Mbona ni jambo la msingi sana kwa hawa wapinzani Maslahi koko kupata kipigo cha mbwa quoquo .
Au mlitaka nani apigwe kama sio mpuuzi mmoja na genge lake lisilo na uelekeo wala tija kwa siasa za mageuzi zaidi ya kutumia siasa kupiga pesa na kula rushwa za watawala huku wanyonge wakikosa mageuzi ya Kweli kwenye nchi .
Hivi kwa Mwana siasa mwenye kujua kuwa watanzania Tangu mwaka 1995 walikua wanataka mabadiliko na kupinga ufisadi wote chini ya NCCR mageuzi ya Mrema mpinga magobachori atapata vipi shida ya kuikabili CCM iliyokataliwa tangu miaka 32 imiyopita.
Nini kinadhoofisha mageuzi au demokrasia hasa ya kupiga kura kama sio wapinzani wenyewe ?
Mwenyekiti amekamatwa wa chama chenye wanachama zaidi ya mil. 8 halafu Kuna msemaji wa chama amejificha darini au uvunguni mwa kitanda cha anatuma kimemo analiomba jeshi la polisi eti limwachie haraka .
Blaliful !!! Hapa mnategemea mageuzi au kugeuzwa nyie.!!
Wajeenger kabisa !!!
.Yaani tulitegemea Mrema awatoe wanachama mil. 8 wote wakajiunge na mwenyekiti wao huko polisi na magerezani na wakatae kabisa kuachiwa . Yaani wagome kutoka ndani hata kwa dhamana . Wakatae dhamana na pasiwe na mtu wa kuwawekea dhamana na wakitaka kuwatoa ndani wakatae waombe kwenda gerezani na huko wakatae kupewa dhamana ili kwa mara ya kwanza mabomu yapigwe ndani ya mahabusu kuwalazimisha watu kutoka vifungoni .Je,serikali itawafungulia kesi watu mil. 8 na kuwafunga gerezani kwa kosa la kukataa kutoka kwenye mahabusu au gerezani?
Kwa sababu CCM inatumia polisi kuwatisha kwa sababu mnaogopa kulala ndani wakati kifo cha wengi ni harusi.
Nendeni mkashangilie na kuandamana ndani ya lokapu ili dunia ione kuwa kweli mnapigania demokrasia ya kweli sio blablah za kuogopa kukamatwa hadharani bila kosa . Huna kosa unaogopa nini kukaa hata gerezani .?
Walevi na wahuni wakubwa ndio maana hata mbinu zenu hazileti mwamko wa kimapinduzi mpaka sasa Watumishi wa Mungu ndio wanapigania uhuru wenu nyie wanasiasa mliojaa hila na usanii huku mkiwa lnakesha kwenye starehe wakati kuna watu wanaumizwa na kufa kwa ajili ya kujenga vyama vyenu?
ACT wameanza kutambua nguvu za kumtanguliza Mungu kwenye wakati huu wa utawala wa giza.
Nyie akina wa Chadema endeleeni kukesha na KVanti na watoto halafu mnataka kuwa juu ya nchi muwatawale wafu na rasilimali zilizoumbwa na Mungu wakati shetani aliona zikiumbwa na akatamani sana yeye ndio apewe nafasi ya kujiundia utawala wake na mifumo na majeshi yake na ukuu heshima kubwa kama alivyopewa binadamu !?
Lisu na Mbowe acheni kulewa kabla ya kupanda kwenye majukwaa mnapoteza nguvu za kiroho.
Mbowe acha starehe za kitoto huu ni wakati wa kujitenga na anasa na kujiweka wakfu kwa Mungu na hata mizimu ya Tanganyika ili kuinua roho za ujasiri na haki kwa Taifa .
Vinginevyo mtapata tabu sana na mtapigwa kipigo cha mbwa koko.
PHEW!
Nimekosa alama sahihi ( kati ya zilizopo) ya kuweka kwenye bandiko hili baada ya kulisoma. Kwenye aya za mwanzo kabisa nilikuwa nashangaa ni nini kilicho mpata mwandishi hadi kubadilika na kuwa na fikra za namna ile; kwani mara nyingi humsoma tofauti na ilivyo kuwa kwenye aya hizo.
Lakini kadri nilivyo endelea kusoma, humo katikati ya andiko lenyewe, nikatamani niishie hapo na kulipa andiko hilo alama ya 'love' hata kabla sijamaliza kusoma andiko zima.
Nikaona nijipe moyo, nisome lote hadi mwisho kabla ya kuamua nitoe alama ipi.
Huku mwisho, pamoja na kuwa bado nina kumbukumbu ya kilicho andikwa humo katikati, nikazidi kuchanganyikiwa; ingawaje 'theme' ya maneno mazito yaliyo tumika hapo katikati ikiwa bado inatawala akili zangu!
Kwa hiyo, siwezi kutoa alama ya "Mshangao, au Masikitiko, ama ya Huzuni na wala siyo ya "Kutopenda" andiko hili
Ila bado naona uzito mkubwa wa ujumbe ulio bebwa ndani yake.
Kwa mfano: Kama kweli CHADEMA wanao wanachama wao milioni nane (milioni 8); ongeza kwenye namba hiyo na wapenzi tu wa chama hicho, ambao siyo lazima wawe wanachama.... Unaelewa maana ya kuwa na wafuasi kiasi hicho? Ummati wa watu hawa; hata kama kati yao wawe milioni tatu tu hivi, ambao kwa kila hali wapo kupigania chama chao----. Unaelewa kinachofikiriwa hapa?
Sasa basi, kama hawa watu hawastuki, wala hawajisumbui kabisa hata wakati viongozi wao wanapo pata masaibu, tena kwa uonevu kabisa; tuwachukulie vipi wanachama na wapenzi hawa wa chama?
Ni nani alaumiwe hapa, wanachama kukosa mwamko, au viongozi kutowaamsha wanachama wao waone kwamba wanayo nguvu ya kupigania haki zao na viongozi wao!
lakini dalili zimeanza sasa kubadilika kidogo, hasa kutokana na uchafu mwingibunao fanywa na viongozi wa CCM na pia baadhi ya viongozi ndani ya CHADEMA kuanza kuonyesha dalili za kuaminiwa na wanachama wao na waTanzania kwa jumla
Mwisho, nirudi kwa mwandishi wa andiko, mkuu '1000Digits'. Napenda kukupongeza kwa fikra ulizo wasilisha kwenye andiko hilo. Sisi sote, kutokana na 'frustrations' za kutojuwa nini cha kufanya mbele ya majaribu makubwa haya yanayo letwa na CCM na vyombo vyake vya dola, mara nyingi hujikuta tunalaumu, hata wakati hatuna njia za kushauri kipi kifanyike kuyaondoa haya yanayo chafua nchi yetu.
Natoa 'love' mbili mfululizo kwa andiko la mkuu 1000 digits'.