Nimepitia maoni yenu wote, kwa mlionipa pole ninawashukuru sana. Ninaomba pia niweke wazi mambo yafuatayo
1. kuhusu kuonana live tulishaonana na alionekana ni innocent na mcha Mungu kwa maneno yake, pia kwa muonekano sio mtu mbaya au anayeonesha kuwa na tabia mbaya
2. Kwa waliokazia kuhusu ulaji wa tunda, sina haja ya kumdanganya mtu nisiye mjua na asiyenijua ukweli ni huo kwamba kamwe hakuwahi kuuona utupu wangu na kwa hilo siko na sikuwa mrahisi kwa yoyote yule. Kwahiyo kama wewe unalazimisha kuamini hivyo wewe amini tu upendavyo ila tunda ni langu na halikuliwa.
3. Watu hukutana popote na kufanikiwa kuwa na mahusiano yenye manufaa tu, hivyo kukutana na mtu online, street, kanisani au kwingineko hakucount ila ni aina ya mtu uliyekutana naye ndio inacount.
4. Hata kama ingekuwaje, bado ingekuwa vigumu kwa mimi kujua mambo ya mahusiano yake kwani mpenzi wake yuko mkoani kama nilivyokwisha elezea kwenye post yeye ndiye anayejua wanawasiliana lini na kwa namna gani.
5. Hii post iko hapa ili kuwapa somo wengine ambao kwa njia moja au nyingine wana mpango wa kuanzisha mahusiano ili wawe makini na kutojirahisisha kabla ya kujuana kwa undani iwe online, street n.k.
Otherwise michango yenu wote kwa upande mmoja au mwingine inajenga kutegemeana na nini unaamini as far as relationship is concerned.