JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

Huyu anaitwa LETTA MBULU, yeye ndiye alieingiza yale maneno ya kiswahili "NAKUPENDA PIA NAKUTAKA PIA, MPENZI WEE" katika wimbo wa MICHAEL JACKSON uitwao LIBERIAN GIRL wa mwaka 1987 , kutoka kwenye album yake iliyoitwa BAD . LETTA MBULU na mume wake aitwae CAIPHUS SEMENYA ambao pia wote ni wanamuziki, walikuwa ni raia wa Afrika ya kusini waliokuwa wakiishi kama wakimbizi nchini Marekani wakati huo.
LETTA MBULU na CAIPHUS SEMENYA bado wapo na wanaishi jijini JOHANNESBURG nchi Afrika Kusini .
Wahenga wengine hawakuwahi kujua.
 
Fundi konde
Majengo siendi tena,
Majengo siendi tena mimi,
Majengo siendi tena,
Kuna ndege za mitambo.

Majengo siendi tena,
Majengo siendi tena mama,
Majengo siendi tena,
Kuna ndege za mitambo.

Moyo wangu wanituma mema,
Niwe mwanachama wa daima,
Sitaweza kuliacha rhumba,
Bila moyo kunituma.

--------
'Majengo Siendi Tena' - Fundi Konde and His Group, EA 284, 1959

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…