Midekoo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2015
- 45,757
- 246,786
- Thread starter
- #41
KUJIKINGA NA SHARI ZA WACHAWI NA MAJINI WAO
Zifuatazo ni baadhi ya Njia za kujikinga na waovu hao:
KUSAFISHA NIA
Ibilisi alipohukumiwa kupotea kwa sababu ya kuasi kwake, aliahidi kuwapoteza viumbe wote isipokuwa wale waliosafika kikweli.
Ibilisi akasema kumwambia Allaah:
"Isipokuwa wale waja wako waliosafika kweli kweli."
Kusafisha nia (Al Ikhlas), maana yake ni kuzihusisha Ibada zote kwa moyo wote kwa ajili ya Allaah peke yake, siyo kujionyesha mbele za watu kuwa ni Mcha Mungu na unapokuwa peke yako unamuasi.
Al Junaid, mmoja katika maulamaa wakubwa wa wakati wake amesema:
"Allaah ana waja wake wenye akili, walipopata akili wakaifanyia kazi, walipofanya kazi wakaitakasa kazi hiyo na kule kuitakasa kwao kukawaingiza katika milango ya kheri yote."
KUTIA UDHU
Katika hadithi nyingi Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) ametufundisha juu ya umuhimu wa kubaki na udhu kila mtu anapoweza kwa ajili ya kupata thawabu na kwa ajili ya kujikinga na kila shari.
SWALA KATIKA JAMAA
KusWali sWala za jamaa msikitini, maana Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) ametufundisha kwamba mbwa mwitu (Shaytwaan) huwala kondoo wanaotembea mbali na wenzao.
SWALA ZA SUNNAH
Swala za Sunnah uziswali nyumbani, usiiache nyumba yako ikawa kama kaburi, na unaposwali nyumbani Shaytwaan hulia na kutoka nje ya nyumba yako huku akisema;
"Sina pa kulala humu, wala sina pa kula humu".
KUMUOMBA ALLAAH
Kumuomba Allaah kila mara Shaytwaan anapotaka kukuchezea na kila unapoingia mahali pachafu. Kwa mfano:
Unapoingia chooni uisome dua ifuatayo:
"Allaahumma inniy audhu bika minal khubuthi wal khabaaith). Na maana yake; (Allaah mimi najikinga kwako kutokana na majini wanaume na majini wanawake).
Kabla ya kulala usome Suratul Ikhlaas, Suratul Falaq na Suratul Naas pamoja na AyatulKursy, maana hadithi sahihi tuliyoitaja mwanzo wa darsi hii inasema kuwa anayeisoma aya hii, Allaah anaendelea kumhifadhi mpaka asubuhi anapoamka.
Ni vizuri pia kuzisoma aya tano za mwanzo za SuratulBaqarah kisha Ayatul Kursy kisha kuzisoma aya tatu za mwisho za Suratul Baqarah na Allaah Atakulinda na majini pamoja na uchawi katika siku nzima.
Kuzisoma dua mbali mbali kama vile:
(Audhu bikalimati Allaahi ttaamah min kulli shaytanin wa haammah wa min kulli aynin laammah).
Na maana yake ni;
"Najikinga kwa Allaah kutokana na kila Shaytwaan na (kila) mdudu anayesota (kama vile nge na nyoka nk. na kwa kila jicho linalodhuru).
(BismiAllaahi lladhiy laa yadhuru ma-a smihiy shayun fil ardhi walaa fiy ssamaa wahuwa ssamiyl aliym).
Unapotoka nje ya nyumba usome:
(BismiAllaah tawakkaltu ala Allaah walaa haula walaa quwwata illa biAllaah)
Zifuatazo ni baadhi ya Njia za kujikinga na waovu hao:
KUSAFISHA NIA
Ibilisi alipohukumiwa kupotea kwa sababu ya kuasi kwake, aliahidi kuwapoteza viumbe wote isipokuwa wale waliosafika kikweli.
Ibilisi akasema kumwambia Allaah:
"Isipokuwa wale waja wako waliosafika kweli kweli."
Kusafisha nia (Al Ikhlas), maana yake ni kuzihusisha Ibada zote kwa moyo wote kwa ajili ya Allaah peke yake, siyo kujionyesha mbele za watu kuwa ni Mcha Mungu na unapokuwa peke yako unamuasi.
Al Junaid, mmoja katika maulamaa wakubwa wa wakati wake amesema:
"Allaah ana waja wake wenye akili, walipopata akili wakaifanyia kazi, walipofanya kazi wakaitakasa kazi hiyo na kule kuitakasa kwao kukawaingiza katika milango ya kheri yote."
KUTIA UDHU
Katika hadithi nyingi Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) ametufundisha juu ya umuhimu wa kubaki na udhu kila mtu anapoweza kwa ajili ya kupata thawabu na kwa ajili ya kujikinga na kila shari.
SWALA KATIKA JAMAA
KusWali sWala za jamaa msikitini, maana Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) ametufundisha kwamba mbwa mwitu (Shaytwaan) huwala kondoo wanaotembea mbali na wenzao.
SWALA ZA SUNNAH
Swala za Sunnah uziswali nyumbani, usiiache nyumba yako ikawa kama kaburi, na unaposwali nyumbani Shaytwaan hulia na kutoka nje ya nyumba yako huku akisema;
"Sina pa kulala humu, wala sina pa kula humu".
KUMUOMBA ALLAAH
Kumuomba Allaah kila mara Shaytwaan anapotaka kukuchezea na kila unapoingia mahali pachafu. Kwa mfano:
Unapoingia chooni uisome dua ifuatayo:
"Allaahumma inniy audhu bika minal khubuthi wal khabaaith). Na maana yake; (Allaah mimi najikinga kwako kutokana na majini wanaume na majini wanawake).
Kabla ya kulala usome Suratul Ikhlaas, Suratul Falaq na Suratul Naas pamoja na AyatulKursy, maana hadithi sahihi tuliyoitaja mwanzo wa darsi hii inasema kuwa anayeisoma aya hii, Allaah anaendelea kumhifadhi mpaka asubuhi anapoamka.
Ni vizuri pia kuzisoma aya tano za mwanzo za SuratulBaqarah kisha Ayatul Kursy kisha kuzisoma aya tatu za mwisho za Suratul Baqarah na Allaah Atakulinda na majini pamoja na uchawi katika siku nzima.
Kuzisoma dua mbali mbali kama vile:
(Audhu bikalimati Allaahi ttaamah min kulli shaytanin wa haammah wa min kulli aynin laammah).
Na maana yake ni;
"Najikinga kwa Allaah kutokana na kila Shaytwaan na (kila) mdudu anayesota (kama vile nge na nyoka nk. na kwa kila jicho linalodhuru).
(BismiAllaahi lladhiy laa yadhuru ma-a smihiy shayun fil ardhi walaa fiy ssamaa wahuwa ssamiyl aliym).
Unapotoka nje ya nyumba usome:
(BismiAllaah tawakkaltu ala Allaah walaa haula walaa quwwata illa biAllaah)