11-26 at 11.01.37_0380af0b.jpg

WhatsApp Image 2024-11-26 at 11.02.34_2bf25e72.jpg
 
Mpanda ni mji unaokua mkuu hivyo majengo chakavu lazima yawepo
Umeona majengo ya hospital ya manispaa yalivyo?
 
Back
Top Bottom