Pre GE2025 Jeshi la Polisi lazingira Ofisi ya Makao Makuu CHADEMA Mikocheni na kuzuia Mkutano wa Mnyika na Waandishi wa Habari

Pre GE2025 Jeshi la Polisi lazingira Ofisi ya Makao Makuu CHADEMA Mikocheni na kuzuia Mkutano wa Mnyika na Waandishi wa Habari

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tuendane na teknolojia.

Haina haja ya kugombana, afanye Zoom Meeting na live streaming kila anayetaka kuuona mkutano aufuate huko.
Hv kumbe hata huo mkutano wa nishati wangeweza kutumia njia kama zoom kupunguza gharama na muda wa viongozi kusafiri. Nawaza kama ulivyowaza
 
Mbona kama hakuna uhusiano wa mkutano wa marais wa Africa na press ya Chadema? Anyway, mambo ya intelligence labda hatuwezi kujua sana.
Unadhani Chadema kama chama kikuu Cha upinzani kikitangaza Maandamano huo mkutano utaendelea?

Huitaji Akili kubwa kuelewa hili
 
Jeshi la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limezuia mkutano wa waandishi wa habari wa Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema John Mnyika uliopangwa kufanyika leo Jumatatu 27/1/2025 saa tano asubuhi.
View attachment 3215420
Nje ya jengo la Makao Makuu hayo wapo askari wa jeshi la polisi kwa taarifa tulizonazo waandishi wa Jambo TV, Azam TV, Mwananchi wamezuiwa na kuondolewa eneo hilo.
View attachment 3215428
Aidha sababu zinazoelezwa juu ya kuzuiwa kwa mkutano huo inadaiwa ni uwepo wa Mkutano wa Kimataifa wa Nishati (M300). Huku ikielezwa kuwa mkutano huo wa CHADEMA ungeweza kusogezwa mbele na kufanyika kuanzia tarehe 29.
View attachment 3215422

Sema Chadema hapa nitasema wachokozi. Yaani jengo hilo hilo kunafanyika Mkutano wa Nishati nao wanataka kuongea na waandishi? The same place? Siyo sawa. Wangeenda fanyia sehemu nyingine.
 
YAANI CHADEMA KUACHA UJI NI KAZI SANA LABDA HUO UJIN UANZE KUWAOMBA HELA, HIVI KWELI UNAONA KABISA KUNA UGENI WA KITAIFA MNAFANYA PRESS YA NINI MNASHINDWA KUVUMILIA SIKU MBILI NDIYO MUANZE HUO UJI WENU? HAMNA ADABU KABISA
Sasa kumfukuza mwehu ukiwa uchi ili upate nguo zako mbele za watu nani anaoneka chizi fresh. Hapo jeshi kwenda kuzingira jengo la chama cha upinzani kinapeleka ujumbe gani kwa hao wageni? Nani anakunywa uji hapo?
 
Jeshi la polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limezuia mkutano wa waandishi wa habari wa Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema John Mnyika uliopangwa kufanyika leo Jumatatu 27/1/2025 saa tano asubuhi.
View attachment 3215420
Nje ya jengo la Makao Makuu hayo wapo askari wa jeshi la polisi kwa taarifa tulizonazo waandishi wa Jambo TV, Azam TV, Mwananchi wamezuiwa na kuondolewa eneo hilo.

Aidha sababu zinazoelezwa juu ya kuzuiwa kwa mkutano huo inadaiwa ni uwepo wa Mkutano wa Kimataifa wa Nishati (M300). Huku ikielezwa kuwa mkutano huo wa CHADEMA ungeweza kusogezwa mbele na kufanyika kuanzia tarehe 29.
View attachment 3215422
Mimi mwenywe nimetoka na ndoo na kopo la kuogea nasema niende kuoga chooni (mtaani kwetu tunatumia vyoo vya nje), nikashangaa ulinzi shirikishi wamenizungusha, wananiambia nirudi ndani hadi wageni watakapo ondoka nchini.
 
Back
Top Bottom