JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

Hii ndoa ilifungwa tarehe 17-4-1964 kati ya DKT SALIM AHMED SALIM na marehemu BI AMNE ALLY RIFAI SALIM
wakati huo salim alikuwa mhariri wa gazeti la kila siku la zanzibar na katibu wa jumuiya ya wandishi wa habari zanzibar na bi Amne akifanya kazi kama katibu katika shirika la habari la zanzibar

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Marehemu Georges Kiamuangana Mateta na bendi yake Veve, miaka ile ya 70 mwanzoni. Kuna kibao kimoja marehemu mzee wangu na marafiki zake walikuwa wanapenda sana kusikiliza, "NAKOMITUNAKA", ikimaanisha kwa Kiswahili "NINAJIULIZA". Kibao hicho kilipotoka miaka ile ya 70 kiliibua mitafaruku kwenye jamii nchini mule (Congo-Zaïre) mpaka Kanisa Katoliki nayo ilikuja juu kwa kutopenda maudhui ya wimbo huo uliosadikika kukufuru, Verkys na bendi ya Veve kupitia kibao hicho "NAKOMITUNAKA" walijiuliza, ngozi nyeusi ilitoka wapi? Kwa nini watakatifu, manabii ni wazungu? Na shetani inasadikika kuwa ni mtu mweusi kama anavyochorwa, kwa nini? Ninajiuliza Mungu wa watu weusi ni yupi? Mbona watakatifu weusi hawakubaliki?, N.K.

Inasadikika kuwa marehemu Georges Kiamuangana Mateta aliwekwa ndani kwa sababu ya kutunga na kutoa huo wimbo kwa kuwa ingeweza kuchagia machafuko.

Ninausikiliza huu wimbo sasa hivi, ninatafakari na kujiuliza maswali kama huyo marehemu...

[emoji848][emoji848][emoji848]

Ustaarabu haukuletwa na Waarabu au wazungu barani Afrika. Tulishastaarabika huko nyuma.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo anaonekana winga teleza EDIBILY JONAS LUNYAMILA AKISHANGILIA BAO huku kipa MOHAMEDI MWAMEJA akishangaa
Mechi ilifanyika uwanja wa taifa au uhuru tarehe 27-3-1993
Yanga ilishinda 2-1
Magoli ya yanga yalifungwa na MAREHEMU SAIDI MWAMBA KIZOTA
NA GOLI LA SIMBA LIMEFUNGWA NA EDWARD CHUMILA


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Young Africans waliosimama kutoka kushoto Ramesh patwa,tarzan,sahau kambi,issa athumani,keneth mkapa,yussuf ismael,lawrence mwalusako,Godwin aswile,denis mdoe,said mwamba, Joel bendera wa mwisho sikumbuki.waliopiga magoti kutoka kushoto fred minziro,Justin mtekere,abubakar salum ,athuman juma chama,abdallah burhan,selestine sikinde mbuga,athumani china na Joseph fungo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…