Freed Freed
JF-Expert Member
- Jun 27, 2017
- 6,547
- 7,167
Jino la waziri Mkuu wa kwanza wa Congo limeibiwa jijini Kinshasa. Ikumbukwe waziri Mkuu Patrice Emilio Lumumba aliuliwa mwaka 1961 na Mwili wake kuyeyushwa kwenye tindikali.
Ilivyo bahati mmoja wa wauaji Askari Mbeligiji aliliondoa jino lake kwa siri bila kumfahamisha mtu yeyote. Baadae aliitoa siri hiyo na kudai amelificha nyumbani kwake Ubelgiji baada ya miaka mingi kupita.
Serikali ya Congo DRC iliwasiliana na serikali ya Ubelgiji na Askari huyo na jino kurudishwa nyumbani ikiwa ndani ya Jeneza na kuhifadhiwa eneo maalumu jijini Kinshasa mwaka 2022.
Nyumba maalumu iliyohifadhi jeneza na jino imeharibiwa usiku wa jumapili 17/11/2024 na jino kuibiwa na watu wasiojulikana.
Hata hivyo walinzi wa Rais waliliona jeneza likitoroshwa na kuliokoa huku jino halipo ndani na waporaji walishakimbia. Inadaiwa kaburi hilo halikuwa na ulinzi maalumu japo halipo mbali na Ikulu ya Kinshasa.
Awali kurejeshwa kwa jino hilo kulipokelewa kwa shangwe na wakongomani wa matabaka yote.
Ilivyo bahati mmoja wa wauaji Askari Mbeligiji aliliondoa jino lake kwa siri bila kumfahamisha mtu yeyote. Baadae aliitoa siri hiyo na kudai amelificha nyumbani kwake Ubelgiji baada ya miaka mingi kupita.
Serikali ya Congo DRC iliwasiliana na serikali ya Ubelgiji na Askari huyo na jino kurudishwa nyumbani ikiwa ndani ya Jeneza na kuhifadhiwa eneo maalumu jijini Kinshasa mwaka 2022.
Nyumba maalumu iliyohifadhi jeneza na jino imeharibiwa usiku wa jumapili 17/11/2024 na jino kuibiwa na watu wasiojulikana.
Hata hivyo walinzi wa Rais waliliona jeneza likitoroshwa na kuliokoa huku jino halipo ndani na waporaji walishakimbia. Inadaiwa kaburi hilo halikuwa na ulinzi maalumu japo halipo mbali na Ikulu ya Kinshasa.
Awali kurejeshwa kwa jino hilo kulipokelewa kwa shangwe na wakongomani wa matabaka yote.