Jina la biashara vs Leseni

whitehorse

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2009
Posts
2,565
Reaction score
4,432
Wana JF wa uwanja huu naomba msaada kidogo kwa wenye kuelewa wanisaidie

Kwa mfano nataka kufungua biashara yangu kitu muhimu kwenye biashara ni Leseni ya Biashara.
Lakini naomba kujua je ni lazima kuandika jina la biashara kwenye leseni hiyo?

Kwa mfano

MAMA CHAUSIKU MIKATE au
MAMA CHAUSIKU NYWELE au
MAMA CHAUSIKU VIATU.

Leseni ya biashara itaandikwa jina hilo au inaweza kuandikwa jina langu mwenyewe mmiliki?

Msaada tafadhali
 
Vyote vitaandikwa nadhani!
 
Vyote vitaandikwa nadhani!
Mfano we ni mwajuma abdul na una jina la biashara ambalo limesajiliwa mfano mwajay general supply.
Kwenye leseni itaandikwa hivi

Mwajuma abdul (Mwajay General Supply)

So vitaandikwa vyote
 
Jina la biashara itategemea na TIN namba umeandika jina gani na vile vile kama umesajili jina la Biashara BRELA. Hii ipo hivi
1. Tukianza Brela
Kama umesajili jina lako la biashara mathalani tusema Mamaa Manywele utakuwa na vile vielelezo viwili yaani cheti cha usajili na extract
2. TIN namba
Ukipeleka TRA hivyo vielelezo viwili watasajili jina lako halisi mathalani jina lako Agnes Mpambe na jina lililosajiliwa Brela. Hivyo Tin namba yako itakuwa inasoma AGNES MPAMBE T/A MAMAA MANYWELE.Kama hujapeleka hivyo vielelezo vya Brela, TIN namba itasoma tu AGNES MPAMBE
3. Leseni ya biashara
Tin namba yako ndiyo itakayotoa maelekezo ya leseni yako ya biashara iandikwe majina gani. Kama Tin namba imeandikwa Agnes Mpambe T/a Mamaa Manywele na leseni itasomeka hivyo na kama iliandikwa Agnes Mpambe, leseni nayo itasomeka majina hayo tu
Naamini utakuwa umepata mwanga wa nini ulichotaka kujua
 
Je katika kuanza biashara unaweza kupata Tin na leseni bila ya kusajili jina la biashara brela?
 
Je ili kuanza biashara ya kawaida ni lazima kusajili jina la biashara brela?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…