JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

Mnamo mwaka 1979 ilitengenezwa Meli yenye uwezo wa kubeba kakribani Tani 850 za mizigo pamoja na idadi ya abiria wasiozidi 430, na kupewa jina la MV Bukoba. Meli hiyo ya MV-Bukoba ilikuwa ikifanya safari zake kati ya Bukoba na Mwanza kupitia Ziwa Victoria.

Mwaka 1996 mwezi Mei idadi ya abiria zaidi ya 1000 na wafanyakazi wa meli hiyo zaidi ya 40 waliagana na marafiki, ndugu na wapenzi wao tayari kabisa kuanza safari kuelekea jijini Mwanza kutoka Bukoba, safari ilianza vyema na kwa amani kabisa huku abiria wote wa Meli hiyo wakiwa na shauku ya kuonana na ndugu, rafiki na jamaa zao walioko jijini Mwanza.

Mmoja kati ya abiria waliokuwemo ndani ya Meli hiyo ya MV-Bukoba ni mama mzazi wa Mwanamitindo maarufu Duniani, Fraviana Matata. Wakati safari ikiendelea mambo mbalimbali yalikuwa yakiendelea ndani ya meli hiyo kama kusali, kucheza muziki na wengine walijikuta wakipata wapenzi wapya ndani ya Meli hiyo.

Robo tatu ya safari ya MV-Bukoba ilikamilika na abiria wa meli hiyo walikuwa tayari kwa kujiandaa kushuka wengine waliwapigia ndugu zao simu kuwa walikaribia kufika kwasababu ni kilimota 30 pekee zilibakia Meli hiyo kufika nchi kavu.

Yalipofika majira ya alfajiri tarehe 21 mwezi Mei mwaka 1996, Meli hiyo ya MV-Bukoba ilitoboka kutokana na uzito uliokuwa umeizidia na kuanza kuruhusu maji kuingia ndani ya meli, sababu iliyopelekea meli hiyo kuanza kuzama taratibu ikiwa imebakiza kilomita 30 pekee kufika nchi kavu.

Abiria zaidi ya 1000 waliokuwa ndani ya meli hiyo hawakuamini kilichotokea akiwemo mama yake Fraviana Matata na kutokana na upungufu wa vifaa vya kuokolea ndani ya meli hiyo abiria wengi ilibidi watumie uwezo wao binafsi kujiokoa kitendo kilichopelekea abiria wasiojua kuogelea kufa maji na hata wale wenye ujuzi wa kuogelea ilifika mahali wakachoka na wengi wao kufa maji pia.

Uwanja wa Nyamagana ambao mara nyingi ulikuwa ukitumika kama uwanja wa michezo siku hiyo ulitumika kuwa sehemu maalumu ya kupokea miili ya wapendwa wetu waliokufa maji ndani ya meli ya MV-Bukoba pamoja na wale waliookolewa wakiwa hai ndani ya meli hiyo, jiji zima la Mwanza na Tanzania kwa ujumla ilipoa kwa siku kadhaa kufuatia ajali hiyo inayosemekekana kuwa ni moja kati ya ajali kubwa duniani zilizowahi kutokea majini.

Miili ya abiria 391 iliopolewa watu wakiwa wamefariki tayari huku miili ya abiria 114 pekee iliokolewa ikiwa hai na zaidi ya miili 495 ukiwemo mwili wa mama yake Fraviana Matata haikupatikana, tuendelee kuwakumbuka na kuwaombea ndugu zetu waliofariki katika ajali hii ya MV-Bukoba kila ifikapo tarehe 21 ya mwezi Mei kila mwaka.

 
Najua enzi zile kusoma vitabu vya hadithi ilkua lazima na msomaji anapata hisia kali sana [emoji848][emoji848][emoji848]na watunzi mashuhuri kipindi kile mmoja wao aliku ni huyu hamie rajab
Mi moja ya kitabu chake nlokisoma na kukipenda ni hicho mtafute akibisha mlipue
 
MUZIKI HALISI USO KWA USO NA HAMZA KALALA

Hamza Kalala :“Muziki wetu ulikuwa na kila sababu za kuishi, kwani ulitengenezwa kwa ustadi wa hali ya juu. Kulikuwa kuna hatua nyingi za kupitia hadi kufanikiwa kurekodi muziki na kupigwa redioni,”

“ Baada ya mtunzi kutunga muziki, ulienda kufanyiwa mazoezi katika maeneo maalumu. Mara nyingi maeneo hayo yalikuwa ni yale yenye watu, kama vile baa au hata maeneo ambayo kuna muingiliano wa watu”.

Lengo hasa ilikuwa ni kuangalia muitikio wao. Ikiwa watu wataonekana kuvutiwa zaidi na tungo za wimbo husika basi hiyo huonekana kuwa ni dalili nzuri.

“Lakini ikitoka hatua hiyo, hatua inayofuata huwa ni kwenda kuujaribu wimbo huo kwenye steji, ndani ya kumbi zetu tulizokuwa tukitumia kufanya maonyesho yetu. Pale tulikuwa tukisoma muitikio wa mashabiki wetu” anaongeza “ Wimbo mkali hukubalika kutoka kwenye hatua za awali kabisa”.

Baada ya kuupiga kwenye kumbi za muziki kwa majaribio, hatua inayofuata huwa ni kuuwasilisha wimbo huo kwa wataalamu kwa ajili ya kupitiwa.

Wataalamu kama Suleiman Hegga walihusika na jambo hili.

Hapa mashairi ya wimbo yalipitiwa neno kwa neno, na kisha maudhui yalihakikiwa, kabla ya wanamuziki kusikilizwa ikiwa wametamka kwa usahihi maneno yaliyomo ndani ya tungo husika. Matatizo ya lafudhi yalisahihishwa katika hatua hii.

“Ikitokea mwimbaji akatamka Lamazani, badala ya Ramadhani, wimbo utarudiwa, hadi pale neno hilo litakapotamkwa kwa usahihi” anaongeza “ Si hivyo tu hata ikitokea kuwa wimbo unamzungumzia mtu mmoja, kwa mfano mwanaume anamlalamikia mke wake hadi mwisho, watalaamu hawa hushauri kuwako kwa majibu ya malalamiko yanayotolewa hivyo kuingizwa kwa sauti ya mwanamke ndani yake”.

Na hii ndiyo sababu nyimbo nyingi za zamani zilikuwa na sehemu mbili sehemu ya kwanza inakuwa na malalamiko huku ya pili inakuwa na majibu au wakati mwingine muziki huo ulikuwa ukija na kisa, kilichosimuliwa kwa umahiri kama kisa hicho kinahusisha watu wawili basi wote walikuwa wakihusishwa kila mhusika kwa nafasi yake.

Kwa mfano kwenye wimbo wa Nachelewa stendi ya basi ulioimbwa na bendi ya Toma Toma kukiwa na sauti za wanamuziki mahiri kama Marehemu Adam Bakari (Sauti ya Zege). Mume anauliza “Kila siku mke wangu unarudi saa za usiku, ufikapo nyumbani macho yau yau. Nimevumilia sasa nimechoka. Leo nataka unieleze ukweli wapi unapochelewa...?” Mke anajibu “ Nachelewa stendi ya basi bwana eee, tabu ya mabasi waijua mume wangu, nihurumie bwana...”

Unaposikiliza muziki kama huu, unaweza ukagundua kazi kubwa iliyofanyika hadi kufikia hatua ya kurekodiwa kwake.

Kwa mantiki hiyo muziki wa wakati ule ulikuwa na kila sababu ya kuwa na uhai, kwani ulifanyiwa kazi kwa umahiri na weledi mkubwa anafafanua.

Kinachofurahisha zaidi ni kwamba, kulikuwa na watu wengi waliohusishwa kwenye utengenezaji wa muziki.

Kwa mfano, prodyuza alikuwa mwingine, mtaalamu wa sauti mwingine na pia vyombo vyote vya muziki kama vile tarumbeta, gitaa na ala nyingine vilipigwa na mtu mmoja mmoja tofauti na sasa.

Mambo kama haya yalichangia kwa kiasi kikubwa kuufanya muziki wa wakati ule kuishi muda mrefu.
 
Muite eddy sheggy mwamba kweli kweli jamaa alikuw anazungumza kingereza kama vile kazaliwa UK. ngoma zake zilikuw hatari sana kama ile [SHAKAZA] mngosh auko nyika amwekuja vyakwe weangu mngosh auko nyika haweea wana weangu....ntende zeze weangu shakaza..
 
Sarafu za Kirumi za Kale za Hisia Sarafu hizi zilitumika kama ishara za kuingia kwenye madanguro ya Kirumi[emoji845] Kulingana na Suetonius, kubeba sarafu yenye sanamu ya mfalme kwenye choo au danguro kunaweza kuhesabiwa kuwa uhaini. Kwa hivyo, hizi ndizo sarafu pekee zilizotumika kwenye madanguro....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…