Ushauri:
1. Wengi tunakimbilia wingi wa mabandiko badala ya uthamani wake. Mwenye machache ya nguvu ni bora kuliko mwenye mengi ambayo yamechanganywa na ya uzushi au tetesi au hoja ambazo hazina maslahi ya Kitaifa. Yaani kuwa na mabandiko kibao yasiyoleta tija katika maendeleo yetu ni matumizi mabaya ya fursa na rasilimali chache tulizo nazo hapa duniani. Kifupi hapa ninazungumzia ufanisi (Input/Output)
2. Je pia tunaangalia namna ya uwasilishwaji wa hoja. Mifano: Aliye jizoeza kuandika kwa lugha ya ufasaha pasipo kuchanganya changa lugha ni sifa njema kuliko kinyume chake.
3. JF si mahala pa kutoa tu kasoro au kuegemea tu upande fulani bila sababu. Mfano, ningependa kumpongeza yule ambaye anaandika hata mazuri ya Serikali au Kiongozi fulani aliyefanya vizuri maana katika hilo wengine wanajifunza kufanya vyema ili nao watuzwe. Hapa nazungumzia Mwandishi ambaye hana mningínio wa upande fulani tu (Lack of objectivity).
4. Ingawa hili halisemwi, nitalisema. Kuna kamtindo ka baadhi ya wadau kupewa nafasi za upendeleo wa kipekee bila sababu za wazi katika jinsi tunavyopokea lile wanaloandika (kumbuka hadithi ya Mfalme bila vazi lakini watu wanashangila kuwa ana vazi zuri kuliko yote). Mfano. kama kila anayeleta habari hapa anaulizwa mara moja atueleze chanzo chake, basi iwe kwa wote. Haipendezi wengine waanzishe tu mada na kusema chanzo changu na ikakubalika eti kwa sababu ana nyota nyingi au kuna siku moja aliwahi kuibuka mambo mazito kama Wikileaks. Tukifanya hivi basi tutakuwa tunasubuliwa na matatizo yaiyayo Halo effects.