JF HARDtalk na "Mshana JR"

JF HARDtalk na "Mshana JR"

Mshana Jr ukiwasili tu, ndani ya uzi huu..
Ili kupunguza maswali common tupe majibu ya particular zako muhimu kama ifutavyo;

Jina: as mshana jr

Umri: unaweza toa hata group age yako.

Jinsia: yako nadhan inajulikana

Kazi: kazi yako pia ni muhimu, ili swali lije direct tujifunze kazi wana JF.

Kabila: lako

Marital status: umeoa au huja owa, na unakaa na mke wako?, Pia una watoto toa idadi ukiweza.

Resident: unakaa kwako au kwa mtu, au umepanga?

Hapo tutaenda vizur, maswali yatakushukia vizur hadi utapenda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Jina sahihi kabisa
Umri above 30 marital status married with 2 kids
Mwajiriwa na mjasiarimali
Naishi Pwani

Jr[emoji769]
 
OK mshana ni kweli kwamba familia nyingi za kitanzania haziamini na hazipendi maswala ya uchawi,swali kwa nn mada zako nyingi zinahusu uchawi ? Na Je ww n mchawi ?au umerithi uchawi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Uchawi ni kama cancer umeenea sana... Naamini uchawi upo lakini siamini katika wachawi na waganga wa kienyeji... Wengi wao ni matapeli na waganga njaa
Mimi sio mchawi ni mlokole mcha Mungu mwenye elimu ya uchawi ushirikina na ulozi

Jr[emoji769]
 
Mshana Jr , ( 1 )ni nini kilichokuvutia mpaka kuwa mshirikina au kwa nini unapenda masuala ya kishirikina kulingana na mada zako kedekede za masuala ya kishirikina humu JF? , napenda mkaangwaji wa kesho awe Ontario

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi sio mchawi na sijawahi kuroga lakini ili kufikisha ujumbe ilinibidi kuvaa uhusika... Nina elimu kubwa na ufahamu juu ya uchawi ushirikina na ulozi hivyo najua ninachomaanisha

Jr[emoji769]
 
Mshana Jr ubongo wako umeshiba mambo mengi sana, nini siri ya mafanikio?

Sent using Jamii Forums mobile app
Uchawi ni kama cancer umeenea sana... Naamini uchawi upo lakini siamini katika wachawi na waganga wa kienyeji... Wengi wao ni matapeli na waganga njaa
Mimi sio mchawi ni mlokole mcha Mungu mwenye elimu ya uchawi ushirikina na ulozi

Jr[emoji769]
Sijawahi kuroga ila nimewahi kuwafanya vibaya walionikosea pakubwa...
Elimu yangu ya uchawi ni kipawa binafsi

Jr[emoji769]
Je ulishawahi kuwa mfanyakazi wa kuhudumia wapendwa wetu waliotangulia mbele za haki(Mochwali) kama mwenyewe unavyojinasibu kwenye nyuzi zako mbali mbali?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi sio mchawi na sijawahi kuroga lakini ili kufikisha ujumbe ilinibidi kuvaa uhusika... Nina elimu kubwa na ufahamu juu ya uchawi ushirikina na ulozi hivyo najua ninachomaanisha

Jr[emoji769]
Hiyo elimu umeipata wapi? Darasani, umejifunza kwa wachawi wenyewe au umefunuliwa kwa njia ya roho mtakatifu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom