Elections 2015 Jinsi jina la Edward Lowassa lilivyokatwa Kamati ya Maadili CCM

Elections 2015 Jinsi jina la Edward Lowassa lilivyokatwa Kamati ya Maadili CCM

Ng'wamapalala

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2011
Posts
6,811
Reaction score
6,503
MVURUGANO mkubwa ulizuka katika kikao cha Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya wajumbe wanaomuunga mkono Edward Lowassa, kubaini jina lake limekatwa.

Hali ilikuwa hivyo baada ya majina matano ya watangaza nia kutoka Kamati ya Usalama na Maadili ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwasilishwa katika Kamati Kuu.

Majina hayo matano ni Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba na Balozi Amina Salum Ally.

Watetezi wa Lowassa waliongozwa na Dk. Emmanuel Nchimbi, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Sophia Simba, Meya wa Ilala, Jerry Silaa, Mbunge wa Afrika Mashariki, Adam Kimbisa na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Sadifa Khamis.

Aliyeanza kuhoji viongozi wa Kamati Kuu kuhusu kufyekwa kwa majina mengine ya watangaza nia, akiwamo Lowassa alikuwa Nchimbi ambaye kama wenzake hao, alitaka kujua sababu za kuenguliwa watangaza nia wengine.

Kundi hilo lilidai kwamba hakuna sababu nzito zilizotumika kuwang’oa watangaza nia wengine na kama hoja ni tuhuma za ufisadi, hiyo ni hoja isiyokuwa na nguvu, kwa mujibu wa mtazamo wao.

Taarifa kutoka ndani ya kikao cha Kamati Kuu kilichoketi mjini Dodoma, zinaeleza kwamba safu hiyo ya watetezi wa Lowassa ilikuwa ikipeana ‘pasi’ kujenga hoja za kushinikiza kuongezwa kwa majina mengine mbali na hayo matano ili yafanyiwe kazi na kikao hicho.

Alikuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi CCM, Abdallah Bulembo ndiye aliyeingilia kati na kuwataka akina Nchimbi kuheshimu viongozi wakuu waliokuwamo kwenye kikao hicho, akipinga hali iliyokuwa ikijitokeza ya kujadili suala hilo kwa njia ya kejeli.

“Watu waheshimu viongozi waliomo humu ndani. Tunao viongozi humu wametumikia Taifa kwa juhudi na umakini mkubwa, wanaheshimika nasi lazima tuwaheshimu na tuheshimu uamuzi uliofikiwa ambao umeshirikisha hawa viongozi wetu (kwenye Kamati ya Usalama na Maadili),” alisema Bulembo ambaye alikuwa akitetea majina matano bora ya watangaza nia wa CCM.

Baada ya Bulembo, alifuatia Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye ambaye alifikia hatua ya kumtaja baba yake mzazi, Moses Nnauye aliyekuwa kada mhamasishaji kindakindaki wa CCM kwa miaka mingi chini ya uenyekiti wa Mwalimu Julius Nyerere na baadaye Ali Hassan Mwinyi.

“Taifa hili linahitaji kuongozwa kwa umakini na watu makini. Taifa linahitaji umakini na busara ya hali ya juu. Tusikubali hata kidogo kuruhusu Kamati Kuu ya Chama hiki ibariki mchezo wa kununua uongozi. Si busara kwa Kamati Kuu kuwa chanzo cha kuruhusu watu kununua madaraka. Lazima kubadilisha mfumo. Tukiruhusu hali hii, masikini hawatakuwa na chao, hawatapata nafasi na sisi wengine tusio na fedha za kununua madaraka itabidi tuondoke humu.

“Inasikitisha watu wapo tayari humu ndani (Kamati Kuu) kutetea ununuzi wa madaraka. Mimi baba yangu (Mzee Moses Nnauye) amefanya kazi kwenye hiki chama kwa uaminifu mkubwa, kwa miaka mingi hadi anaondoka hakuwahi hata kuwa na nyumba, leo watu wananunua uongozi, wengine siku mbili tatu baada ya kupata madaraka ana nyumba nyingi,” alisema Nape.

Baada ya Nape, alizungumza Zakhia Meghji ambaye kwa ukali aliwataka wajumbe wa Kamati Kuu kuheshimu uamuzi wa Kamati ya Usalama na Maadili akisema imeongozwa na Mwenyekiti Kikwete ambaye kwa nafasi yake ya Urais, anazo taarifa za kina kuhusu watangaza nia wote.

“Kamati Kuu lazima iwe na ujasiri. Mwenyekiti anazo taarifa zote tena za kina, kwa hiyo lazima wanazo sababu za msingi za kuleta humu majina matano,” alisema Meghji kwa mujibu wa nukuu ya chanzo chetu cha habari kutoka kikaoni humo.

Rais msitaafu Benjamin Mkapa naye alizungumza kwa ukali akisema; “Tunapata wapi ujasiri wa namna hii wa kutetea maslahi binafsi? Naona hapa ni mtu kwanza chama baadaye, si chama kwanza mtu baadaye. “Hapa hakuna mwenye taarifa za kina kama Mwenyekiti. Ni nani huyo mwenye taarifa za kina kumshinda Mwenyekiti? Tuna imani na uamuzi wa Kamati ya Maadili”.

Naye Mzee Mwinyi alisema; “Ni lazima tuheshimu kiti. Lazima muwe na uwezo wa kukubaliana na mambo yanavyokwenda. Nashangaa watu wapo tayari kukitishia chama, nguvu hizi za kukitisha chama mnazitoa wapi?”

Waziri Mkuu wa zamani, John Malecela, yeye alitoa mfano wake mwenyewe namna Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere alivyomwondoa kwenye kinyang’anyiro cha urais mwaka 1995.

“Lazima tuheshimu mamlaka, Mwenyekiti anazo taarifa nyingi. Mimi mwaka 1995 Mwalimu Nyerere alining’oa na akasema kama nitapewa nafasi CCM yeye ataondoka, anakwenda kuanzisha chama. Mimi nikanyoosha mikono na kujitoa, Mwalimu akanifuata na kunikumbatia,” alisema Malecela ambaye alikuwa akisisitiza wajumbe wenzake wakubaliane na hali halisi.

Mzee Malecela ambaye alikuwa nje ya nchi kwa matibabu, alilazimika kutopumzika ili kuungana na wazee wenzake kuokoa jahazi lililoelekea kuzamishwa na nguvu ya fedha.

Rais msitaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, kama ilivyokuwa kwa wenzake, naye aliweka bayana kuunga mkono uamuzi wa Kamati ya Usalama na Maadili akisema ni uamuzi uliopaswa kuungwa mkono.

Baada ya jina lake kutofikishwa Kamati Kuu na baadaye kushindwa kuilazimisha jina lake lirudishwe NEC, wapambe wa Lowassa wanadaiwa kuandaa mpango wa kutaka kumsaidia Balozi Amina aweze kupitishwa kuwa mgombea wa urais wa CCM, ili naye baadaye amtangaze Lowassa kuwa Mgombea Mwenza na hatimaye aweze kuwa Makamu wa Rais.

Mkakati huo ulitiwa nguvu na Balozi Amina mwenyewe wakati akijieleza kuomba kura ambaye mara mbili alisema kwamba alikuwa tayari kufanya kazi na Lowassa.

Hata hivyo, habari zinasema mpango huo ulikuja kuvuja kutokana na papara za baadhi ya wapenzi wa Lowassa kuanza kampeni za wazi kwa ajili hiyo katika Mkutano Mkuu ili Balozi Amina ashinde kwa kura nyingi.

Kwa hisani ya RaiaMwema.
 
Kama hii habari ni kweli, basi niwapongeze sana CCM angalau kwa kuthubutu kukata gogo lililojidai halikatiki!

Hakika huu ulikuwa mtihani mkubwa sana kwa CCM. Haijapata kutokea kiongozi au mwanachama akaitisha CCM kiasi hiki!

Wengi walidhani kweli hili hogo halikatwi!

CCM ingejitakia balaa huko mbele ya safari kama isingekata! Tena kwa mkato mkali!

Hongereni sana! Dawa ya kiungo kilichooza mwilini ni kukatwa! Kukiacha ni kujichulia kifo!
 
Hakuna siku nilifarijika pale MTU aliyejitanabahisha kuwa juu ya uongozi Wa chama na nchi. Liwe fundisho kwa Sikh zijazo kwa watu wasio na shukrani katika nchi hii wanaofikiri pesa ndo kilakitu.
 
Kati ya wote hao ni nani msafi wa kumuhukumu mwenzie zaidi ya kulinda maslahi yao tu?

Aliyejiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kutupa anawezaje leo hii kuhoji ya Lowassa?

Alieshirikiana na Lowassa kwenye Richmond anaweza vipi leo hii kumtuhumu Lowassa?

Kashifa ya Richmond ilipozimwa kihuni Bungeni ni nani kati ya maraisi hao wastaafu na huyu aliepo madarakani leo hii alijitokeza hadharani kupinga na kukemea uamuzi huo batili wa Bunge?!

Aliehusika kumvua madaraka ya uwaziri mh. Mrema eti kwa kile kilichoitwa kukiuka dhana ya "collective responsibility" wakati Mrema alijitoa kulinda maslahi ya Taifa anaweza vipi leo hii kuhoji ya Lowassa?

Watu(wastaafu) hawa waliokaa kimya na kujifanya viziwi kuhusiana na yaliyokuwa yanaendelea kuhusiana na Escrow,Richmond na EPA leo hii wamepata wapi uzalendo wa kututafutia kiongozi bora?1

Huu ni unafiki wa kiwango cha juu sana!!
 
Kama hii habari ni kweli, basi niwapongeze sana CCM angalau kwa kuthubutu kukata gogo lililojidai halikatiki!

Hakika huu ulikuwa mtihani mkubwa sana kwa CCM. Haijapata kutokea kiongozi au mwanachama akaitisha CCM kiasi hiki!

Wengi walidhani kweli hili hogo halikatwi!

CCM ingejitakia balaa huko mbele ya safari kama isingekata! Tena kwa mkato mkali!

Hongereni sana! Dawa ya kiungo kilichooza mwilini ni kukatwa! Kukiacha ni kujichulia kifo!

Mkuu Ng'wamapalala Unanishangaza unaposema unaipongeza ccm kwa kumkata Lowasa zaidi umejishusha thamani yako unaposema mtu hawezi kukitisha chama na unashangaza zaidi unaposema chama ndio kenye maamuzi ya mwisho.

Ashamkun si matusi, Upumbavu wako ni unaposema chama ndio kenye maamuzi ya mwisho bila kujua kuwa wanachama ndio chama chenyewe na haiwezekani KITENGO kikafanya maamuzi ya wanachama wote.

Pia hujue kuwa kamati kuu ndio chombo pekee kilichotakiwa kifanye uchujaji wa majina 38 ya watangaza nia kwa njia ya upigaji kura ili kuyapata hayo majina 5 na 3. Na badala yake kikafanyika ubatili mkuuu uliofanya ubatili wao na kuwakata watangaza nia na kumpitisha mtu wao.

Kwakuwa Makufuli kapitishwa na chama chake kwa njia ya uvunjaji wa katiba na dhuluma nyingi na yeye binafsi analijua hilo...

Je! Makufuli akiwa Raisi wa Tanzania atapata wapi ujasiri wa kusimamia katiba na kukomesha dhuluma na ubatili wakati chimbuko la uraisi wake ni Dhuluma, uvunjifu wa katiba na ubatili mtupu?
 
Umeelezea sababu tosha za kuonyesha uhuni na ufisafi wa hawa wanafiki wa chama cha wahuni na mafisadi.

Kati ya wote hao ni nani msafi wa kumuhukumu mwenzie zaidi ya kulinda maslahi yao tu?

Aliyejiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kutupa anawezaje leo hii kuhoji ya Lowassa?

Alieshirikiana na Lowassa kwenye Richmond anaweza vipi leo hii kumtuhumu Lowassa?

Kashifa ya Richmond ilipozimwa kihuni Bungeni ni nani kati ya maraisi hao wastaafu na huyu aliepo madarakani leo hii alijitokeza hadharani kupinga na kukemea uamuzi huo batili wa Bunge?!

Aliehusika kumvua madaraka ya uwaziri Mrema kwasababu tu Mrema alijitoa kulinda maslahi ya Taifa anaweza vipi leo hii kuhoji ya Lowassa?

Watu(wastaafu) hawa waliokaa kimya na kujifanya viziwi kuhusiana na yaliyokuwa yanaendelea kuhusiana na Escrow,Richmond na EPA leo hii wamepata wapi uzalendo wa kututafutia kiongozi bora?1

Huu ni unafiki wa kiwango cha juu sana!!
 
Kama hii habari ni kweli, basi niwapongeze sana CCM angalau kwa kuthubutu kukata gogo lililojidai halikatiki!

Hakika huu ulikuwa mtihani mkubwa sana kwa CCM. Haijapata kutokea kiongozi au mwanachama akaitisha CCM kiasi hiki!

Wengi walidhani kweli hili hogo halikatwi!

CCM ingejitakia balaa huko mbele ya safari kama isingekata! Tena kwa mkato mkali!

Hongereni sana! Dawa ya kiungo kilichooza mwilini ni kukatwa! Kukiacha ni kujichulia kifo!
Kwa hiyo unawapongeza kwa kuvunja kanuni zao ili tu wamkate Lowassa. Hivi kulikuwa na ugumu gani kupeleka taarifa za wagombea wote na kuwapa sababu za msingi kwa nini hao watano ndiyo bora badala ya kujificha nyuma ya 'mwenyekiti ana taarifa nyingi'
 
mkuu asante sana kwa taarifa iliyoenda shule.

MVURUGANO mkubwa ulizuka katika kikao cha Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya wajumbe wanaomuunga mkono Edward Lowassa, kubaini jina lake limekatwa.

Hali ilikuwa hivyo baada ya majina matano ya watangaza nia kutoka Kamati ya Usalama na Maadili ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwasilishwa katika Kamati Kuu.

Majina hayo matano ni Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba na Balozi Amina Salum Ally.

Watetezi wa Lowassa waliongozwa na Dk. Emmanuel Nchimbi, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Sophia Simba, Meya wa Ilala, Jerry Silaa, Mbunge wa Afrika Mashariki, Adam Kimbisa na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Sadifa Khamis.

Aliyeanza kuhoji viongozi wa Kamati Kuu kuhusu kufyekwa kwa majina mengine ya watangaza nia, akiwamo Lowassa alikuwa Nchimbi ambaye kama wenzake hao, alitaka kujua sababu za kuenguliwa watangaza nia wengine.

Kundi hilo lilidai kwamba hakuna sababu nzito zilizotumika kuwang'oa watangaza nia wengine na kama hoja ni tuhuma za ufisadi, hiyo ni hoja isiyokuwa na nguvu, kwa mujibu wa mtazamo wao.

Taarifa kutoka ndani ya kikao cha Kamati Kuu kilichoketi mjini Dodoma, zinaeleza kwamba safu hiyo ya watetezi wa Lowassa ilikuwa ikipeana ‘pasi' kujenga hoja za kushinikiza kuongezwa kwa majina mengine mbali na hayo matano ili yafanyiwe kazi na kikao hicho.

Alikuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi CCM, Abdallah Bulembo ndiye aliyeingilia kati na kuwataka akina Nchimbi kuheshimu viongozi wakuu waliokuwamo kwenye kikao hicho, akipinga hali iliyokuwa ikijitokeza ya kujadili suala hilo kwa njia ya kejeli.

"Watu waheshimu viongozi waliomo humu ndani. Tunao viongozi humu wametumikia Taifa kwa juhudi na umakini mkubwa, wanaheshimika nasi lazima tuwaheshimu na tuheshimu uamuzi uliofikiwa ambao umeshirikisha hawa viongozi wetu (kwenye Kamati ya Usalama na Maadili)," alisema Bulembo ambaye alikuwa akitetea majina matano bora ya watangaza nia wa CCM.

Baada ya Bulembo, alifuatia Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye ambaye alifikia hatua ya kumtaja baba yake mzazi, Moses Nnauye aliyekuwa kada mhamasishaji kindakindaki wa CCM kwa miaka mingi chini ya uenyekiti wa Mwalimu Julius Nyerere na baadaye Ali Hassan Mwinyi.

"Taifa hili linahitaji kuongozwa kwa umakini na watu makini. Taifa linahitaji umakini na busara ya hali ya juu. Tusikubali hata kidogo kuruhusu Kamati Kuu ya Chama hiki ibariki mchezo wa kununua uongozi. Si busara kwa Kamati Kuu kuwa chanzo cha kuruhusu watu kununua madaraka. Lazima kubadilisha mfumo. Tukiruhusu hali hii, masikini hawatakuwa na chao, hawatapata nafasi na sisi wengine tusio na fedha za kununua madaraka itabidi tuondoke humu.

"Inasikitisha watu wapo tayari humu ndani (Kamati Kuu) kutetea ununuzi wa madaraka. Mimi baba yangu (Mzee Moses Nnauye) amefanya kazi kwenye hiki chama kwa uaminifu mkubwa, kwa miaka mingi hadi anaondoka hakuwahi hata kuwa na nyumba, leo watu wananunua uongozi, wengine siku mbili tatu baada ya kupata madaraka ana nyumba nyingi," alisema Nape.

Baada ya Nape, alizungumza Zakhia Meghji ambaye kwa ukali aliwataka wajumbe wa Kamati Kuu kuheshimu uamuzi wa Kamati ya Usalama na Maadili akisema imeongozwa na Mwenyekiti Kikwete ambaye kwa nafasi yake ya Urais, anazo taarifa za kina kuhusu watangaza nia wote.

"Kamati Kuu lazima iwe na ujasiri. Mwenyekiti anazo taarifa zote tena za kina, kwa hiyo lazima wanazo sababu za msingi za kuleta humu majina matano," alisema Meghji kwa mujibu wa nukuu ya chanzo chetu cha habari kutoka kikaoni humo.

Rais msitaafu Benjamin Mkapa naye alizungumza kwa ukali akisema; "Tunapata wapi ujasiri wa namna hii wa kutetea maslahi binafsi? Naona hapa ni mtu kwanza chama baadaye, si chama kwanza mtu baadaye. "Hapa hakuna mwenye taarifa za kina kama Mwenyekiti. Ni nani huyo mwenye taarifa za kina kumshinda Mwenyekiti? Tuna imani na uamuzi wa Kamati ya Maadili".

Naye Mzee Mwinyi alisema; "Ni lazima tuheshimu kiti. Lazima muwe na uwezo wa kukubaliana na mambo yanavyokwenda. Nashangaa watu wapo tayari kukitishia chama, nguvu hizi za kukitisha chama mnazitoa wapi?"

Waziri Mkuu wa zamani, John Malecela, yeye alitoa mfano wake mwenyewe namna Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere alivyomwondoa kwenye kinyang'anyiro cha urais mwaka 1995.

"Lazima tuheshimu mamlaka, Mwenyekiti anazo taarifa nyingi. Mimi mwaka 1995 Mwalimu Nyerere alining'oa na akasema kama nitapewa nafasi CCM yeye ataondoka, anakwenda kuanzisha chama. Mimi nikanyoosha mikono na kujitoa, Mwalimu akanifuata na kunikumbatia," alisema Malecela ambaye alikuwa akisisitiza wajumbe wenzake wakubaliane na hali halisi.

Mzee Malecela ambaye alikuwa nje ya nchi kwa matibabu, alilazimika kutopumzika ili kuungana na wazee wenzake kuokoa jahazi lililoelekea kuzamishwa na nguvu ya fedha.

Rais msitaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, kama ilivyokuwa kwa wenzake, naye aliweka bayana kuunga mkono uamuzi wa Kamati ya Usalama na Maadili akisema ni uamuzi uliopaswa kuungwa mkono.

Baada ya jina lake kutofikishwa Kamati Kuu na baadaye kushindwa kuilazimisha jina lake lirudishwe NEC, wapambe wa Lowassa wanadaiwa kuandaa mpango wa kutaka kumsaidia Balozi Amina aweze kupitishwa kuwa mgombea wa urais wa CCM, ili naye baadaye amtangaze Lowassa kuwa Mgombea Mwenza na hatimaye aweze kuwa Makamu wa Rais.

Mkakati huo ulitiwa nguvu na Balozi Amina mwenyewe wakati akijieleza kuomba kura ambaye mara mbili alisema kwamba alikuwa tayari kufanya kazi na Lowassa.

Hata hivyo, habari zinasema mpango huo ulikuja kuvuja kutokana na papara za baadhi ya wapenzi wa Lowassa kuanza kampeni za wazi kwa ajili hiyo katika Mkutano Mkuu ili Balozi Amina ashinde kwa kura nyingi.

Kwa hisani ya RaiaMwema.
 
Kati ya wote hao ni nani msafi wa kumuhukumu mwenzie zaidi ya kulinda maslahi yao tu?

Aliyejiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kutupa anawezaje leo hii kuhoji ya Lowassa?

Alieshirikiana na Lowassa kwenye Richmond anaweza vipi leo hii kumtuhumu Lowassa?

Kashifa ya Richmond ilipozimwa kihuni Bungeni ni nani kati ya maraisi hao wastaafu na huyu aliepo madarakani leo hii alijitokeza hadharani kupinga na kukemea uamuzi huo batili wa Bunge?!

Aliehusika kumvua madaraka ya uwaziri Mrema kwasababu tu Mrema alijitoa kulinda maslahi ya Taifa anaweza vipi leo hii kuhoji ya Lowassa?

Watu(wastaafu) hawa waliokaa kimya na kujifanya viziwi kuhusiana na yaliyokuwa yanaendelea kuhusiana na Escrow,Richmond na EPA leo hii wamepata wapi uzalendo wa kututafutia kiongozi bora?1

Huu ni unafiki wa kiwango cha juu sana!!

wapo wanaowasifu na kuona ni watu safi kabisa... huwa inafikia hatua siwaelewi baadhi ya watu hususan baadhi ya waandishi habari wetu. wanakopewa husifia na kupigia kimya huku walikokosa wakipasiliba na kuzua uongo usio na kifani.
 
Kati ya wote hao ni nani msafi wa kumuhukumu mwenzie zaidi ya kulinda maslahi yao tu?

Aliyejiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei ya kutupa anawezaje leo hii kuhoji ya Lowassa?

Alieshirikiana na Lowassa kwenye Richmond anaweza vipi leo hii kumtuhumu Lowassa?

Kashifa ya Richmond ilipozimwa kihuni Bungeni ni nani kati ya maraisi hao wastaafu na huyu aliepo madarakani leo hii alijitokeza hadharani kupinga na kukemea uamuzi huo batili wa Bunge?!

Aliehusika kumvua madaraka ya uwaziri mh. Mrema eti kwa kile kilichoitwa kukiuka dhana ya "collective responsibility" wakati Mrema alijitoa kulinda maslahi ya Taifa anaweza vipi leo hii kuhoji ya Lowassa?

Watu(wastaafu) hawa waliokaa kimya na kujifanya viziwi kuhusiana na yaliyokuwa yanaendelea kuhusiana na Escrow,Richmond na EPA leo hii wamepata wapi uzalendo wa kututafutia kiongozi bora?1

Huu ni unafiki wa kiwango cha juu sana!!

Hawashindani nani kaiba sana Dada, hapa mantiki ni kuheshimu kiti. Wewe kama kwako utakuwa mama alafu unataka kila mtoto awe mwenyekiti basi utapata shida
 
Hawashindani nani kaiba sana Dada, hapa mantiki ni kuheshimu kiti. Wewe kama kwako utakuwa mama alafu unataka kila mtoto awe mwenyekiti basi utapata shida
Sorry,mimi sio dada

Back to the topic,jiheshimu utaheshimiwa na si vinginevyo.
 
Ndiyo upumbavu wao miaka nenda miaka rudi. Itakuwa poa sana kama huu unafiki wao wa safari hii utazua mpasuko mkubwa sana ndani ya chama chao cha wahuni na wa kulaumiwa pindi mpasuko huo ukitokea wanajulikana dhahiri. Waswahili walisema mficha ugonjwa kifo humuumbua.

Wanatufanya watanzania wajinga na hatuna kumbukumbuku.
 
Back
Top Bottom