JF Exclusive: Wawindaji tuliowauzia wanyama na ardhi yetu tukichekelea!

Hawa nao wamewekeza nini? Maana wanachovuna hawajakileta wao wala hawajaongeza lolote kwenye kilichopo. Labda wameajiri manamba wa kuwasaidia na kuwafulia nguo

hawa ni wachukuaji na sio wawekezaji, ni kama vile tu wale wa madini
 
umasikini ni balaa ndugu yangu,masikini hatuwezi hata siku moja kufurahi tukimuona mtu anatumia kipato chake alichojaaliwa na mungu.mwarabu na pesa zake za mafuta kaja kutumia,tunamchongea ngenga pia ,haya kipi cha kwetu kaiba? sanasana kaongeza mapato ya utalii.hawa si ndo tunawaita watalii jamani?
 

Usinilazimishe nikafuata fikira zako kwasababu sikujui... Mahakama gani unayoiongelea wewe na ipo wapi ? Nachoandika hapa naandika kwa vikira zangu..! Nilishawahi kukwambia naabudu wazungu au unataka kuonyesha udhaifu wako kwa wazungu hapa ? usi copy post za watu kama huna cha kuzungumzia binafsi..!!
 
Dah jamaa wanatesa jamani mwenye pesa sio mwenzio tutaishia kuwaangalia tu na kuwapigia magoti.
 
Nimekubali, i thought sisi tunaoenda serengeti na arusha kula bata tunaona dili kumbe nchi inawenyewe....wameniacha hoi na hiyo vx convertible sijawahi ona! Tukubali matokeo hao ndo wenye nchi...wameuziwa na mikataba wanayo ya ushaidi tumekwisha!!
 
Mimi namuunga mkono kwa ndugu aliojibu kama hao waarabu hawakuingia kwa wizi bali kwa kibali maalum toka serekalini.Sioni sababu ya kukereketwa na kuwepo kwao nchini,isitoshe unajua kama fedha ngapi ya geni imeingia nchini?
kama ni halali basi hata siku wakipewa ikulu itakuwa halali tu
 
Tatizo ni wageni au uwarabu wao?mbona kuna wazungu wanazeekea tanzania na wameshatia mimba dada zetu wengi tu huchukii?
 
Tuache chuki jamani,mbona wazungu huwataji?au hujawaona?
 
Mambo safi kabisa - hawa jamaa nasikia wakija nchini wanatumia dola bila ubanizi zao na Tanzania inafaidika sana. Kuacha malipo ya kumiliki eneo hilo. Tunahitajia watu kama hawa.
 
kamuulizene mwinyi kwani yeye ndio aliyeuza hiyo mbuga,,,,,msibishane mkaumizana hawa jamaa wanatua na ndege yao na kuondoka kuna uwanja mkubwa tu ndege zinatuaga pale.....hakuna cha kibali wala nini wale walishauzi eneo hilo huwa wanakuja na kuwinda na kuondoka.....TULAUMU SERIKALI YETU YENYE VIONGOZI WASIO NA AKILI.....
 
Lawama zangu zote ni kwa viongozi wetu. Mimi siwalaumu hao waarabu. Ni upumbavu na ujinga wa viongozi wetu wanaoruhusu watu wageni kutanua hivyo bila kulipia vizuri.
 
Kazi ya M k w e r e hiyo amepewa madaraka na nguvu asizojua kuzitumia yeye amezoea utumwa alioridhi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…