Pre GE2025 Jeshi la polisi watanda Ruanda Nzovwe kudhibiti maadhimishi ya Bavicha

Pre GE2025 Jeshi la polisi watanda Ruanda Nzovwe kudhibiti maadhimishi ya Bavicha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Snapinsta.app_455027605_1516122285667272_5159461134856069549_n_1080.jpg

Askari wa Jeshi la Polisi wametanda katika Uwanja wa Ruanda Nzovwe, jijini Mbeya kulipopangwa kufanyika maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani yaliyokuwa yameandaliwa na Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha).

Maadhimisho hayo yalikuwa yafanyike leo Jumatatu, Agosti 12, 2024, lakini Jeshi la Polisi kupitia kwa Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Awadh Juma Haji lilitangaza kuyasitisha baada ya kutilia shaka tukio hilo akieleza kutokuwa rafiki kwa mustakabali wa nchi.

Soma Pia: Jeshi la Polisi lapiga marufuku mkutano wa BAVICHA siku ya vijana duniani

Polisi ilitangaza uamuzi huo ukitanguliwa na barua ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kwenda Chadema ya Agosti 8, 2024 kukitaka kusitisha shughuli hiyo, kwani lugha za viongozi wa Bavicha zinahatarisha usalama na zinakiuka sheria.

Mwananchi imefika eneo la Uwanja wa Ruanda Nzovwe na kushuhudia idadi kubwa ya polisi wakiwa na bunduki pamoja na gari la washawasha, huku wakiwa wamezunguka kona zote za uwanja huo.
 
Hawo policcm na wanaowatuma na wanaoshabikia wote ni wapumbavu.
 
Wanatumia nguvu sana kwa vitu ambavyo haikutakiwa kutumia nguvu akili tu sema ndio hivyo..
 
Hii nchi bado inatawaliwa na Chama kimoja, upinzani na demokrasia ni danganya toto.

Huko Zanzibar ccm walijazana hukusikia polisi, ACT pemba hukusikia polisi, Ridhiwani Kikwete Leo Dodoma na vijana husikii polisi ila Chadema tayari polisi inaingia front kukamata viongozi na kukamata mamia ya vijana.
Hongera serikali ya CCM kwa 4R alisikika Mwashambwa
 
Ccm endeleeni hivyo hivyo ata makaburu walikaza hivyo hivyo lakini leo hatunao
Kuna siku hao policcm hawatatosha kuzuia wananchi ni suala la muda tu.
 
Back
Top Bottom