Uchaguzi 2020 Jimbo la Morogoro mjini linamuhitaji Mbunge msomi na mwenye mikakati

Uchaguzi 2020 Jimbo la Morogoro mjini linamuhitaji Mbunge msomi na mwenye mikakati

Mvidunda

Senior Member
Joined
May 30, 2020
Posts
122
Reaction score
170
Hicho ndicho kilio cha wana Morogoro mjini walio wengi. Wanalalamika uwakilishi usiokata kiu ya maendeleo ya wakaazi wa Jimbo hilo. Wasomi na wasio wasomi, hii inajumuisha pia wananchi wa kada zote jimboni hapa wanalalamika kuwa na mwakilishi kwa miaka 15, asiye na maono ya kimikakati na amebaki kujigeuza kama mfadhiri ilhali anavyovifadhiri havina tija kwa jamii pana na kwa kesho ya wananchi wa jimbo hilo.

" Hatuhitaji vitu vinavyonufaisha mtu mmoja mmoja. Hatuhitaji misaada ambayo sio endelevu kwa kesho ya wanaMorogoro. Tunahitaji Mbunge ambaye atakuwa na uwezo wa kujenga hoja, kupanga mikakati ya muda mfupi wa kati na muda mrefu kwa ajili ya kuipeleka Manispaa yetu mbele. Mbunge ambaye atashirikiana vyema na wataalamu na watendaji wa Manispaa kwa ajili ya kusukuma gurudumu la maendeleo. Wamenukuliwa baadhi ya wananchi wakisema.
Ombi kwa CCM

Wananchi wa Morogoro wanakipenda chama CCM, wanakiomba chama hicho kiwaletee mgombea msomi, makini, mjenga hoja na ambaye hatatafsiri kuwa ubunge ni kutoa vimisaada ambavyo havibadilishi maisha ya jamii pana. Wanaomba chama hicho kiwaletee mtu makini na asiye na chembe za ubepari. Ndiyo! Wanaomba chama CCM kiwaletee mgombea asiye na chembe za ubepari ambapo kwake siasa isiwe kivuli cha kujinufaisha na kulinda amali zake bali liwe ni jukwaa la kupanga na kutekeleza mikakati ya maendeleo.

"Rais Dkt John Pombe Magufuli anahitaji watu makini wa kumsaidia. Anahitaji wapanga na watekeleza mikakati. Anahitaji wasomi, wabunifu na wenye uzalendo na uchungu wa maendeleo ya nchi. Ni vema safari hii akiwa Kama mwenyekiti wa CCM akatuletea watu/mtu makini jimbo la Morogoro mjini. Huyu apumzike aendelee na biashara zake amepwaya kwa kiasi kikubwa katika muktadha wa kuleta maendeleo endelevu jimboni hapa" Alisema mmoja wa watu wenye ushawishi kwa siasa za Morogoro ambaye ni msomi wa sayansi ya siasa.
 
Watu wa Morogoro, hasa Moro Mjini wamelaza Sana akili, wanaenda vya bure wanavyogawiwa na Avoid. Lakini Moro Kuna changamoto nyingi Sana Kama za barabara,maji n.k
 
Mnakosea sana kufikiri haya.

Kwanza inaelekea wengine tunajiandikia tu huku hata hatujui kazi ya "mbunge" ni nini

Mbunge ni mpeleka mawazo tu ya watu anaowawakilisha kutoka katika eneo linaloitwa "jimbo la uchaguzi" katika baraza ama mkutano mkuu wa taifa wa wawakilishi wote wa majimbo yote katika nchi yote....

Mkutano ama baraza kuu hili linaitwa "BUNGE"...

Ndani ya mkutano huu wa " BUNGE", zipo pande mbili. Upande huu ni "wananchi" kupitia "wawakilishi wao - wabunge". Upande wa pili huu ipo " serikali kuu - Rais na mawaziri wake"....

Bunge ndiyo wananchi wenyewe. Bunge ni "supreme power" dhidi ya serikali. Bunge (wananchi) ndiyo wameipa serikali mamlaka ya kuamua kwa niaba yao. Bunge linakuwa pale kuidhibiti serikali isiende nje ya mstari...

Serikali kupitia vyombo na taasisi zake ndiyo ina jukumu la kukusanya kodi na kuzipangia matumizi yake. Ili matumizi hayo yawe "legal" ni sharti yawe approved na wanachi kupitia chombo chao - Bunge...

Unapofika wasaa huu wa kupitisha matumizi ya serikali kwa nchi nzima, ndipo kila mbunge anapotoa mahitaji ya watu wake ktk locality (jimbo) lake....

Kwamba jimboni kwangu wananchi wanahitaji 1, 2, 3, 4.....nk. Sasa Tanzania nasikia ina majimbo zaidi ya 250...

"Mbunge" huyu si mwamuzi wa kile watu waliomtuma wanataka kiwe;

Mfano kama waliomtuma wanataka wajengewe barabara ama shule ama kitu hiki ama kile. Kiuhalisia yeye hana uamuzi wa kusema watu wa jimbo la Morogoro mmenituma kupeleka ombi la mjengewe barabara ama shule ama stendi, basi mmepata tayari...

Hana uamuzi huo asilani hata awe msomi wa kiwango cha juu chochote duniani..!!!!

Kupeleka mawazo ya unaowakilisha kama mbunge na kupokelewa ni jambo moja. Lakini maombi/mawazo kufanyiwa kazi ni jambo jingine kabisa. Na hapa ndipo palipo na shida....

Kufanyiwa kazi kwa mawazo ya watu anaowakilisha mbunge kunategemea mambo mengi;

å Allocatiin ya bajeti/rasrimali fedha ya nchi
å Utashi wa kisiasa wa wenye maamuzi na mamlaka
å Vipaumbele vya kibajeti (budgetary priorities) vya nchi
å Nani anahitaji zaidi kuliko mwingine ama jimbo gani linahitaji zaidi kitu hicho hicho...
å Nk nk nk..

Kwa kuzungatia jukumu ama kazi ya mbunge, mtu yeyote anaweza kuwa mbunge ili mradi ana akili timamu, msikilizaji mzuri, anajali, ana uwezo wa kujenga hoja na kueleweka, mbunifu, mhamasishaji (mobilizer & motivator) mzuri wa anaowakilisha nk nk....

"Usomi" wa mbunge wa kiwango chochote "it's just an added advantage" lakini hakiwezi kuwa kigezo cha jimbo fulani kuwa guaranteed kupiga hatua kubwa za kimaendeleo kijamii na kiuchumi eti kwa sababu lina mbunge msomi...!!

Na kwa taarifa na faida ya wasomaji, wengi wa "watu wasomi wana sifa hizi; wana viburi, watafuta vyeo tu kwa kutumia usomi wao, si wanyenyekevu, wana maringo kwa sababu ya elimu yao na tabia zingine zinazofanana na hizi....

Hawa kwa ujumla wengi wao hawafai kuwa wakikilishi wa watu kwenye nafasi kama ya ubunge, udiwani nk.....

Kinacholeta tatizo ktk nchi yetu ni mfumo wetu wa kiutawala kikatiba na kisheria kuwa na matundu ama matobo tobo mengi....

Walioweka kigezo kikuu cha mwakilishi (mbunge ama diwani) kuwa na sifa ya KUJUA KUSOMA na KUANDIKA tu ba kiwango cha elimu ya drs la VII ama form IV tu, walikuwa sahihi sana kwa kuwa walizingatia jukumu/kazi ya mwakilishi huyu ni nini.

As time went on na kutokana mfumo wa utawala wa nchi ukaondoka katika lengo lake kuu yaani kuhudumia wananchi na kuwa kujinufaisha viongozi kwanza kwa gharama ya wananchi (wapiga kura).

Wasomi wengi wakaiona fursa hii. Wengi wakawa wanaacha taaluma zao na kuingia kwenye siasa na kuanza kusaka nafasi za uongozi wa kisiasa kama uDC, uRC, uWaziri, ubunge nk nk

Watapitia wapi? Ni huko kwa wananchi kwa kuwarubuni na usomi wao kwa ahadi kuwa watatumia usomi wao kuwandolea kero ya umasikini wao hawa wananchi huku ukweli ukiwa ni kuwa wanaenda kujikwamua wao na familia zao kutoka kwenye umasikini....!!

Kwa hiyo tusidanganyane hapa....
 
Mnakosea sana kufikiri haya....

Kwanza inaelekea wengine hatujui hata kazi ya "mbunge" ni nini....

Mbunge ni mpeleka mawazo tu ya watu anaowakilisha kutoka katika eneo linaloitwa "jimbo la uchaguzi" katika baraza ama mkutano mkuu wa wawakilishi wa majimbo yote katika nchi yote....

Mkutano ama baraka kuu hili linaitwa "bunge"...

"Mbunge" huyu si mwamuzi wa kile watu waliomtuma wanataka kiwe; mfano kama waliomtuma wanataka wajengewe barabara ama shule ama kitu hiki ama kile.....

Absolutely, yeye hana uamuzi wa kusema watu wa jimbo la Morogoro mmenituma kupeleka ombi la mjengewe barabara ama shule ama stendi, basi mmepata tayari... Hana uamuzi huo..!!

Kupeleka mawazo ya unaowakilisha kama mbunge na kupokelewa (na mara zote huwa hivyo) ni jambo moja. Lakini kufanyiwa kazi ni kitu kingine na hapa ndipo palipo na shida....

Kufanyiwa kazi kwa mawazo ya watu anaowakilisha mbunge kunategemea mambo mengi;
å Bajeti/rasrimali fedha
å Utashi wa kisiasa wa wenye maamuzi na mamlaka
å Vipaumbele (priorities) vya nchi
å Nani anahitaji zaidi kuliko mwingine ama jimbo gani linahitaji zaidi kitu hicho hicho...
å Nk nk nk..

Kwa jukumu ama kazi ya mbunge, mtu yeyote anaweza kuwa mbunge ili mradi ana akili timamu, msikilizaji mzuri, anajali, ana uwezo wa kujenga hoja na kueleweka, mbunifu, mhamasishaji (mobilizer & motivator) mzuri wa anaowakilisha nk nk....

"Usomi" wa mbunge wa kiwango chochote "it's just an added advantage" lakini hakiwezi kuwa kigezo cha jimbo fulani kuwa guaranteed kupiga maendeleo makubwa kijamii na kiuchumi....

Na kwa taarifa na faida ya wasomaji, wengi wa "watu wasomi sana" ni kwenye viburi, watafuta vyeo tu kwa kutumia usomi wao, si wanyenyekevu, wana maringo kwa sababu ya elimu yao na tabia zingine zinazofanana na hizi. Hawa wengi hawafai kuwa wakikilishi wa watu kwenye nafasi kama ya ubunge nk.....

Kinacholeta tatizo ktk nchi yetu ni mifumo yetu ya kikatiba na kisheria ya kiutawala kuwa na matundu ama matobo tobo mengi....

Walioweka kigezo kikuu cha mwakilishi (mbunge ama diwani) kuwa na sifa ya KUJUA KUSOMA na KUANDIKA walikuwa sahihi sana kwa kuwa walizingatia jukumu/kazi ya mwakilishi huyu ni nini....

As time went on na kutokana mfumo wa utawala wa nchi ukaondoka katika lengo lake kuu yaani kuhudumia wananchi na kuwa kujinufaisha viongozi kwanza kwa gharama ya wananchi (wapiga kura)....

Wasomi wengi wakaiona fursa hii. Wengi wakawa wanaacha taaluma zao na kuingia kwenye siasa na kuanza kusaka nafasi za uongozi wa kisiasa kama uDC, uRC, uWaziri, ubunge nk nk

Watapitia wapi? Ni huko kwa wananchi kwa kuwarubuni na usomi wao kwa ahadi kuwa watatumia usomi wao kuwandolea kero ya umasikini wao hawa wananchi huku ukweli ukiwa ni kuwa wanaenda kujikwamua wao na familia zao kutoka kwenye umasikini....!!

Kwa hiyo tusidanganyane hapa....

Khaah!,
Nimekubali Katibu wa Mh.Aziz Abood,
Si kwa kutiririka huku.
 
Mnakosea sana kufikiri haya....

Kwanza inaelekea wengine hatujui hata kazi ya "mbunge" ni nini....

Mbunge ni mpeleka mawazo tu ya watu anaowakilisha kutoka katika eneo linaloitwa "jimbo la uchaguzi" katika baraza ama mkutano mkuu wa wawakilishi wa majimbo yote katika nchi yote....

Mkutano ama baraka kuu hili linaitwa "bunge"...

"Mbunge" huyu si mwamuzi wa kile watu waliomtuma wanataka kiwe; mfano kama waliomtuma wanataka wajengewe barabara ama shule ama kitu hiki ama kile.....

Absolutely, yeye hana uamuzi wa kusema watu wa jimbo la Morogoro mmenituma kupeleka ombi la mjengewe barabara ama shule ama stendi, basi mmepata tayari... Hana uamuzi huo..!!

Kupeleka mawazo ya unaowakilisha kama mbunge na kupokelewa (na mara zote huwa hivyo) ni jambo moja. Lakini kufanyiwa kazi ni kitu kingine na hapa ndipo palipo na shida....

Kufanyiwa kazi kwa mawazo ya watu anaowakilisha mbunge kunategemea mambo mengi;
å Bajeti/rasrimali fedha
å Utashi wa kisiasa wa wenye maamuzi na mamlaka
å Vipaumbele (priorities) vya nchi
å Nani anahitaji zaidi kuliko mwingine ama jimbo gani linahitaji zaidi kitu hicho hicho...
å Nk nk nk..

Kwa jukumu ama kazi ya mbunge, mtu yeyote anaweza kuwa mbunge ili mradi ana akili timamu, msikilizaji mzuri, anajali, ana uwezo wa kujenga hoja na kueleweka, mbunifu, mhamasishaji (mobilizer & motivator) mzuri wa anaowakilisha nk nk....

"Usomi" wa mbunge wa kiwango chochote "it's just an added advantage" lakini hakiwezi kuwa kigezo cha jimbo fulani kuwa guaranteed kupiga maendeleo makubwa kijamii na kiuchumi....

Na kwa taarifa na faida ya wasomaji, wengi wa "watu wasomi sana" ni kwenye viburi, watafuta vyeo tu kwa kutumia usomi wao, si wanyenyekevu, wana maringo kwa sababu ya elimu yao na tabia zingine zinazofanana na hizi. Hawa wengi hawafai kuwa wakikilishi wa watu kwenye nafasi kama ya ubunge nk.....

Kinacholeta tatizo ktk nchi yetu ni mifumo yetu ya kikatiba na kisheria ya kiutawala kuwa na matundu ama matobo tobo mengi....

Walioweka kigezo kikuu cha mwakilishi (mbunge ama diwani) kuwa na sifa ya KUJUA KUSOMA na KUANDIKA walikuwa sahihi sana kwa kuwa walizingatia jukumu/kazi ya mwakilishi huyu ni nini....

As time went on na kutokana mfumo wa utawala wa nchi ukaondoka katika lengo lake kuu yaani kuhudumia wananchi na kuwa kujinufaisha viongozi kwanza kwa gharama ya wananchi (wapiga kura)....

Wasomi wengi wakaiona fursa hii. Wengi wakawa wanaacha taaluma zao na kuingia kwenye siasa na kuanza kusaka nafasi za uongozi wa kisiasa kama uDC, uRC, uWaziri, ubunge nk nk

Watapitia wapi? Ni huko kwa wananchi kwa kuwarubuni na usomi wao kwa ahadi kuwa watatumia usomi wao kuwandolea kero ya umasikini wao hawa wananchi huku ukweli ukiwa ni kuwa wanaenda kujikwamua wao na familia zao kutoka kwenye umasikini....!!

Kwa hiyo tusidanganyane hapa....
Mkuu unachokisema kipo sahihi kwa asilimia 100.
Tatizo ni uelewa finyu wa wananchi, hapo kwenye uelewa finyu hawa washenz wanaogombea nafasi za ubunge nao wanaingia na kuahidi mambo yaliyo nje ya uwezo wao kama vile kujenga hospitali, barabarani n.k
 
Khaah!,
Nimekubali Katibu wa Mh.Aziz Abood,
Si kwa kutiririka huku.

Wala....!!

Umekosea pakubwa tu. Mimi niko zangu kwetu Shinyanga huku...

Huyo Abdul Aziz wala hata simjui ni nani. Na kiukweli hata Morogoro yenyewe siijui na sijawahi hata kuishi kwa siku mbili zaidi ya kupita barabarani naenda zangu Dsm ama sehemu zingine...

Nimechangia tu kwa kadiri nijuavyo na kufahamu....
 
Mkuu unachokisema kipo sahihi kwa asilimia 100.
Tatizo ni uelewa finyu wa wananchi, hapo kwenye uelewa finyu hawa washenz wanaogombea nafasi za ubunge nao wanaingia na kuahidi mambo yaliyo nje ya uwezo wao kama vile kujenga hospitali, barabarani n.k

Kwa kweli it's too sad...

Na afadhali hata angesema MOROGORO INAHITAJI MBUNGE TAJIRI ili ingalau akipenda atumie fedha zake kufanya hiki kinachosemwa sana blindly, "kuwaletea maendeleo wananchi"..

Hata hivyo ni tajiri gani huyo aliye tajiri kwa kiwango cha kuhudumia mamilioni ya watu kuleta maendeleo katika jimbo halafu asifilisike baada ya siku moja tu?

Hayupo huyo zaidi ya Mungu mwenyewe peke yake. Kwa binadamu mbinafsi, ni kujidanganya na kujilisha upepo tu....
 
Abood Ana watosha bado
Na htoki hapo....
Mnataka huyo msomi aje apooze njaa zake

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app

Hamna hata aibu watu wa Morogoro. Hivi kweli Aboud ni mwakilishi wa wananchi wa hali ya chini wa Morogoro? Jaribu kwenda India uone kama utapata hata uwenyekiti wa mtaa....#Gabachori
 
Nawaambieni Morogoro mlianza kuwa na akili mlipowachagua CDM, sasa kama mnataka kurudi nyuma basi endeleeni kuwachagua ccm mtabaki kama mlivyokuwa zamani, yaani moja ya mikoa midebwedo nchini.
 
Back
Top Bottom