Jicho la Tatu: Bashite na Diamond rudini studio Upya,Tumewasitukia

Jicho la Tatu: Bashite na Diamond rudini studio Upya,Tumewasitukia

Wimbo ni mistari ya mashairi siyo Melody wala umarufu wa mtu
Wimbo huu umekuja ki mkakati umekuja kulifanya jina la MAKONDA lijadiliwe
Liimbwe na media zilizomkataa, Dai kajilipua kumsaidia aliyekataliwa asikike
Ni akili kubwa imecheza ili tusiye mtaka arejee vinywani mwetu kupitia ushawishi wake,wapenzi wake kimuziki[emoji15][emoji15][emoji15]

Tunachezeshwa kwa sauti nyororo yenye kujaa huruma huku yeye akiwa anacheza dili ya kumfufua mfu kisiasa na kimadili

Kagusa hata Bunge ili kushawishi pande zote ili lengo lake litimie hiyo ni akili kubwa mno[emoji12][emoji12]

Walijipanga vizuri sana kama hujifikirishi sana unanasa tu
Mwanzo nilinasa nikachambua shairi nikagundua baada kujiuliza nini Gwajima, Mange kuhusishwa

Nikagundua Askofu Gwajima na Dada Mange ndo wahanga wa wimbo huu wala siyo Roma
Wimbo upo mahususi kimlinda mtu na kushambulia wanaohoji uharali wa vyeti
Hitimisho ni dharau kwetu kuwa tunakaa vijiweni kujadili VYETI VYA BASHITE badala ya KUSAKA SENTI[emoji15][emoji15][emoji15]

Diamond hayupo na Roma Mkatoriki yupo kutetea Mjadala wa VYETI
TUSANUKE TUSIINGIZWE CHAKA TUDAI VYETI BASHITE TOA VYETI

Allan Bhujo FBI
Kumbe nyie ndio mnawatungia mistari wasanii wanaotukana!
 
Kumbe nyie ndio mnawatungia mistari wasanii wanaotukana!
Taja msanii aliyetukana na katoa matusi yapi?
Nyinyi ndiyo mapyukaji bila kujua nini unapayukia. Ukiulizwa utaje tusi utakosa na kubaki kujilamba ulimi tu as if unatongo*****wa
 
Mlisema hivihivi kua Dai kushiriki kwenye kampeni za chama dola,lakini ndo hivyo,huyu jamaa anang'aa tu.Wimbo ni mzuri sana,nilipo hapa unapigwa kila kona.
Wapi kwenu kolomije au chato?
 
Taja msanii aliyetukana na katoa matusi yapi?
Nyinyi ndiyo mapyukaji bila kujua nini unapayukia. Ukiulizwa utaje tusi utakosa na kubaki kujilamba ulimi tu as if unatongo*****wa
Huna marinda wewe.
 
Kila mtu na uhuru wake wa kufanya kitu. Wewe umehamasisha lipi kwa yanayoendelea Tanzania kwa sasa? Anza kampeni ukiwa umeshika bango kuelekea ikulu sio blablaa za jf tu
 
Sasa hapo ameoimba nini kama si unafiki tu,dia kaisha kwa sasa,abuni issue nyingine tu
 
Kwa wanaojua mziki na maana yake haswa ya kila neno kinaloimbwa dimond katoa bonge moja ya somo,,na uzur kaongea linalomkera kwa ustad wa kisanii ambayo hauwez kumtia hatiani.. Anawachamba bila wao kujijua,anatuchamba kufuatilia yasiyotuhusu bila sisi kuelewa,,kapiga kila mahal bila lugha ya kukera.. Huu ndio usanii..

Suala la Makonda nadhan tatizo sio kumzungumzia au kumfufua km ameterereka kwa sasa,nadhan tatizo we mwenyewe unashindwa kuuvumilia moyo wako kumtaja,unavumiliaaaa bado kama kikohoz linakuja tu,,bas hakuna kibaya kam moyo ushindane na akili,,akili haitak kukumbuka huku moyo unakuuma mwsho unakuja kuanzia uzi kuhusu wewe,,,hapo kitaalam umefeli sekta ya maamuz..
 
Ninachosikitika siasa zimetugawa, yaani imekuwa kama uadui, na hii sumu wanaisambaza watu wa upinzani ni sumu mbaya sana, itafika kipindi utashindwa kumsaidia mtu tu kisa itikadi zenu tofauti, sasa kosa la diamond platnumz lipo wapi, hii inchi kila mtu yupo free kuchagua anachokitaka ili mradi asivunje sheria, diamond kawasilisha maoni yake kupitia mziki. Kuwa na itikadi tofauti isiwe tatizo, ila Ninachosikitika sana wanasiasa na mitandao ya kijamii inatugawa vibaya sana, mpaka inafikia Kipindi tunaomba mabaya yatokee kwa nchi yetu, ili kuikomoa serikali, yaani mpaka kwenye kusifia tunakosoa na kwenye kukosoa tunasifia.Watu wanaomponda diamond platnumz ndio hao wanalalamika kila siku inchi haina demokrasia, lkn hawajui diamond platnumz ametumia haki yake ya msingi ya demokrasia kawasilisha mawazo yake kupitia mziki wake. Tanzania kwanza, tusilichukulie hili swala la ROMA kisiasa eti ni la upande fulani. Nammlaani sana kimambi, kwani hii sumu anayoisambaza, haina tofauti na kile kituo cha radio Rwanda kilichorusha habari za kibaguzi, mwisho wake kukawa na mauwaji ya Kimbari. Watanzania tuwe makini sana tusiruhusu mitandao ya jamii na wanasiasa watugawe.
 
daimond naye si bashite....tuuu sanaa bila elimu ni kupoteza muda tuu....dai anapoteza muda....na muda utatoa jibu....walikuwepo kina T.I.D, mr, NICE , FEROUz na wengine wengi leo hii wapo kama hawapo....hivyo dai nae ajiangalie sana...Tanzania si nchi ya kujipendekeza kwa viongozi hata kidogo watamtumia kama toilet paper wakisha jifutia uchafu wao wanamzima kama taa.
 
daimond naye si bashite....tuuu sanaa bila elimu ni kupoteza muda tuu....dai anapoteza muda....na muda utatoa jibu....walikuwepo kina T.I.D, mr, NICE , FEROUz na wengine wengi leo hii wapo kama hawapo....hivyo dai nae ajiangalie sana...Tanzania si nchi ya kujipendekeza kwa viongozi hata kidogo watamtumia kama toilet paper wakisha jifutia uchafu wao wanamzima kama taa.
Sawa..!
 
Ukiona makele MENGI sana ya watu juaa ya kuwa wamefika sehem wamechoka na vituko vinavyoendelea IPO siku mtakipata mbachokitafuta tuu
Aca masihara kaka. Makelele gani? Ya mtandaoni? Usinichekeshe.
 
Back
Top Bottom