Jifunze namna ya kutengenza Mkaa kwa kutumia takataka za shambani

Jifunze namna ya kutengenza Mkaa kwa kutumia takataka za shambani

MAMESHO

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
1,432
Reaction score
1,738
Hello JF members!

Natoa shukrani za dhati kwa hili jukwaa. Ni kwa namna nyingi nimenufaika nalo.

kwa wale wanaotaka kujifunza kutengeneza mkaa nimewaanzishia huu uzi. Najua wapo walioamua kuuza huu ujuzi kwa namna mbali mbali. hapa naanika bure kile nikijuacho.

Furahia na tengeneza hela!

KUTENGENEZA MKAA KWA NAMNA RAHISI.
Mahitaji:

1.Takataka za mashambani: magunzi, mbaki ya kuangua nazi, majani, makuti ya mmnazi na kadhalika. Au vumbi la mkaa uliosalia kwenye uuzaji au tanuru la kuchomea mkaa
2. Chombo cha kuchoma takataka za mashambani. Drum bovu, ndoo la chuma au kinginecho
3. Bomba la plastiki la nchi tatu upana urefu nchi sita
4. Mche wa kugandamiza
5. Unga mchafu, pumba zilizosagwa au mckanganyiko wa karatasi laini na na maji(paper pulp) ambao utatumika kama gundi.

HATUA YA KWANZA.
Kubadili taka kuwa hali ya mkaa (carbonisation process) kusanya takataka za mashambani kisha weka kwenye drum (liwe na matundu madogo chini halafu zichome.

Zikiwaka baada ya moto mkali kutulia weka mfuniko kisha pembezoni ziba na tope(udongo na maji) ili hewa isiingie. Acha kwa muda mpaka taka zigeuke kuwa mkaa. Mimina na acha mkaa upoe.

2.PNG

HATUA YA PILI.
Twanga mkaa ili kupata unga kama unavyoonekana hapo chini. Kama ni mabaki ya mkaa twanga na chekecha kupata unga

3.PNG
4.PNG

HATUA YA TATU
Kuandaa gundi ya mkaa. Chukua unga ( unawaza kuwa wa muhogo, mahindi, ndizi (pia maganda ya nafaka hizi yanafaa, pumba n.k ) au nafaka nyingineyo.

Vipimo ni nusu kilo ya unga itatumika kuchanganye na kilo kumi ya vumbi ya mkaa. Chukua unga upike uji mzito kabla ya kuchanganya na mkaa kama inavyoonekana hapo juu kwenye picha.

Uji wakati unachemka ukianza kutokota utakuwa tayari. Changanya ukiwa wa moto na finyanga uwe kama ugali.

Angalizo: usifwate sana vipimo. Aina ya taka zina vumbi la aina tofauti. Unaweza ukalowanisha vumbi lako la mkaa kwanza kabla ya kuweka gundi (binder) pia ukiona wakati unachanganya ni mlaini sana ongeza vumbi. Ukiona ni mgumu sana ongeza uji (gundi) finyanga kama ugali.

HATUA YA NNE
Uzalishaji: unaweza ukafinyanga matonge kwa mkono na kuweka juani yakauke. Pia unaweza kutumia njia hii rahisi
Utahitaji

  1. bomba la plastiki nchi 2 mpaka nchi 3 kwa kipenyo na nchi 4 mpaka 6 kwa urefu
  2. Mche wa kusukumia (kugandamiza) hakikisha unateremka kwa urahisi kwenye bomba (usibane wala kukwangua)
  3. Kibao cha kuweka chini
5.PNG
Weka mkaa ndani ya bomba kisha gandamiza (unaweza kugonga na mbao kidogo kwa juu kama bomba lako ni gumu vya kutosha unaweza kutumia la chuma pia kwa kazi hii) geuza upande ulioshikia na gandamiza kutoa mkaa. Mche ukae kwa chini na wewe ukamate bomba mkaa upande juu.

6.PNG

HATUA YA MWISHO
Anika mkaa wako kwenye jua kwa siku nne hadi tano. Tumia ukiwa umekauka sawasawa.

Mwisho kabisa
Mwongozo huu ni kukuwezesha kujua machache. Nitazidi kuboresha hii post. Kwa makosa ya uandishi kazi hii nawaachia editors.
 

Attachments

mkuu nilizi paste hazikutokea ila zipo ndani ya attachment ya PDF nitaziandaa wakati mwingine niziambatanishe

mkuu humu watumia simu hasa mchina tupo wengi,tusaidie kwa hilo
mi huwa sibanduki kwenye hili jukwaa
 
wakuu,lile bandiko la mkaa la mdau. biashara 2000 na hili zina uhusiano wowote?
 
Last edited by a moderator:
wakuu,lile bandiko la mkaa la mdau. mwingine na hili zina uhusiano wowote?

Mimi mtoa uzi najulisha kwamba halina uhusiano wowote. siuzi ujuzi nimeutoa bure.
 
Hicho kibarua c mchezo, nilishuhudia jamaa akitengeneza huo mkaa karibia wiki nzima, mkaa uliopatikana haukuweza kuivisha maharage nusu kilo!!!
 
Hicho kibarua c mchezo, nilishuhudia jamaa akitengeneza huo mkaa karibia wiki nzima, mkaa uliopatikana haukuweza kuivisha maharage nusu kilo!!!

mimi pia niliwahi kukutana na hiyo kazi. inategemea unatumia malighafi za namna gani. vumbi aliliokuwanalo alipaswa achanganye na vumbi alilokusanya kwa wauza mkaa 50:50 unawaka kama kawaida. kosa lingine hutokea kama utachoma na kupitiliza kiwango zile taka za mashambani.
 
Hello JF members!

Natoa shukrani za dhati kwa hili jukwaa. Ni kwa namna nyingi nimenufaika nalo.

kwa wale wanaotaka kujifunza kutengeneza mkaa nimewaanzishia huu uzi. Najua wapo walioamua kuuza huu ujuzi kwa namna mbali mbali. hapa naanika bure kile nikijuacho.

Furahia na tengeneza hela!

KUTENGENEZA MKAA KWA NAMNA RAHISI.
Mahitaji:
1.Takataka za mashambani: magunzi, mbaki ya kuangua nazi, majani, makuti ya mmnazi na kadhalika. Au vumbi la mkaa uliosalia kwenye uuzaji au tanuru la kuchomea mkaa
2. Chombo cha kuchoma takataka za mashambani. Drum bovu, ndoo la chuma au kinginecho
3. Bomba la plastiki la nchi tatu upana urefu nchi sita
4. Mche wa kugandamiza
5. Unga mchafu, pumba zilizosagwa au mckanganyiko wa karatasi laini na na maji(paper pulp) ambao utatumika kama gundi.

HATUA YA KWANZA.
hatua ya kwanza.jpg
Kubadili taka kuwa hali ya mkaa (carbonisation process)
kusanya takataka za mashambani kisha weka kwenye drum (liwe na matundu madogo chini halafu zichome. Zikiwaka baada ya moto mkali kutulia weka mfuniko kisha pembezoni ziba na tope(udongo na maji) ili hewa isiingie. Acha kwa muda mpaka taka zigeuke kuwa mkaa. Mimina na acha mkaa upoe.

HATUA YA PILI.
Twanga mkaa ili kupata unga kama unavyoonekana hapo chini. Kama ni mabaki ya mkaa twanga na chekecha kupata unga
hatua ya pili na ya tatu.jpg
HATUA YA TATU
Kuandaa gundi ya mkaa. Chukua unga ( unawaza kuwa wa muhogo, mahindi, ndizi (pia maganda ya nafaka hizi yanafaa, pumba n.k ) au nafaka nyingineyo. Vipimo ni nusu kilo ya unga itatumika kuchanganye na kilo kumi ya vumbi ya mkaa. Chukua unga upike uji mzito kabla ya kuchanganya na mkaa kama inavyoonekana hapo juu kwenye picha. Uji wakati unachemka ukianza kutokota utakuwa tayari. Changanya ukiwa wa moto na finyanga uwe kama ugali.
Angalizo: usifwate sana vipimo. Aina ya taka zina vumbi la aina tofauti. Unaweza ukalowanisha vumbi lako la mkaa kwanza kabla ya kuweka gundi (binder) pia ukiona wakati unachanganya ni mlaini sana ongeza vumbi. Ukiona ni mgumu sana ongeza uji (gundi) finyanga kama ugali.
HATUA YA NNE
Uzalishaji: unaweza ukafinyanga matonge kwa mkono na kuweka juani yakauke. Pia unaweza kutumia njia hii rahisi
Utahitaji

  1. bomba la plastiki nchi 2 mpaka nchi 3 kwa kipenyo na nchi 4 mpaka 6 kwa urefu
  2. Mche wa kusukumia (kugandamiza) hakikisha unateremka kwa urahisi kwenye bomba (usibane wala kukwangua)
  3. Kibao cha kuweka chini

hatua ya nne.jpg
Weka mkaa ndani ya bomba kisha gandamiza (unaweza kugonga na mbao kidogo kwa juu kama bomba lako ni gumu vya kutosha unaweza kutumia la chuma pia kwa kazi hii) geuza upande ulioshikia na gandamiza kutoa mkaa. Mche ukae kwa chini na wewe ukamate bomba mkaa upande juu.
hatua ya tano.jpg
HATUA YA MWISHO
Anika mkaa wako kwenye jua kwa siku nne hadi tano. Tumia ukiwa umekauka sawasawa.
Mwisho kabisa
Mwongozo huu ni kukuwezesha kujua machache. Nitazidi kuboresha hii post. Kwa makosa ya uandishi kazi hii nawaachia editors.
 
Ubarikiwe mkuu na pia umeniongezea nyama katika ujuzi niliokuwa nao!
changamoto zipo hasa kwenye uanikaji wa mkaa kipindi hiki cha mvua ukizingatia demand na soko hushamiri kwenye masika haya!
Hivi hatuwezi kugundua nyingine ya kudrain mkaa huu? I mean something mechanical like a kiln(tanuri lenye high temp.) ili kuspeedup ukaushaji. Ila wasiwasi wangu pengine ukitumia njia hii mkaa unaweza utoke very lighter in waight.
Tuchangie mawazo jamani ili tupate mbadala wa jua.
 
Ubarikiwe mkuu na pia umeniongezea nyama katika ujuzi niliokuwa nao!
changamoto zipo hasa kwenye uanikaji wa mkaa kipindi hiki cha mvua ukizingatia demand na soko hushamiri kwenye masika haya!
Hivi hatuwezi kugundua nyingine ya kudrain mkaa huu? I mean something mechanical like a kiln(tanuri lenye high temp.) ili kuspeedup ukaushaji. Ila wasiwasi wangu pengine ukitumia njia hii mkaa unaweza utoke very lighter in waight.
Tuchangie mawazo jamani ili tupate mbadala wa jua.
Uko sahihi mkuu,
mimi ni niko kwenye hii industry ya renewable energy, Tuna plant ya kuzalisha huu mkaa lakini ya kwetu ni mass production. Sis tunatumia drier kubwa zinazo tumia mafuta(oil chafu). Hii inatusaidia sana kuzalisha na kukidhi soko ambalo ni kubwa sana.
 
Ubarikiwe mkuu na pia umeniongezea nyama katika ujuzi niliokuwa nao!
changamoto zipo hasa kwenye uanikaji wa mkaa kipindi hiki cha mvua ukizingatia demand na soko hushamiri kwenye masika haya!
Hivi hatuwezi kugundua nyingine ya kudrain mkaa huu? I mean something mechanical like a kiln(tanuri lenye high temp.) ili kuspeedup ukaushaji. Ila wasiwasi wangu pengine ukitumia njia hii mkaa unaweza utoke very lighter in waight.
Tuchangie mawazo jamani ili tupate mbadala wa jua.

Mkuu hii kitu inawezekana. Inahitaji ubunifu na majaribio. kitu kama oven au kaushio litoalo hewa ya joto bila kuwa na mgusano na moto ambayo itatumia nishati ambayo inapatikana kwa urahisi kama mapumba ya mbao. au nishati nyingine rahisi. ila changamoto ni kuwa itabidi kifaa hicho kiwe na eneo kubwa ili utoke mwingi kwa wakati. haiwezi kupunguza uzito wake.
 
Uko sahihi mkuu,
mimi ni niko kwenye hii industry ya renewable energy, Tuna plant ya kuzalisha huu mkaa lakini ya kwetu ni mass production. Sis tunatumia drier kubwa zinazo tumia mafuta(oil chafu). Hii inatusaidia sana kuzalisha na kukidhi soko ambalo ni kubwa sana.

Mkuu unaweza kuelezea kidogo drier mlizonazo zimetengenezwa wapi na zinafanyaje kazi?
 
Back
Top Bottom