Jengo letu pendwa Mwanza

Jengo letu pendwa Mwanza

Raha sana, Mwanza tumebahatika kuwa na jengo zuri la kibiashara.
Zamani ulikuwa ukitoka mkoani ukifika jiji la samaki lazima ukapige picha pale kwenye samaki, kwa sasa tuna jengo jipya la kibiashara la Rock City Mall ukifika mwanza karibu sana ndani ya jengo letu pendwa. Jamani ndani ya jengo hili hata ukiwa chooni au kwenye lift ya mizigo iliyojaa vumbi lazima kwa mbali utasikia mziki laini ukikubembeleza.

Kilichonifurahisha zaidi ni baada ya Chuo flani kuwa sehemu ya wapangaji wa jengo hili, kwanza coarse zitolewazo na chuo hiki ni kozi pendwa na Maua ya Uaridi. 85% ya wanachuo wote ni Ua la Kondeni. Kiuhalisia haya maua na zile nyimbo nyororo ndani ya jengo letu pendwa vimenifanya kuwa mwadilifu kazini, wa kwanza kuingia na wa mwisho kutoka. Kinachonifurahisha, muda mwingi viumbe hivi pendwa hushinda vikizungukia jengo letu pendwa, kiufupi binafsi nafaid sana
Ujue hata machangudoa watajitambulisha kuwa ni wanachuo, nasubiri ulete uzi wa kuwalalamika kuwa wanafunzi hao ni matapeli.
 
Mkuu mbona cc tupo tu, hizi n changamoto za kawaida, wenye unafuu ni sisi wenye ofisi za kawaida lakini wenye maduka ya bidhaa hali sio nzur kiukwel

Tatizo lao wanauzia sifa,yaani shati la 20,000 ukiingia humo unauziwa 60,000
 
Sasa nimeelewa kwann kuna siku kuna mtu alileta mada ya chuo Fulani kuleta wanafunzi hapo uku akilalamika kwa chuo icho kumpa mtihani wa kushindwa kufanya kazi zake vizuri
 
Sasa nimeelewa kwann kuna siku kuna mtu alileta mada ya chuo Fulani kuleta wanafunzi hapo uku akilalamika kwa chuo icho kumpa mtihani wa kushindwa kufanya kazi zake vizuri
Kitaje basi hicho chuo
 
Back
Top Bottom