Jifunze kilimo cha nyanya

Jamani Bei ya Nyanya ikoje huko Masokoni? kwa maana Huku niliko (Tanga) Bei ni Maumivu, Creti linaenda mpaka elfu kumi (10) Na nikicheki shambani zianiva kwa fujo. Kichwa kimepata Moto.
Mkuu naomba kuulizia kitu kama hutojali, mimi pia nipo Tanga huku Korogwe, nimekuwa nikijishughulisha na kilimo cha maharage haya ya njano, ila kuanzia mwezi wa 10 ninataka kujaribu kilimo cha nyanya. Je kwa uzoefu wako mbegu hii ya Assila f1 kwa upande huu inafanya vizuri? Ukizingatia muda tunaolekea ni msimu wa joto ila nategemea kulima kwa kumwagilia, na je kama Assila haifanyi vizuri huku Tanga ni mbegu gani nyingine ya kisasa (hybrid ) inayokubali huku hasa Korogwe kama unaufahamu nako? Nimefwatilia huku wengi wanatumia mbegu hizi za kawaida kama vile Tanya na Tengeru ambazo wadau wanasema mavuno yake ni kidogo. Msaada wenu wakuu kwa mtu anayefahamu mazingira haya ya Korogwe joto lake linarange kwenye 27 centigrade mpaka 30 centigrade kama Dar es Salaam vile ila udongo wake ni mweusi na una kichanga kwa mbali sana. Je mbegu ya Assila f1 inaweza kuhimili hiyo hali ya hewa?
 
Mm ni mkulima wa nyanya na mpunga kijiji cha mbigili,dumila mkoani morogoro
wakulima wenzangu wa nyanya tubadilishe uzoefu kilimo cha nyanya kuhusu mbegu,mbolea,magonjwa,madawa na masoko
karibuni sn


Nyanya nyanyua, nyanya nyanyasa
 
Naomba kuuliza, ni wakati gani nyanya huwa na bei juu sana, na ni wakati gani bei huwa chini, na ni kwasababu zipi, majibu wataalamu
 
Tumia mbegu inaitwa ZARA F1 ya balton Tanzania, utaleta matokeo baadae
 
Naomba kuuliza, ni wakati gani nyanya huwa na bei juu sana, na ni wakati gani bei huwa chini, na ni kwasababu zipi, majibu wataalamu
Huwa tofauti kulingana na mikoa, ila kwa bei kua chini au juu husababishwa na uzalishaji kipindi cha mvua kikipita tu wengi wanazalisha nyanya sababu kila sehemu kuna kua na unyevu au maji ya kutosha
 
Huwa tofauti kulingana na mikoa, ila kwa bei kua chini au juu husababishwa na uzalishaji kipindi cha mvua kikipita tu wengi wanazalisha nyanya sababu kila sehemu kuna kua na unyevu au maji ya kutosha
Je kipindi cha mvua, nyanya haioti, na je nikiamua kupanda nyanya kipindi hicho cha mvua ni changamoto gani nitapitia.
 
Okays sawa sawa, ngoja nianze na practical bustani ya nyumbani, na mvua hizi huwa nyingi kipindi gani!? Hasa kwa dar es Salaam.
Madawa ya fungus utatumia sana, kuna kua na magonjwa mno ya ukungu sababu ya hali ya hewa ya unyevu
 
wakuu,mm nipo zenji na huku nilipo ardhi yake ya mawe na udongo mweusi je nitumie mbegu gan nzur ili nipate mazao meng lkn natumia dripu irrigation
Tumia Zara f1, inapatikana pale kwa Masudi Biziredi (Mwembeladu), nami niko Zenji kwa sasa unalima sehemu gani Zenji hii???
 
Ninataka kulima nyanya kipindi cha masika ni mbegu ipi nzuri kulima kati ya eden f1 na gamhar f1 ya rijk zwaan nipo Igunga udongo ni black cotton soil hali ya hewa ni joto mvua ni kidogo
Swali lako sijalielewa umesema masika (mvua) halafu umesema mvua kidogo?????
 
Tumia mbegu inaitwa ZARA F1 ya balton Tanzania, utaleta matokeo baadae
Mkuu kwanza asante sana kwa jibu lako, pili ninaomba unijulishe ofisi za BALTON TANZANIA kwa Dar es Salaam zinapatikana eneo gani kama unafahamu au hata namba zao za simu za ofisi. Tatu hii ZARA f1 50gram inauzwa bei gani kama unafahamu, na vipi eneo la ekari 1.5 gram ngapi zaweza tumika endapo nitatumia vipimo vifuatavyo 30cm shimo hadi shimo, na 60cm mstari hadi mstari. Je hii mbegu vipi kuhusu uzaaji wake shambani unaweza chuma mara ngapi? Horticulturalist msaada wako tafadhali na kama hutojali naomba unipm namba yako ya simu. Thanks in advance for your help.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…