Jeshi la Polisi limetoa taarifa tukio la kijana Samwaja aliye uwawa na kukatwa sehemu zake za siri na marafiki zake

Jeshi la Polisi limetoa taarifa tukio la kijana Samwaja aliye uwawa na kukatwa sehemu zake za siri na marafiki zake

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Jeshi la Polisi limetoa taarifa ya matukio matatu ya watu kutekwa/kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na kukutwa wakiwa wameuawa, likiwemo tukio la kijana Samwaja Sifael Said, Mkazi wa Kijiji cha Chalunyangu mkoani Singida kuuawa kisha kukatwa sehemu zake za siri na marafiki zake.

Tukio la kutoweka kwake liliripotiwa katika Kituo cha Polisi Makuro na lilifunguliwa jalada na uchunguzi kuanza.

Baada ya ufuatiliaji wa kina wa Polisi, zilipatikana taarifa kwa kijana ambaye walikwendakutizama mpira na Samwaja Sifael Said (marehemu) na baada ya mpira kumalizika walipokuwawakirejea nyumbani, walikutana na vijana wawili waliomwambia twende tukanywe pombe na walipoona doka pamoja hakurejea nyumbani na ndipo ndugu zake wakafika Polisi kutoa taarifa.

Soma Pia: Special Thread: Taarifa za Watu waliopotea au kuchukuliwa na “Watu Wasiojulikana”

Polisi walifanikiwa kuwakamata vijana hao wawili na baada ya mahojiano walieleza ni kweli walikwendwa kunywa pombe na marehemu na walipokuwa wanarejea walimua kwa kumnyonga kisha kukata sehemu zake za siri na kuufukia mwili wake kwenye shimo.

Watuhumiwa hao pia walieleza walifanya hivyo baada ya kuelezwa na Mganga wa kienyeji kuwa, wakipata sehemu za siri za binadamu watafuka matajiri. Polisi walifanikiwa kumkamata mganga huyo.
 
Jeshi la Polisi limetoa taarifa ya matukio matatu ya watu kutekwa/kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na kukutwa wakiwa wameuawa, likiwemo tukio la kijana Samwaja Sifael Said, Mkazi wa Kijiji cha Chalunyangu mkoani Singida kuuawa kisha kukatwa sehemu zake za siri na marafiki zake.
Hii ndo shida kwa nchi kama hizi ambazo watu wanaendekeza ushirikina kuliko kufanya kazi daah inasikitisha sana 🙆🙆🙊😔
 
Jeshi la Polisi limetoa taarifa ya matukio matatu ya watu kutekwa/kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na kukutwa wakiwa wameuawa, likiwemo tukio la kijana Samwaja Sifael Said, Mkazi wa Kijiji cha Chalunyangu mkoani Singida kuuawa kisha kukatwa sehemu zake za siri na marafiki zake.
Okay sawa, lakini wamechelewa Sana kuchukua hatua stahiki.
Wananchi wote wa kawaida wanajua kwamba 'Watu wasiojukikana' ambao wamekuwa wakihusishwa Sana na matukio ya kuteka watu, kuwapoteza na kuwaua ni hao hao Polisi pamoja na Tiss. Watu wengi huku mitaani wanatambua hivyo. Hivyo, wahusika Hawa wanatakiwa wafanye kazi ya ziada ili kuweza kuyasafisha majina yao na kuwaaminisha upya Raia kwa kuwaondolea fikra za kwamba wao hawahusiki kabisa kwa namna yoyote ile na matukio ya kuteka watu.
 

Attachments

  • IMG-20240824-WA0010.jpg
    IMG-20240824-WA0010.jpg
    73.2 KB · Views: 12
Okay sawa, lakini wamechelewa Sana kuchukua hatua stahiki.
Wananchi wote wa kawaida wanajua kwamba 'Watu wasiojukikana' ambao wamekuwa wakihusishwa Sana na matukio ya kuteka watu, kuwapoteza na kuwaua ni hao hao Polisi pamoja na Tiss. Watu wengi huku mitaani wanatambua hivyo. Hivyo, wahusika Hawa wanatakiwa wafanye kazi ya ziada ili kuweza kuyasafisha majina yao na kuwaaminisha upya Raia kwa kuwaondolea fikra za kwamba wao hawahusiki kabisa kwa namna yoyote ile na matukio ya kuteka watu.
wanahusika
 

Polisi Tanzania yatoa taarifa juu ya matukio matatu ya watu kutekwa na kuuawa​

h

Chanzo cha picha,Jeshi la Polisi Tanzania/X
Polisi nchini Tanzania imetoa taarifa kuhusu watu matukio ya watatu walioteka na kuuawa, katika mazingira ya kutatanisha nchini humo.
Hii imekuja baada ya hivi karibuni baaadhi ya jamaa wa watu waliopotea nchini Tanzania kuisimulia BBC kuhusu jinsi ndugu zao walivyopoteza maisha katika mazingira ya kutatanisha.
Taarifa iliyotolewa na jeshi hilo hii leo, inamhusu kijana Samwaja Sifaeli Said, mwanye umri wa miaka 22, aliyetoweka tarehe 8 Agosti, 2024 Singida Tanzania, na mwili wake kupatikana ukiwa umefunikiwa kwenye shimo, huku sehemu zake za siri zikiwa zimekatwa.
Kufuatia mauji ya Samwaja Sifaeli Said, taarifa hiyo inasema, wameweza kuwakamata vijana wawili ambao walikwenda kunywa pombe na marehemu, na baada ya mahojiano ‘‘waliielezea polisi kwamba ni kweli walikwenda kunywa pombe na marehemu na walipokuwa wanarejea walimuua kwa kumyonga na kisha kumkata sehemu zake za siri’’
Polisi imeendelea kusema kuwa watuhumiwa waliieleza kuwa walielezwa na mganga wa kienyeji kuwa wakipata sehemu za siri za binadamu watakuwa matajiri.
Baadaye watuhumiwa waliwaonyesha polisi mwili ambao ulitambuliwa kuwa ni wa Samwaja Said Raphael.
Polisi imetaja tukio la pili linalomhusu muathiriwa mwanamke kwa jina la Ezenia Stanley Kamana mwenye umri wa miaka 32, Mkazi wa Tandika Magorofani jijini Dar es Salaam, ambaye alitekwa/ kutoweka.
Imesema baada ya uchunguzi wake ilibaini kuwa marehemu alikuwa na rafiki yake wa kiume kwa jina Abdalla miraji@ mussa ambaye alikana kuwa na marehemu, lakini baada ya polisi kufanya uchunguzi na kupatikana kwa viungo vya marehemu, mshukiwa alikubali kuwa alimuua mpenzi wake.
Aidha tukio jingine lililotajwa na polisi katika taarifa hiyo ni la mtoto Elia Elfaza Raymond Mchome mkazi wa wilaya ya Handeni Tanga mwenye umri wa miaka 3 , aliyetoweka tarehe 9 Agosti, 2024 wakati alipokuwa anacheza nje.
Polisi inasema baada ya uchunguzi wa tukio hilo ilifanikiwa kumkamata mshukiwa Jackson Elisante @ Maeda mkazi Kwadjava Tanga mwenye umri wa miaka 23. Baada ya kuhojiwa mshukiwa akiliri kuwa mtoto huyo kumfukia ndani ya chumba anachoishi, polisi imesema katika taarifa yake.
Watuhumiwa wengine wawili bado wanashikiliwa kuhusiana na tukio hilo.
Polisi imetoa rai kwa viongozi wa kidini, wazee wa kimila , wananchi na wadau mbali mbali kushirikiana kuzuia ‘‘ matatizo haya yanayotokea ndani ya jamii’’
Polisi imewatahadharisha baadhi ya wananchi wenye tabia ya kujichukuliwa sheria mkononi, kufahamu kuwa kufanya hivyo ni kosa la kisheria. chanzo.BBC
 
Jeshi la Polisi limetoa taarifa ya matukio matatu ya watu kutekwa/kutoweka katika mazingira ya kutatanisha na kukutwa wakiwa wameuawa, likiwemo tukio la kijana Samwaja Sifael Said, Mkazi wa Kijiji cha Chalunyangu mkoani Singida kuuawa kisha kukatwa sehemu zake za siri na marafiki zake.

Soma Pia: Special Thread: Taarifa za Watu waliopotea au kuchukuliwa na “Watu Wasiojulikana”

Mbona tukio la sativa hajalitolea ufafanuzi? Sativa si alisema kwamba alipelekwa kuteswa Oysterbay?
 
Mbona wanaotekwq ni wengi mno kwa mjibu wa TLS mbona taarifa hazitolewi. vipi?
 
Back
Top Bottom