Jerry Muro afungiwa kujihusisha na soka kwa Mwaka mmoja!!

Sasa Yanga watashinda maana taarabu zake zilikua zinawatia mkosi uwanjani.
 
Jerry Muro ajifunze kuwa na kaba ya mdomo. Mwaka mzima ni pigo kwake. Hopefully atajifunza na kuomba radhi asamehewe. Asifanye kiburi namshauri
 

....wacha kelele wewe,ulishaonywa mara nyingi ukajidai mjanja hukutaka kusikia,inshort huna adabu huo mwaka mimi nauona mdogo sana!.Ulimtukana mdada wa watu mwandishi wa habari kenge wewe wala hukuomba radhi,unajidai kichwa ngumu unajua kila kitu,kakae huko porini sasa ujifunze adabu.

...Umeitwa mbumbumbu hujui sheria za CAF unaleta kelele una degree tatu!,hizo degree zinahusiana nini na sheria za CAF?!, mimi nasisitiza wewe ni mbumbumbu kajifunze adabu.
 
Tatizo lako ni: (1) kuamini kwamba mimi ni Jerry Muro kwa sababu tu nimeelezea udhafu wa hukumu dhidi yake. Nakusikitikia kwa kupoteza muda na matusi yako dhidi ya unauemdhani kuwa ndiye JM. Pole sana. (2) Unadhani mwenye haki ya kutukana wenzake ni wewe tu kama ulivyofanya hapo juu kumtukana unayemdhani ni JM. Kama wewe una haki hiyo, kwa nini naye asiwe nayo, iwapo kweli alitukana? Pole sana. (3) Kukurupuka kumtukana mtu kwa dhana tu kwamba ndiye hasa unayemchukia kwa sababu tu hupendezwi na kauli zake ni kiashirio cha vyote, ukosefu wa adabu uliokithiri na umbumbumbu uliotopea. Pole sana.
Ushauri wangu kwako ni uleule wa awali, kwamba kila mtu ana haki ya kutoa mawazo yake madhali havunji Katiba wala Sheria. Aidha, weledi ni pamoja na kuwastahamilia wanaojaribu kuwasilisha mawazo yao lakini wakateleza katika kujieleza kwao. Ndio maana ninaheshimu matusi yako kwangu. Ila ni vyema ukaelewa kwamba si kila mtu ni mstahamilivu kama mimi, unaweza ukan'gatwa na Sheria ya Makosa ya Kimtandao na ukajikuta umetumikia kifungo cha Dola, siyo cha kamba ya mgomba cha TFF unachokifurahia kwa Jerry Muro unayemdhani kuwa ni mimi.
 
Yaani hawa vijana ni shida sana. Ona kama huyo naye anajiona ni Nabii anaanza kutabiri uhalisia wa watu wengine.

Si kwamba tunawaonea hawa Mashabiki wa upande wa pili ila ukiangalia kwa undani na kuwachunguza zaidi utagundua wengi wao wana matatizo ya "Brain Dysfunctions"

Ila huwa sisahau kuwaweka kwenye maombi, pale ninapokuwa kwenye maombi na Mwenyezi MUNGU.
 
Ndio maana nimewasikia baadhi ya wapenzi wa Yanga wakijisikitikia kuwa watani wao wa jadi ni watu wa aina hii!
 
Well said mkuu..
Mpka nmejiulza io kamat ilyotoa hukumu ni wanafunzi wa primary au watu wazma
 
Ingawa mimi ni shabiki na mwanachama wa Msimbazi, ila kuna sehemu hawa wakubwa wameteleza, hasa hili la kukosa kujitetea mbele ya kamati baada ya kutopata wito wa kuitwa. Wakubwa wameteleza!
 
Tatizo jamaa pumba nyingi sana
Na kutaka sifa. Utakumbuka alikuwa ITV akiendesha kipindi kilichovuma sana mida ya saa tatu usiku. Akawagusa wazee, akaibukia TBC nako naona hakuwa na bahati njema na sasa hapo jangwani ananyea kambi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…