Jifunze Mambo Mbalimbali Kuhusu Kilimo cha Tunda la Makakara (Passion)

Jifunze Mambo Mbalimbali Kuhusu Kilimo cha Tunda la Makakara (Passion)

Kama ulifanikiwa mkuuu naomba mrejesho.

Mana na mm nasafisha shamba nataka nipande hili zao la matunda.
 
Heshima kwanza

Wakuu, nina shamba eneo la Makaa Yamu, Kirua Vunjo, wilaya ya Moshi vijijini lenye ukubwa wa ekari kumi na sita 16 (limepimwa na hati miliki)

Shamba lipo kilometer nne kutoka barabara kuu iendayo Dar es salaam na Mombasa.Shamba hili lipo eneo la ukanda wa tambarare Kusini mwa mlima Kilimanjaro.Ukanda wa eneo hili lilipo shamba langu ni mkubwa sana na wamiliki wengi wa mashamba haya hulima mahindi wakati wa msimu wa mvua (masika).

Eneo hili lina rutuba nzuri sana, udongo wake ni tifutifu. Inaonyesha kuwa water table yake haipo mbali sana.

Wakuu wazo langu ni kugeuza uwanda huu kuwa horticultural hub kwa kilimo cha aina ya zao la matunda ya passion lengo likiwa ni kuweza kusindika tunda hili la passion na kupata passion powder kwa ajili ya flavoring kwenye bidhaa mbali mbali za chakula kama ice creams, cakes, fruit yougurt, juices and soft drinks, jams n.k

Pia tunda hili la passion linaweza kutengeneza wine mzuri sana.

Naomba pia anayejua bidhaa tofauti zinazotokana na zao hili na masoko yanayohusu passion fruit.

Wakuu ninaomba ushauri juu ya utaalam wa ulimaji wa zao la passion, hivyo basi nikiweze kuanzisha kilimo hicho nitatoa mfano wa shamba bora na kuwabadilisha wakulima wote wa eneo / uwanda huu waweze kulima hili zao na baadae kulisambaza maeneo ya nchi nzima ambapo zao hili products zake zina soko lenye bei nzuri na kubadilisha maisha ya wananchi hawa.

Haya ni mawazo tu ya mwanzo ambayo sijayafanyia utafiti wa kina nikisubiri changamoto na michango ya wenzangu wapenda kilimo na wenye utaalam na uzoefu zaidi .

Pia yeyote yule humu JF anakaribishwa kutoa ushauri na mchango wake.

---------------------------------
Asante sana
 
Asante sana

Nimejaribu hii kitu Kwa kuotesha miche minne mwezi April 2016 jana tar 04 Jan nimepata kiasi cha matunda 20
IMG_20161210_074454.jpg
 
mbona kidogo au?

Kidogo miche au matunda? Kama ni matunda yapo mengi, yaliyovunwa ni yaliyokomaa Kwa awali.

Lakini kama unaulizia uchache wa yanayoonekana pichani, ni kuwa hiyo umechukua katika mti mmoja zaidi ya mwezi uliopita. Natumaini nimejitahidi kufafanua
 
Miche minne matunda 20?
Mi najua yanazaa sana ndo maana nashangaa

Sielewi unavyotumia neno kuzama Sana unamaanisha idadi gani Kwa kilo ktk mti.

Kwa kuwa ndio yameanza ninaweza jibu vizuri kadri siku zinavyokwenda. Lakini kuna baadhi ya machapisho yanaeleza kuwa mti mmoja hutoa kilo 30 Kwa msimu.
 
Hili zao siku hizi lina changamoto sana, nakumbuka zamani nyumbani tulikuwa tukiotesha walau mche mmoja unaweza kupata matunda hata 200, siku hizi hakuna cha mtunda wala nini, nadhani mnyauko wa ndizi pia unanyausha matunda pasheni.
 
Kuna aina nyingi za matunda haya lakini yale ya kijani/manjano hustawi zaidi ukanda wa pwani na yale yenye wekundu fulani hustawi zaidi maeneo ya misitu, hupendelea udongo wa kichanga wenye mbolea na usiotuamisha maji, pia udongo usiwe na chumvi nyingi na pia kusiwe na mwamba chini kasi cha mita moja tu.

IMG_4794.JPG
IMG_4798.JPG



Upandaji.

Mbegu zipandwe kwanza kwenye mifuko ya plastiki yenye udongo wenye rutuba ya kutosha , kiasi cha Mbegu 3 kwa kila mfuko na mara zinapoota mimea ikingwe na jua kali na ikifikia urefu wa sentimeta 30, huweza kuhamishiwa shambani


Kwenye shamba lako hakikisha kuna nguzo zenye waya mmoja kwa ajili ya mimea kutambaa juu yake, sehemu ya juu baada ya nguzo kuzikwa chini ibakie kama mita mbili na kati ya msatari na mstari iwe ni mita 2 (ukanda wa pwani ) na mita 3 ukanda wa juu kiasi, na umbali kati ya nguzo na nguzo kwenye mstari ni mita 6, na mimea ipandwe umbali wa mita 3 kati ya nguzo na nguzo kufuata mstari.

IMG_4790.JPG

IMG_4795.JPG


UPANDAJI WA KITAALAM


Mbolea

Mbolea za viwandani ziwekwe kutokana na hali ya udongo, muone afisa ugani kilimo ili afanye vipimo kujua mahitaji na upungufu wa udongo.

Magonjwa na wadudu.

Wadudu kama chawa wa mimea na mchwa wekundu ndio adui wa makakara, pia fangasi husshambulia sana maua ya makakara.

Dawa za jamii ya kopa zitumike mara dalili za magonjwa au wadudu kuonekana, kiasi cha kilo 2.8 – 3 hutosha kwa hekta moja au gramu 225 kwa ajili ya dumu moja la lita 20.

Magugu.
%

Makakara yanatakiwa yawe kwenye shamba safi lisilo na majani na magugu, jembe la Mkono au madawa kama ROUND-UP na GRAMOXONE zinaweza kutumika mimea ikisharefuka na kuwa juu kwenye waya.

IMG_4791.JPG


KUPUNGUZA MATAWI

Kupunguza matawi.


Silazima kupunguza matawi kwa sababu mmea mkubwa zaidi ndio hutoa matunda mengi zaidi, labda kama kuna matatizo katika uchumaji ndio unaweza kupunguza baadhi ya matawi kiasi.

Uvunaji.
Uvunaji huanza baada ya miezi 8 – 9 baada yam mea kupandwa na matunda hukusanywa baada ya kudondoka yenyewe chini au waweza chuma pindi rangi inapokuwa imekolea kias cha kuridhisha tunda limeiva,matunda huiva kila baada ya wiki moja, matunda yahifadhiwe sehemu kavu na isiyo na joto , kiasi cha tani 5 – 10 huweza kupatikana katika heka moja kwa msimu.

IMG_4803.JPG
 
Ni kweli mikakara inaharibu rutuba ya ardhi?
Nilikuwa na mpango wa kuilima ila nikatishika na hii tetesi
 
Wakuu nataka nianze kilimo cha matunda ya passion,naomba mwenye kujua utaalamu wake,masoko na etc. anisaidie
 
Back
Top Bottom