Elections 2010 Jimbo la Ngara: Mgombea wa CCM matibabuni; wapambe wamnadi kwa picha!

Elections 2010 Jimbo la Ngara: Mgombea wa CCM matibabuni; wapambe wamnadi kwa picha!

Ni kweli, yu hoi matibabuni India, na tetesi ni kwamba huenda hatapona. CCM imempitisha mgombea ambaye ni MGONJWA MAHUTUTI, na kumuengua mgombea anayekubalika na mwenye uwezo mkubwa kuchaguliwa.

Ama kweli, siku ya kufa kwa nyani, miti yote HUTELEZA! CCM wamechanganyikiwa kiasi kwamba wanapoteza majimbo kwa maamuzi ya KIJINGA! Tayari wameshapoteza majimbo kadhaa kwa upande wa upinzani, hata kabla ya uchaguzi, likiwamo Masasi (ambayo ilikuwa ngome ya CCM mikoa ya kusini). Wanajinadi kwamba wana majimbo 10 ambayo wagombea wa CCM hawana upinzani. Lakini wamesahau, NEC inaweza kutupilia mbali pingamizi za CCM kwa wagombea wa upinzani, kwani kila siku rufaa zinakatwa. Tayari imeshatokea.

Kitaeleweka mwaka huu, kwani HATUDANGANYIKI!
 
Ni kweli, yu hoi matibabuni India, na tetesi ni kwamba huenda hatapona. CCM imempitisha mgombea ambaye ni MGONJWA MAHUTUTI, na kumuengua mgombea anayekubalika na mwenye uwezo mkubwa kuchaguliwa.

Ama kweli, siku ya kufa kwa nyani, miti yote HUTELEZA! CCM wamechanganyikiwa kiasi kwamba wanapoteza majimbo kwa maamuzi ya KIJINGA! Tayari wameshapoteza majimbo kadhaa kwa upande wa upinzani, hata kabla ya uchaguzi, likiwamo Masasi (ambayo ilikuwa ngome ya CCM mikoa ya kusini). Wanajinadi kwamba wana majimbo 10 ambayo wagombea wa CCM hawana upinzani. Lakini wamesahau, NEC inaweza kutupilia mbali pingamizi za CCM kwa wagombea wa upinzani, kwani kila siku rufaa zinakatwa. Tayari imeshatokea.

Kitaeleweka mwaka huu, kwani HATUDANGANYIKI!

Mkuu MwanaHaki,

Naomba kuuliza, maana sijui sheria ya uchaguzi inasemaje. Hivi kwa mfano mgombea yeyote ikitokea akafariki kipindi cha kampeni, je kunaweza kuwa na replacement? AU kwa maneno chama chake kinaruhusiwa ku-nominate mwingine ili kuziba pengo la mgombea?

Hilo jimbo la Masasi limepotezwa vipi na CCM? Naona hii news ya kupoteza hilo Jimbo sikuwa nimeipata. Nitashukuru iwapo unaweza kufafanunua kwenye haya mawili.
 
There is something wrong with the list. Mgombea wa ubunge Nkenge ni Mr Phocas Rwegasira.
========

Hata aliyetajwa wa Ngara kwa Chadema si mwenyewe aliyeteuliwa, bali aliteuliwa mzee mooja mstaafu wa TRA lakini jina lake nimelisahau na ndiye anapambana na Ruhuza. Huyu Ruhuza ameanza kulalamika kuwa Chadema wanamnyima pumzi wakati yeye ndiye anakubalika. Na ukweli Ruhuza ndiye angefaa pale Ngara, lakini ni huyo huyo Ruhuza aliyekuwa mwiba katika majadiliano ya kuunda umoja wa wapinzani, sasa yanamrudi.

Kuhusu mgombea kufariki wakati wa Kampeini, nadhani sheria inasema chama husika kinaruhusiwa kuteua mgombea mwingine wakati kampeini zimesimamishwa. Hali si hii si nzuri kwa mgonjwa wetu wa CCM Ngara maana tuna mafisadi wameanza kumwambia Makamba kuwa "tuzime" mashine ili afe ateuliwe mwingine ili kupata jimbo hilo.

Just thinking aloud from inside.
 
kwa jimbo la Ngara uhalisia wake ni kuwa NCCR Mageuzi HUWA INA NGUVU SANA tena hii ni toka zamani , hivyo ni vema kama wapinzani wangemsapoti bwana RUHUZA ili kumondoa huyo mnyrwanda NTUKAMAZINA kwanza sio raia ni mtusi.
 
SISIEMU yapoteza jimbo LIVE
I doubt, Mtukamazina anaweza kuchaguliwa in absentia!.
Watu wa Ngara wengi wao ni Wahangaza, hawa ni sehemu ya Intalucustrine Tribes, ni makabila ya Bahima Empire, falme ndogo ndogo za bahima ni Baganda, Mkama Rumanyika, Bunyoro etc, tabia za watu hawa ni misimamo isiyoyumba.

Kwa wafuatiliaji wa siasa za Kagera, kwa wanaomjua Masilingi, ametekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM kwa asilimia 100% kwenye jimbo lake, na bado CCM ikamtosa na kumpa Prof. Tibaijuka, sababu ni moja tuu, CV nene!.

Ukimlinganisha Mtukamazina na Ruhuza, utagundua hawatcha hata kidogo, Sam ni kijana imara, mwenye sura ya haiba ya uchangamfu, mwenye uwezo mkubwa wa kujieleza na nguvu ya hali ya juu ya ushawishi lakini CV yake ni nyepesi mno ukimlinganisha na Deo Mtukamazina. Hivyo hata bila kuongea chochote, haya makabila ya huku wanaangalia na elements za 'Nshomile'.
 
Wagombea wa Chadema Kagera na majimbo yao
KAGERA
1 Muleba Kaskzn Msedemu Milanga
2 Karagwe Deusdedit Jovin
3 Bukoba Mjini Wilfred Lwakatare
4 Kyerwa Innocent kato6 Nkenge Walter Nyahoza.
7 Bukoba vijijini Artides Ndibalema
8 Biharamulo Magharibi Dr. Anthony G. Mbassa
9 Biharamulo Mashariki Vedastus Lukumbuzya
10 Ngara Robson Robert Mushika


Mbona simwoni Arcardo Ntagazwa kwenye list? Au yeye sio huko Bukoba?
 
Mbona simwoni Arcardo Ntagazwa kwenye list? Au yeye sio huko Bukoba?

Tangu lini Jimbo la Muhambwe limehamia Mkoa wa Kagera. Ntagazwa anagombea Jimbo la Muhambwe ambalo liko mkoa wa Kigoma. Majimbo yaliyotajwa hapo juu ni ya Mkoa wa Kagera zamani ukijulikana kama Mkoa wa Ziwa Magharibi.
 
Habari nilizopata hivi punde toka jimbo la Uchaguzi la Ngara Mkoani Kagera, ni kuwa lina wagombea wawili Moja ni Ndugu Ruhuza wa NCCR na Mzee Ntukamazina. Wakati Ruhuza anapiga kampeni kwa bid bila kuwa na washabiki wengi, Mgombea wa CCM Ntukamazina yuko kwenye matibabu India baada ya kupata ajari jijini Dar.

Habari zinasema kwamba viongozi wa CCM wa wilaya wanatembeza picha ya mgombea na kuendesha kampeni mpaka hapo atakaporudi.

Habari hizi nimezipata kwa njia ya simu toka kwa rafiki yangu aliyeko jimbo hilo la uchaguzi. kama kuna aliye na habari zaidi au picha, atujuze zaidi.
jamani mnaojua sheria hivi mtu asipopiga kampeni jukwaani anaruhusiwa kuendelea kuwa mgombea hapo sheria inasemaje?au watapigia picha then anakuja kuapishwa?maana kuugua haijulikani kupona lini nisaidieni hapo jamani.
 
jamani mnaojua sheria hivi mtu asipopiga kampeni jukwaani anaruhusiwa kuendelea kuwa mgombea hapo sheria inasemaje? au watapigia picha then anakuja kuapishwa? maana kuugua haijulikani kupona lini nisaidieni hapo jamani.

Mgombea asipopiga kampeni bado anaendelea kuwa na sifa yake ya ugombea. Kwa hiyo kama mgombea anapendwa sana anaweza akachaguliwa huku akiwa amelazwa hosp.

Lakini once akishachaguliwa lazima aende kula kiapo yeye mwenyewe. Kwenye Kampeni, watu wengine wanaweza kumpigia kwa niaba, lakini kiapo lazima akale yeye mwenyewe na sio mwakilishi wala picha.
 
I doubt, Mtukamazina anaweza kuchaguliwa in absentia!.
Watu wa Ngara wengi wao ni Wahangaza, hawa ni sehemu ya Intalucustrine Tribes, ni makabila ya Bahima Empire, falme ndogo ndogo za bahima ni Baganda, Mkama Rumanyika, Bunyoro etc, tabia za watu hawa ni misimamo isiyoyumba.

Kwa wafuatiliaji wa siasa za Kagera, kwa wanaomjua Masilingi, ametekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM kwa asilimia 100% kwenye jimbo lake, na bado CCM ikamtosa na kumpa Prof. Tibaijuka, sababu ni moja tuu, CV nene!.

Ukimlinganisha Mtukamazina na Ruhuza, utagundua hawatcha hata kidogo, Sam ni kijana imara, mwenye sura ya haiba ya uchangamfu, mwenye uwezo mkubwa wa kujieleza na nguvu ya hali ya juu ya ushawishi lakini CV yake ni nyepesi mno ukimlinganisha na Deo Mtukamazina. Hivyo hata bila kuongea chochote, haya makabila ya huku wanaangalia na elements za 'Nshomile'.
Hii ni story tu au historia tangu lini watanzania wakapiga kura kwa kuangalia CV ya mtu, kwa tanzania mgombea anachaguliwa kutokana na jinsi alivyofanya kampeni hasa siku za mwishomwisho.
 
Mwanahaki naomba nikupe dondoo muhimu kutoka jimbo la Ngara. Mgombea uliyemuita mahututi ameshinda kwa kishindo. Katika kata 20 amechukua 17 na Mungu wetu aliye mwaminifu amempa afya njema Mgombea wetu mteule. Najua unaweza ukawa ulipewa information vibaya lakini wale waliodhani hatapona hakika wamezodoka
 
Phd naona unatoa information bila ya kuwa na supporting evidence. Kwanza kukusahihisha NCCR haijawahi kuwa na Nguvu ya kutisha Ngara kwasababu hata ofisi hawana na hata matawi waliyonayo hayazidi matatu.
Kukupa tu updates za Ngara ni kwamba Ntukamazina na CCM wameshinda kwa Kishindo huku wakiwaacha wapinzani wanalia.
:smile:
 
Jamani, tuwe tunaandika habari ambayo imehakikiwa. Kuhusu Ngara mgombea wa CCM ameshinda. Kama ni kuumwa, hiyo ni hali ya kawaida kwa kila binadamu; lakini kuzusha eti alikua mahututi na alikuwa ananadiwa kwa picha hilo sio la kweli kabisa. Mbunge mteule Mzee Ntukamazina yuko na afya njema, na anatakuwepo Dodoma kwa ajili ya kuapishwa pamoja na Wabunge wengine wateule!
 
PhD, sasa mwenzangu hata kama Mzee Ntukamazina ni Mtanzania, achana na mambo ya ukabila ndugu yangu. Kama angekua sio raia, sidhani kama angekua ameshika nyadhifa alizoshika katika Serikali ya Tanzania. Sehemu nyingi za mipakani makabila yanaingiliana, kuna Wamasai wanaishi Kenye na wengine Tanzania; kuna Wajaluo wanaishi Kenya na wengine Tanzania!
 
Phd naona unatoa information bila ya kuwa na supporting evidence. Kwanza kukusahihisha NCCR haijawahi kuwa na Nguvu ya kutisha Ngara kwasababu hata ofisi hawana na hata matawi waliyonayo hayazidi matatu.
Kukupa tu updates za Ngara ni kwamba Ntukamazina na CCM wameshinda kwa Kishindo huku wakiwaacha wapinzani wanalia.
:smile:

kigabogabo nakusoma,hao wanaosema mzee ntukamazina siyo mtanzania ni waongo na wanafiki,mzee ntukamazina ni mtanzania halisi na namjua fika ni uncle wangu na mimi ni mmasai mtanzania,na anapendwa balaa kapita kwa asilimia 66.Na itakuwa chachu ya maendeleo ya wananchi wa Ngara,Big up mzee ntuka
 
Ndugu wana Jamii Forum, habari za kwenu. Jamani nimesikitishwa sana na hii habari ya mbunge wa Ngara kwamba ni mgonjwa mahututi, hivi mnataka tuelewe kwamba hizi habari za humu ndani hazina uhakika? Mimi nikiwa mtu wa karibu na mzee Ntukamazina tumesikitishwa sana na hizi habari za uzushi na tunaomba hao waliotoa habari hizi za uzushi wajitaje wenyewe kabla hatujawataja maana wasipojitaja tutawachukulia hatua za sheria. Wengi wenu inawezekana mmechangia bila hata kujua wasifu wa mzee huyu ambae amelitumikia taifa la Tanzania kwa uadilifu mkubwa na ujuzi wa uongozi. Siko hapa kumlinganisha mzee Ntukamazina na wagombea wengine au kujaribu kumtetea maana CV inatosha kumuuza kokote atakapotaka kushiriki katika ujenzi wa taifa hili. Kwa taarifa yenu mzee Ntukamazina ni mzima wa afya, alipata ajali kidogo tu, hivi hata ajali mtu unaweza kuizuia? lakini yuko very fit sasa na mshindwe katika jina la YESU na maneno yenu ya eti yuko kwenye mashine na kina Makamba wanataka kuzima mashine? nimeshangazwa na vijana humu ndani kumkashifu mzee wa watu, hivi hamna wazazi nyie? na wazazi wenu wakiumwa mtawakashifu hivyo? hebu kuweni na utu na muache kuwa na kiburi cha uzima, leo mu wazima kesho hata nyie mnaweza kuumwa, je mnataka watu wawatukane kwa sababu ya tatizo la afya kidogo? Je nyie ni Mungu mnaumba watu? TAFADHALINI SANA NYIE WENYE CHUKI BINAFSI HEBU JARIBUNI KUANDIKA MAMBO YA MAANA NA SIO UMBEA MSIO NA UHAKIKA NAO, NIMESIKITISHWA SANA. KWA MODERATOR WA JAMII FORUM JARIBU KU SCAN MSG ZINAZOLETWA HUMU AMA SIVYO UTAPELEKEA KUPELEKWA MAHAKAMANI KWA KUPOST HABARI ZISIZO NA UHAKIKA. NITARUDI NA ATTACHMENT CV YA MHESHIMIWA MBUNGE WA JIMBO LA NGARA NDUGU DEOGRATIAS NTUKAMAZINA.
 
Mwanamayu acha use.nge, uraia wa mtanzania si kazi yako. Kashtaki idara ya uhamiaji. Watu kama nyie ndio mnatoka wilaya zilizofulia, with or without ccm, ngara is moving forward, nyani wewe. Mwenyewe wa wapi? Pumbavu wewe!
 
Back
Top Bottom