JF is my homeland

JF is my homeland

Mkuu ngumbuke nakuunga mkono, mara nyingi ukweli kwa maana ya fact huwa mgumu kweli.Kwakweli kama kuna uwezekano wa kukusanya mtaji hapo ulipo please do it. mimi pia nawashukuru hawahawa waajiri. ugumu nilioupata umekuwa somo tosha kwangu, ila pia kiukweli sehem ya mtaji imetoka hapohapo. whether nilisave mshahara ama nilitumia mkataba wa ajira kama dhamana ya mkopo, fine tu. ila hili la kuchoma meli moto liko independent kidogo. zamani nilikuwa nikiona wafanyabiashara waliofanikiwa nadhani ni miujiza ila sasa najua ukweli, ni commitment inatakiwa because kiukweli ukilegea unaanguka mbona?[/QUOTE]
Kaka Ngamakisi, ninamshukuru Mungu kwamba hapa nilipo uwezo wa kukusanya mtaji mdogo wa kuanzia upo. Hata sasa ninapochangia mada hii, nimeshawasiliana na rafiki zangu wawili, mmoja alikuwa na wazo la kuendelea kuajiriwa kama nilivyo mimi ( sasa nimebadilika ), alipata kazi ya uhadhiri huko Makumira mwishoni mwaka jana, kwa mshahara wa 1.8 monthly,jamaa yake mmoja akampa shule ya kilimo cha mpunga na vitunguu( huko lumuma Kilosa). Huyu ndugu yangu sasa najihisi aibu kuongea naye.
Kwa sasa ninajipanga kwenda Lumuma kwa mwongozo wa huyu ndugu au Bagamoyo, bonde la mto Ruvu kuna jamaa mwingine ameanzisha kilimo cha vitunguu septemba hii.
Nina hakika sitokosa 3m ya kuanzia by feb 2014 nikishalipa ada za wanangu wawili. Mungu atutie nguvu na tuendelee kuelimishana na kutiana moyo.
Hakika kila kitu ni kuthubutu na kuwa tayari kwa matokeo kwani ni kweli hao matajiri tuwaonao na kuwashangilia kila siku walithubutu na kuwa tayari kwa matokeo yoyote yale. Sisi bado tumejawana woga na kibaya zaidi tunafikiri kuajiriwa ndio MAUJANJA!! Kumbe hakuna kitu.
 
habari zenu wana jamvi hili la ujasiriamali. kwa muda mrefu sana nimekuwa nikipita JF kama visitor tuu na sio user..ila ikafika kipindi nikaamua kabisa kuwa member.
My regret ni kwamba why didn't i know this site earlier? JF is so useful, has been so to me in one particular way.

tangu siku nyingi sana huwa najiona kwamba hii mambo ya kuajiriwa is not for me at all..nakuwa kwenye ajira kwa kujilazimisha sana ili kusudi angalau baadhi ya mambo yaende sawa..lakini siko comfortable. msahahara haukidhi, mazingira ya ajira somehow negative, room ya growth huioni(ni mpaka labda upate bahati ya kuwa na immediate supervisor ambae ni brilliant) habari ya savings ndo kabisa, ie never achieved

nimesha attempt several projects lakini zimekufa njiani, lakini haikunikatisha tamaa kwani najua wazi source ni nini--lack of close supervision. mimi nionavyo hakuna mjasiriamali mwajiriwa, hakuna..you cant be both(hapa naomba tuzingatie maana halisi ya ujasiriamali). so baada ya kuridhika na analysis yangu mwenyewe ofcourse na msukumo kutoka hapa jukwaani, nikafanya what everyone called me crazy, nuts, a fool,whatever! yes even my family. I simply said it was enough and quit my job. that was April 10 mwaka huu huu.

napenda sana kufuga kuku, mama yangu alikuwa mfugaji mwenye bidii, kweli kabisa pasipo my mom kufuga sijui kama mlango wa shule ningeuona. so nikaamza na kuku wa nyama, broiler. nili battle sana na swala la idadi, kuna wanaokuambia anza na wachache kama mia 2, wengine mia tano..ila mimi nikastick na imani yangu ya kijasiriamali---hakuna kuogopa wala hakuna kujaribu...nikanunua vifaranga elfu moja(by that time nimejenga chumba na sebule....still unfinished. nalala chumbani, nafugia sebuleni.niliwalea wale vifaranga kwa kuzingatia sana ushauri wa kitaalam, nina rafiki mama mmoja mtuzima kuliko mimi naye mkongwe wa kufuga alinisaidia sana. Katika vifaranga elfu moja walikufa watatu tu. ila inataka umakini. nilikua sitokitoki nyumbani ovyo, usiku ndo kabisa namonitor joto bandani. nilikuja kuuza jumla ya kuku 997. nilipata faida nzuri, nilifurahi lakini nilisikitika pia. nilijilaumu nilikuwa wapi siku zote..nimepoteza muda wangu mwingi in mylife kutumikia waajiri kwa stress nyingi, mambo za deadlines, targets, eeeh.

Kwahiyo mpaka sasa bado nafuga hao hao 1000, sijaongeza idadi, nakusanya mtaji vizuri, na pia nikwasababu banda langu ni dogo. naendelea kujifunza pia na mbinu nyingine za kupunguza gharama za uendeshaji. na pia ni commitment, sio kitu kidogo inabidi kujitoa hasaa. huwa nasoma comments za wakongwe wa ufugaji na kilimo huku jamvini naona kama they are speaking my mind! ujasiriamali is tough work but its profitable...kikubwa zaidi ambacho mimi najivunia, ni the fact kwamba im actually producing, selling my produce and making that money...i couldn't be prouder guys! kitu kingine imenifundisha sana kuwa mwangalifu wa matumizi, im so eye opened in this nowadays..

Lengo la kuandika post hii ni kukupa moyo wewe ambae unajijua ni mjasiriamali na unatamani sana kupractise, wacha kusita,risks zipo lakini kumbuka hata kwenye kuajiriwa risks pia zipo, tunazioverlook ili kujidanganya. Nisikuboe sana mpendwa, chamsingi fanya maamuzi. Napendaga kale ka slogan ka "kuchoma meli moto''.

LONG LIVE JAMII FORUM



nakupa moyo sana ngumbuke, ukiamua kwa dhati hakika utaweza. hii nchi imejaa fursa we usipime. huoni wageni wanavyoikodolea macho,ona hata viongozi wetu walivyochanganyikiwa mpaka wamebaki kununua ma ekari ya ardhi kila uchao? kila kiti kiko hapa nyumbani. utavuka amini.
 
nakupa moyo sana ngumbuke, ukiamua kwa dhati hakika utaweza. hii nchi imejaa fursa we usipime. huoni wageni wanavyoikodolea macho,ona hata viongozi wetu walivyochanganyikiwa mpaka wamebaki kununua ma ekari ya ardhi kila uchao? kila kiti kiko hapa nyumbani. utavuka amini.


Kaka Ngamakisi, nashukuru mno kwa kunitia moyo. Yaani sasa najiona kama kijana mmojawapo mwenye mafanikio hasa nisomapo topic hii na ile ya Eberhard.
Pia ongezea michango ya wataalam kama akina Chasa, Malila, Mama Joe na wengineo.
Kwa mijadala hii na mawazo ya kimaendeleo kama haya miongoni mwetu vijana hasa tunaoteseka katika ajira za sekta binafsi, mimi sasa ninauona mwisho ulivyo mzuri na watoto wangu watakavyokuwa na furaha na raha kwani baba yao nitakuwa nimewaandalia kilichochema!

Asanteni sana wana JF!
 
Hongera Mkuu kwa ujasiri wa kuthubutu kuacha kazi na kujikita kwenye ujasiriamali.Wengi wetu tuna hofu ya uthubutu ,tumeng'an'gania mishahara ya mwisho wa mwezi..Nashukuru umenipa moyo kupitia post yako.
 
one day yes!
bado nina changamoto 2 kubwa (sina umeme na sina uzio) but with time nitapata solution tu.

I just cant wait!
 
Back
Top Bottom