Jeshi la Uhamiaji wamenirudisha Nyumbani wakidai sipo Fiti. Nimepoteza dira ya maisha

Pole sana ,mimi ilinikuta changamoto kama hiyo miaka ya nyuma, nilijiunga na jkt kwa kujitolea miaka miwili, siku mkataba unaisha na sisi wengine tubasomwa majina tunarudi nyumbani wenzetu wanaenda kozi msata, hakukuwa na namna zaidi ya kuukubali ukweli na kurudi nyumbani. Nikajipanga upya na maisha yakaendelea.

Ushauri wangu kwako ni kukubaliana na ukweli na ujipange kwa maisha mengine huko achana napo, nakwambia hivyo kwa sababu wapo wengi tulimaliza nao mkataba ila hawakutaka kukubaliana na hali wakaanza kuforce kurudi kambini kwa kuhonga wakaishia kuliwa pesa na kupoteza muda.
 
Yah kiukweli Biashara ni passion yangu, huku kwenye ajira nahangaikia kwa ajili ya kupata mtaji uliosimama
 
Upo tayari kujilipua kufanya kazi nje?
 
Kwanza pole sana mkuu, je jeshini wanaruhusu kuingia mtu aliyeishazaa kujinga na jeshi? Labda hilo ndilo tatizo. Lakini kwa sasa siyo hoja hiyo nadhani wahotaji msaada zaidi jinsi ya kusonga mbele.
 
Aisee, Huyo kweli Mungu alimpangia kuwa mwanajeshi
 
Bongo nyoko sana hii nchi, inahitaji mapinduzi ya kijeshi . Mtu ana shahada ya maabara ya kisayansi anakosa kazi kweli??? wakati hizo ndio kazi muhimu ughaibuni. Halafu utamuachishaje mtu kozi kienyeji hivyo ???
Ushauri wangu wa bure; usipanic sana na kupoteza matumaini, tulia chini anza tena upya kupanga mipango yako wapi pa kuanzia ikibidi hata tafuta mkopo kidogo wa kuanzia ili ujiinue taratibu. USIKATE TAMAA miaka ulionayo ni bado mdogo sana, kumbuka Life begins at 40. Kila la kheri.
 
Kwanza pole sana mkuu, je jeshini wanaruhusu kuingia mtu aliyeishazaa kujinga na jeshi? Labda hilo ndilo tatizo. Lakini kwa sasa siyo hoja hiyo nadhani wahotaji msaada zaidi jinsi ya kusonga mbele.
Kweli kwa Sasa msingi ni Uhitaji wake.Ila nimejaribu kufuatilia ni kwamba kama watu waliokwishazaa huwa hawataki kwenye vigezo vyao kama sijakosea Wataalamu wanaweza kuja.Na wengi wao huwa wanaondolewa wakiwa Vyuoni kwenye kozi.Ndio maana nilimuuliza walikagua Maungo yake kipindi amefika chuoni kwenye comment yangu Hapo Juu...Maaana hapa ndipo nahisi Unfit ndio ilipotokea...

Members yoyote mwenye kuweza kumuunganisha viwanda vya Chanjo,na Maabara zinginezo ufanyike msaada,hasa viwanda Pwani Kule,Silverlands,Ester na kwingineko kwenye Maabara,maana Huyu ni mtaalamu chochote kile akifundishwa hasa cha Maabara atafanya.
"Yote kwa yote Mungu ni mwema sana,kila jambo lolote liwe zuri au Baya linapotokea shukuru Mungu,pengine Uhamiaji haikuwa ridhki na ridhiki yako ipo mahali pengine,Kikubwa kutokata tamaa tu na Huku ukimtanguliza Mungu.
 
Pambana mdogo wangu.

Hiyo ni changamoto ya kawaida sana kwenye maisha.

As long as una afya njema rudi kwenye biashara yako ya nafaka, hata kama utaanza kwa kuchukua mzigo kwa mali kauli kwa wale uliokuwa unafanya nao huko mwanzoni.

Jitahidi kuwa consistent na focused pia, ukiamua kufanya jambo moja simama nalo bila kuwaza waza options zingine.. Hapa wengi huwa tunafeli sana. Omba kwa Mwenye enzi akujalie Subra na Uvumilivu kwa kipindi hiki.

Have hope, despair is for the defeated..
 
Mkuu shukuru mungu kwa kila jambo,japo ni ngumu kwako kukabiliana na Hali hiyo ila tambua kuwa kila Jambo linalotokea hapa duniani lina sababu zake,

Amini hili halikuwa fungu lako,la kwako bado lipo linakuja,na tambua mlango mmoja wa riziki ukijifunga kuna mwingine utafunguka.

Nina mifano mia kidogo juu ya ukuu wa mungu,kuna jamaa moja alikuwa mwalimu mwenzangu,tumefundisha naye kwa miaka kama mitano hivi,baadae akawa amefukuzwa kazi,jamaa yule alitaabika sana,ila uzuri kwao walikuwa njema kimaisha ,wakamtafutia kazi jeshini na akapata ila kigezo kikawa atumie elimu ya darasa la Saba kuingia jeshini ,jamaa alikataa kwakuwa alikuwa na digrii yake,


Mwaka mmoja baadae akawa anajihusisha na uimbaji wa nyimbo akitumbuiza kwenye makumbi na kwenye masherehe kwa malipo kiasi,mwisho wa siku akawa amepata wadhamini wazungu wa kumpeleka ulaya kwajili ya shughuli za mziki kwani alikuwa mtaalamu sana na upigaji gitaa pia,na maisha aliyapatia sana akawa ananiambia kipato chake kilikuwa Mara tano ya mshahara wa ualimu alokuwa akilipwa,mpaka naongea hapa jamaa sio wa level zangu za ualimu,yuko juu sana.

Mkuu relax na nakuambia fungu lako lipo na ni kubwa sana ,tambua dhahabu ili ing'are lazima ipite kwenye moto, relax dear
 
Hakika kila mtu ana historia na hii nimepata funzo na Mimi pia.Hakika kila jambo lina makusudi yake
 
Kumbe kuna mtu alikuunganishia kwamaana ya kwamba ulitoa hongo hi bongo inanuka rushwa balaa. Ila yote kwa yote pole sana kwa maswahibu yaliyokupata
Bongo hadi kule Masijala ukitaka file lako lazima utowe kitu kidogo! Ila Kama kweli ni haki yako basi usikose hata buku mfukoni,wataipokea kwa Masimango lakini kazi yako watakufanyia kwa haraka!!
 
Afya na ualimu zimetoka nafasi za Kairuki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…