Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Ukiachana na uchapakazi , uzalendo na kubadilika kulingana na Mazingira kwa Mheshimiwa Jenista Mhagama.
Lakini ukweli unabakia kuwa heshima na unyenyekevu wake ni miongoni Mwa vitu vinavyomfanya kujenga ushawishi kwa kila Rais anayeingia Madarakani kumuweka katika majina ya awali kabisa ya Baraza la Mawaziri.
Unyenyekevu wake ndio unaofanya aweze kufanya kazi kila wizara anayopelekwa na kupewa ushirikiano mkubwa sana na watumishi anaowakuta.
Ndio sababu ni miongoni Mwa waheshimiwa waliopita wizara nyingi na kufanikiwa kufanya vizuri sana na kuacha alama kubwa sana .
Hana viburi wala dharau wala majibu ya hovyo ni mtu mwenye kauli nzuri na za hekima sana hata kwa wapinzani. Hajiinui wala kujikweza licha ya kuwa na uhakika wa namba na nafasi katika Baraza la Mawaziri.
Lakini ameendelea kuwa Jenista Mhagama yule yule mwenye unyenyekevu ule ule kwa watu wote.
Hata katika Biblia unyenyekevu ni vitu vinavyosisitizwa sana kwa mkiristo na unaweza kufunguliwa milango mingi sana ya Baraka .Mtu mnyenyekevu ni lazima pia utakuta ndani yake ana moyo wa huruma, upendo, utu, uungwana, hekima na busara.
Ndio maana Mama huyu anaendelea kudumu na kubakia katika Baraza la Mawaziri na kung'ara muda wote Nyota yake.
Siyo mara ya kwanza kusema jambo hili hata awali nimewahi kusema na kuandika humu jukwaani juu ya jambo hili la unyenyekevu na heshima aliyo nayo Mama huyu..
Wanasiasa wengine wanayo Mengi sana ya kujifunza kutoka kwa Mama huyu asiye na Makuu.
Kiongozi yeyote yule siku zote angependa kufanya kazi na wafanyakazi ama wasaidizi wanyenyekevu, wenye heshima na wachapakazi aina ya Mheshimiwa Jenista Mhagama. Kwa sababu watu na viongozi wa aina hiyo ni rahisi kubadilika kulingana na mazingira, kuhudumia watu vyema, wasikivu na wenye kuleta matokeo chanya.
Mwisho niseme wazi kuwa Mimi huwa sina wivu wala kuacha kumsifia na kumpongeza mtu anayefanya vizuri. lakini pia ukifanya vibaya nakukosoa tu ili ujirekebishe..
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Ukiachana na uchapakazi , uzalendo na kubadilika kulingana na Mazingira kwa Mheshimiwa Jenista Mhagama.
Lakini ukweli unabakia kuwa heshima na unyenyekevu wake ni miongoni Mwa vitu vinavyomfanya kujenga ushawishi kwa kila Rais anayeingia Madarakani kumuweka katika majina ya awali kabisa ya Baraza la Mawaziri.
Unyenyekevu wake ndio unaofanya aweze kufanya kazi kila wizara anayopelekwa na kupewa ushirikiano mkubwa sana na watumishi anaowakuta.
Ndio sababu ni miongoni Mwa waheshimiwa waliopita wizara nyingi na kufanikiwa kufanya vizuri sana na kuacha alama kubwa sana .
Hana viburi wala dharau wala majibu ya hovyo ni mtu mwenye kauli nzuri na za hekima sana hata kwa wapinzani. Hajiinui wala kujikweza licha ya kuwa na uhakika wa namba na nafasi katika Baraza la Mawaziri.
Lakini ameendelea kuwa Jenista Mhagama yule yule mwenye unyenyekevu ule ule kwa watu wote.
Hata katika Biblia unyenyekevu ni vitu vinavyosisitizwa sana kwa mkiristo na unaweza kufunguliwa milango mingi sana ya Baraka .Mtu mnyenyekevu ni lazima pia utakuta ndani yake ana moyo wa huruma, upendo, utu, uungwana, hekima na busara.
Ndio maana Mama huyu anaendelea kudumu na kubakia katika Baraza la Mawaziri na kung'ara muda wote Nyota yake.
Siyo mara ya kwanza kusema jambo hili hata awali nimewahi kusema na kuandika humu jukwaani juu ya jambo hili la unyenyekevu na heshima aliyo nayo Mama huyu..
Wanasiasa wengine wanayo Mengi sana ya kujifunza kutoka kwa Mama huyu asiye na Makuu.
Kiongozi yeyote yule siku zote angependa kufanya kazi na wafanyakazi ama wasaidizi wanyenyekevu, wenye heshima na wachapakazi aina ya Mheshimiwa Jenista Mhagama. Kwa sababu watu na viongozi wa aina hiyo ni rahisi kubadilika kulingana na mazingira, kuhudumia watu vyema, wasikivu na wenye kuleta matokeo chanya.
Mwisho niseme wazi kuwa Mimi huwa sina wivu wala kuacha kumsifia na kumpongeza mtu anayefanya vizuri. lakini pia ukifanya vibaya nakukosoa tu ili ujirekebishe..
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.