Midekoo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2015
- 45,757
- 246,786
JINA LAKE
Ameitwa JINNI kwa sababu ya kutokuonekana kwake na watu, na hii ni kwa sababu kila kisichoonekana kwa jicho la binadamu katika lugha ya kiarabu jina lake hutokana (hutoholewa) na herufi mbili hizi; (Jiym) na (Nuun).
Kwa mfano; 'Bustani' huitwa 'janna' kwa sababu ya kuzungukwa kwake na majani kila upande pasiweze kuonekana ndani. Elimu ya uzazi huitwa 'Ilmul ajinna', kwa sababu ya kutokuonekana kwa kile kilichokuwemo tumboni mwa mzazi. Hata mwendawazimu naye huitwa 'majinun' kwa sababu ya kutoweka kwa akili yake. NaMajinni nao wamepewa jina hilo kwa sababu ya kutokuonekana kwao kwa macho ya binadamu.
Ukichunguza utaona kuwa maneno yote hayo; 'Janna, ajinna, majinun, jinni', yana herufi ya 'Jiym na Nuun' ndani yake.
IMANI JUU YA GHAIBU
Kuamini juu ya ghaibu (yasiyoonekana) ni katika misingi ya itikadi ya Dini.
Allaah Anasema:
"Alif Laam Miym. Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake.Ni uwongozi kwa wamchao Allaah. Ambao huyaamini yasiyoonekana (maadam yamesemwa na Allaah na Mtume Wake) na husimamisha Sala na hutoa katika yale Tuliyowapa".
Al Baqarah
Katika aya hizi, Allaah ametaja baadhi ya sifa za wachaji Allaah ikiwemo ikiwemo sifa hii ya kuamini Ghaibu.
Na maana ya neno 'Ghaibu', ni yale tusiyoweza kuyaona tuliyofundishwa na Allaah Subhaanahu waTaala au Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam).
USHAHIDI WA KUWEPO MAJINI KATIKA QUR-AAN TUKUFU
Katika Qur-aan Allaah Anasema:
"Na (wakumbushe) tulipokuletea kundi la majini (kuja kwako) kusikiliza Qur-aan."
Al Ahqaf - 29
Na Akasema:
"(Siku ya Qiyaamah wataambiwa) “Enyi makundi ya majini na wanaadamu! Je, hawajakufikieni Mitume miongoni mwenu kukubainishieni Aya zangu?"
Al An am 130
Itaendelea.......... .............
Ameitwa JINNI kwa sababu ya kutokuonekana kwake na watu, na hii ni kwa sababu kila kisichoonekana kwa jicho la binadamu katika lugha ya kiarabu jina lake hutokana (hutoholewa) na herufi mbili hizi; (Jiym) na (Nuun).
Kwa mfano; 'Bustani' huitwa 'janna' kwa sababu ya kuzungukwa kwake na majani kila upande pasiweze kuonekana ndani. Elimu ya uzazi huitwa 'Ilmul ajinna', kwa sababu ya kutokuonekana kwa kile kilichokuwemo tumboni mwa mzazi. Hata mwendawazimu naye huitwa 'majinun' kwa sababu ya kutoweka kwa akili yake. NaMajinni nao wamepewa jina hilo kwa sababu ya kutokuonekana kwao kwa macho ya binadamu.
Ukichunguza utaona kuwa maneno yote hayo; 'Janna, ajinna, majinun, jinni', yana herufi ya 'Jiym na Nuun' ndani yake.
IMANI JUU YA GHAIBU
Kuamini juu ya ghaibu (yasiyoonekana) ni katika misingi ya itikadi ya Dini.
Allaah Anasema:
"Alif Laam Miym. Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake.Ni uwongozi kwa wamchao Allaah. Ambao huyaamini yasiyoonekana (maadam yamesemwa na Allaah na Mtume Wake) na husimamisha Sala na hutoa katika yale Tuliyowapa".
Al Baqarah
Katika aya hizi, Allaah ametaja baadhi ya sifa za wachaji Allaah ikiwemo ikiwemo sifa hii ya kuamini Ghaibu.
Na maana ya neno 'Ghaibu', ni yale tusiyoweza kuyaona tuliyofundishwa na Allaah Subhaanahu waTaala au Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam).
USHAHIDI WA KUWEPO MAJINI KATIKA QUR-AAN TUKUFU
Katika Qur-aan Allaah Anasema:
"Na (wakumbushe) tulipokuletea kundi la majini (kuja kwako) kusikiliza Qur-aan."
Al Ahqaf - 29
Na Akasema:
"(Siku ya Qiyaamah wataambiwa) “Enyi makundi ya majini na wanaadamu! Je, hawajakufikieni Mitume miongoni mwenu kukubainishieni Aya zangu?"
Al An am 130
Itaendelea.......... .............