Jinsi HR officers wanavyoua ndoto za vijana wengi

Jinsi HR officers wanavyoua ndoto za vijana wengi

Bunchari

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2017
Posts
558
Reaction score
661
Habari wakuu

Katika pilika pilika za kutafuta ajira,nilijaribu kutuma maombi taasisi fulani ,mchakato wa maombi ulipokamilika nikapigiwa simu na hr nimekua selected hivyo niende kuonana naye.

Nilipofika ofisini kwake,akaniagiza siku inayofuata niende na watu watakao nidhamini niliitikia wito nikawachukua jamaa tukaenda, akanielekeza majukumu,mshahara utakua kiasi gani na mambo mengine ya kazi kisha akanielekeza niende nitapigiwa simu siku ya kuja kuanza kazi rasmi nikaitikia sawa kisha nikaondoka.

Nimekaa karibu mwezi mzima pasipokupokea simu toka kwa HR au mwakilishi yoyote toka ile ofisi nikapata wasiwasi labda nimesahaulika ikabidi niende kuulizia nilipofika nikasalimiana kidogo na mlinzi katika mazungumzo akaniambia mbona wenzako wameishaanza kazi kitambo, kiukweli nimejiskia vibaya nikaamua kuingia ndani ili kujiridhisha kama ni kweli nikakuta jamaa hayupo ofisi imefungwa sikupata majibu.

Ikabidi nikae chini najiuliza maswali,lengo la HR kufanya hivi ni nini mbona kanifedhehesha vibaya si angenipotezea wakati wa selection tusingefikishana huku.

Daah hii dunia hii
 
Siku nyingine ukiambiwa leta wazamn hasa kwa kaz za marketing jtahd kupeleka watu presentable na wanaoonekana wako comited kwenye ishu yako apo hr alisoma saikolojia ya uliowaleta akaona apa naingizwa chaka mchana kweupe
 
Usilaumu HR!
Je wewe ni Msafi?
Je, watu walioenda kukudhamini ni wasafi?
Hapo ilipigwa bonge ya Vetting ukakutwa na dosari, endelea kupambana
Taaasisi siyo hiyo moja pekee. Kama ipo ipo tu!
Tujitahidi kuwa waaminifu na Waadilifu ukikaidi utaishia kulaumu watu bureee
 
Huyo HR usimlazie damu. Hakikisha unamvizia ili siku akiwepo tu ofisini unaenda kumchana waziwazi mbele ya hao subordinates wake ya kwamba yeye ni Snitch.

Halafu ukitoka tu kumchana, nitafute faster ili nikutumie hela ya kwenda kupoza koo.
 
Nilipofika ofisini kwake,akaniagiza siku inayofuata niende na watu watakao nidhamini niliitikia wito nikawachukua jamaa tukaenda,
Khaaaaa!
Yaani ukokote watu wazima waaache shughuli zao kwenda kukudhamini uso kwa uso
Hii ni taasisi gani?
 
Pole sana mkuu, mwenyw Kuna simu Niliambiwa nitapigiwa nipo tuu naiskizia daah 😂

Ila referees wako waeke watu ambao ni presentable, wasiwe ndugu, inakuwa poa zaidi
 
mkuu siku nyingine peleka watu wenye hadhi ya kueleweka, Kama wafanyakazi wa taasisi au wamiliki wa biashara fulani.
(Yenye kufanana na hiyo).

*Wenye kuelewa unacho enda kufanya, au kuweza kuthibitisha kuwa una aminika.

Pengine uli enda na watu wapo rough au sio wasomi wa issue husika, akaona Kama hauko serious!.
 
Habari wakuu

Katika pilika pilika za kutafuta ajira,nilijaribu kutuma maombi taasisi fulani ,mchakato wa maombi ulipokamilika nikapigiwa simu na hr nimekua selected hivyo niende kuonana naye.

Nilipofika ofisini kwake,akaniagiza siku inayofuata niende na watu watakao nidhamini niliitikia wito nikawachukua jamaa tukaenda, akanielekeza majukumu,mshahara utakua kiasi gani na mambo mengine ya kazi kisha akanielekeza niende nitapigiwa simu siku ya kuja kuanza kazi rasmi nikaitikia sawa kisha nikaondoka.

Nimekaa karibu mwezi mzima pasipokupokea simu toka kwa Hr au mwakilishi yoyote toka ile ofisi nikapata wasiwasi labda nimesahaulika ikabidi niende kuulizia nilipofika nikasalimiana kidogo na mlinzi katika mazungumzo akaniambia mbona wenzako wameishaanza kazi kitambo, kiukweli nimejiskia vibaya nikaamua kuingia ndani ili kujiridhisha kama ni kweli nikakuta jamaa hayupo ofisi imefungwa sikupata majibu.

Ikabidi nikae chini najiuliza maswali,lengo la hr kufanya hivi ni nini mbona kanifedhehesha vibaya si angenipotezea wakati wa selection tusingefikishana huku.

Daah hii dunia hii
Saa nyingine unaweza kukuta HR wala hana makosa. Inawezekana kweli wewe ndio ulistahili hiyo kazi na HR akakuita, ila baada ya wewe kuondoka kikaja "kimemo" kutoka juu kwamba hiyo kazi usimpe mtu nna kijana wangu anakuja kuanza kesho.

Ndio hivyo tena 😐
 
Ukiona hivyo ujue hiyo office ni ya magumashi
 
Back
Top Bottom