Jerry Muro afungiwa kujihusisha na soka kwa Mwaka mmoja!!

akimaliza hio adhabu tutamrejesha kwe nafas yake
 
Kuhamasisha mashabiki wa Yanga waje kwa wingi uwanjani na kuwanyima nafasi Simba!!? Sijaelewa hapo
 
Kwa wakati huu Jerry anaposhughulikia rufaa yake, Masao Bwire atakaimu kwa muda. Wembe ule ule
 

....ondoa mashairi yako hapa,huu ushauri wako ungempa huyo muro unaemtetea ningekuona wa maana zaidi.Inshort, muro ni mhuni anastahili adhabu full stop!,mlimuendekeza sasa yamemkuta unanza kuleta analysis hapa!,kamtetee mahakamani,hop unapendezwa sn na ule mdomo wake! (hilo jina sijaanza kwa herufi kubwa kwa sababu maalum!)
 
Nashukuru umeelewa kwamba mimi siyo Muro. Hongera. Usijionee haya kwa utumbo wako wa awali kuwavaa watu kwa dhana. Lichukulie kuwa ni funzo kwako, kama utakuwa na akili ya kujifunza. Najua umesema 'full stop' kwa maana ya kuwa huhitaji tena mjadala nami. Nami kwako nasema sitaendeleza mjadala nawe kwa hili. Full stop.
 
Well said mkuu..
Mpka nmejiulza io kamat ilyotoa hukumu ni wanafunzi wa primary au watu wazma
Exactly. Wanashindwa hata kuelewa kwamba Muro ni mwajiriwa wa Yanga na kwa hivyo waitake Yanga iliyo mwanachama wao TFF ndiyo imfungie msemaji wake. Hata hilo hawalijui basi? Kusoma hawajui, basi hata picha hawaoni?
 
Ingawa mimi ni shabiki na mwanachama wa Msimbazi, ila kuna sehemu hawa wakubwa wameteleza, hasa hili la kukosa kujitetea mbele ya kamati baada ya kutopata wito wa kuitwa. Wakubwa wameteleza!

Kutokuhudhuria mbele ya kamati kwa visingizio vya kitoto hakuwezi kukufanya uepuke adhabu. Alishapata wito, alipaswa kwenda kujitetea
 
Exactly. Wanashindwa hata kuelewa kwamba Muro ni mwajiriwa wa Yanga na kwa hivyo waitake Yanga iliyo mwanachama wao TFF ndiyo imfungie msemaji wake. Hata hilo hawalijui basi? Kusoma hawajui, basi hata picha hawaoni?

Hivi sheria au hizi kanuni unazipata wapi? Kosa linaweza kuwa la mtu mmoja mmoja au taasisi, au vyote. Hebu pitia tena details za shauri la Muro halafu ndio ulete analysis zako. Adhabu anapewa menda kosa na sio familia yake au taasisi anayofanyia kazi
 
Ingawa mimi ni shabiki na mwanachama wa Msimbazi, ila kuna sehemu hawa wakubwa wameteleza, hasa hili la kukosa kujitetea mbele ya kamati baada ya kutopata wito wa kuitwa. Wakubwa wameteleza!

Hili la Muro kutopata wito wa kamati una uhakika nalo au ni dhanio lako tu? Huoni kama Katbu wa Yanga alihudhuria kikao kutoa udhuru wa mdomo kuhusu Muro kwenda Moshi kwa mambo yake binafsi? Someni vzr details za shauri kabla hamjatafuta pa kuchomokea
 
Nasoma post za weng hum lkn naona weng hatujajua bado kazi ya MSEMAJI wa klabu...
 
Sio mimi niliyechomeka, ni Jerry Muro!
 
Adhabu na kosa unalozungumzia wewe ni la makosa ya jinai ambayo msikilizaji na anayehukumu ni Mahakama pekee. Hili la Muro ni swala la nidhamu (disciplinary matter) baina ya mkubwa na aliye chini yake (boss and his subordinate). Unapochelewa kwenda kazini, mwajiri anaweza kukukata mshahara bila ya kupitia mahkamani kwa sababu ni swala lililo ndani ya mkataba wa ajira yako. Yanga ikiruka ukuta kuingia uwanjani itaadhibiwa na TFF bila ya kupitia mahkamani kwa sababu nidhamu ya kuingia uwanjani ni sehemu ya makubaliano baina ya Yanga na TFF ndani ya kanuni za kuendesha Ligi. Niambie Muro ana uhusiano gani wa moja kwa moja na TFF au kuna makubaliano gani ya moja kwa moja baina ya Muro na TFF bila ya kupitia Yanga iliyomwajiri ambayo ndiyo ina makubaliano yenye mashiko na TFF? Umeona wapi baba mkwe akatoa talaka kwa mke wa mwanawe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…