Jf Hard Talk "Mwifwa"

Jf Hard Talk "Mwifwa"

Nilipokuwa O-level nilitamani niwe Mhandisi maana nilipenda nikasome PCM A-level.

Uwezo wangu kwenye masomo ulikuwa wa kawaida.

Wakati wa hatua za mwisho kumaliza mtihani wa NECTA form 4, tulipoanza kujaza comb na shule za Advance ambazo tutachagualiwa tukifaulu.

Nilianza kwa kuchagua comb ya PCB kwa kuchagua Ilboru kama chaguo la kwanza, lengo likiwa nikichaguliwa hiyo shule kwa comb ya PCB, baadae nikabadili niende PCM(maana nilifanya utafiti mdogo nikagundua unaweza kuwa na ufaulu wa One ya kawaida na unaweza kuchaguliwa shule kubwa kama Ilboru, Mzumbe, Kibaha, Tabora Boys kwa PCB)

Lakini mambo yakawa tofauti, nilichaguliwa shule nyingine ambayo sikuitarajia japo niliichagua kwa comb nyingine.

Wakati naenda kuanza Alevel nikaambiwa nibaki PCB maana nitasoma mambo ya Afya nikifika chuo endapo nitafaulu, basi hadi hapo nikabaki na PCB na nikakomaa kufanya juhudi za kufaulu(nilisota sana) hadi nikafanikiwa na nikafanikiwa pia kusoma mambo ya Afya.

Bila shaka nitakuwa nimekujibu.
Dah PCB nataka nikufuate mkuu.
 
Shukran kwa kujitokeza na kutoa majawabu baadhi ya maswali uliyoulizwa.

Nina maswali machache waweza kuyajibu kwa lugha yoyote Swahili au English.
1.What important truth do very few people agree with you on.. ?

2. How long will you be remembered after you die..?

3.What two questions would you ask to get the Most information about who a Person truly is..??

4.What is the purpose of life..?

5.Fikiria kama ungekuwa na uwezo wa kuanzisha Taifa/Nchi.
Nchi yako ingekuwa ya namna gani..?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uongozi ni hekima, busara na upendo kwa wote anaowaongoza.

Najisikia vibaya sana.
Hili jambo serikali inatakiwa iliangalie kwa umakini sana.

Kusoma kozi za Afya hasa kwa MUHAS bila kuwa na mkopo/boom/au mfadhili mwingine(halafu ujigharamie mwenyewe hasa kwa mwananchi wa kawaida mwenye kipata kidogo na sio tajiri) ni hatari sana.

Mimi nilikuwa na mkopo asilimia zote lakini shule ilinipeleka puta sana(japo tunatofautiana kiakili) hadi nikasahau kula bata kama jinsi nilivyotegemea[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
@mwifwa Mkuu kwa nini PCB ilikupeleka puta?
Mana aiseeee..
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Unaruhusiwa kuuliza muda wowote swali lako, utajibiwa
Mkuu Mwifwa. Nataka niingie advance kupiga PCB kama mdogo hapa hadharani unsnishauri nini?

Ni ipi siri ys kufaulu PCB advance?
 
Back
Top Bottom