ToniXrated
JF-Expert Member
- Sep 21, 2022
- 1,134
- 2,993
Amani iwe nanyi:
Natoa pole kwa vilabu vya Tanzania vilivyoumaliza mwendo katika mechi za awali za Mashindano ya Afrika ,nazungumzia Yanga,Azam na Kipanga.
Mara baada ya mechi za jana nilitulia kidogo kufanya tathmini kujua mapungufu ya vilabu vya Tanzania katika soka la Kimataifa, nikagundua tatizo kubwa linalotusumbua ni KASI, jinsi gani tunautembeza au kuukimbiza mpira uwanjani. Ama kwa hakika tupo (very slow) taratibu sana.
Timu za waarabu huwa zinazitesa sana timu za Tanzania kutokana na kucheza mpira wa kasi.Nimekuwa na nitaendelea kuwa muumini wa soka la kasi kwani ndio soka la nchi zilizopo ulimwengu wa kwanza kisoka.
Katika hii mechi ya Al-Akhdar dhidi ya Azam tutakuwa tumejifunza kitu kuwa wenzetu wa Afrika ya kaskazini ambao wamepakana na mataifa ya ulaya kwa kutenganishwa na bahari ya mediterrenia wamefanikiwa sana kupata chembechembe za soka la ulaya.
Kwa jinsi ya hawa Al-akhdar walivyokuwa wakicheza kwa kasi unaweza kujiuliza imekuwaje wakacheza kombe la shirikisho badala ya klabu bingwa Afrika!?
Kama Al-akhdar alimaliza ligi ya nchini Libya akiwa nafasi ya tatu ,vipi hao vinara wa nafasi ya kwanza na ya pili?!
Soka letu limebarikiwa kuwa na wachezaji ambao wana individual skills ila linapokuja suala la kasi uwanjani ,naweza kusema kwa kjnywa kipana kuwa wapo chini sana!! Work rate ya wachezaji wetu wa ligi kuu ya Tanzania ipo chini sana. Wachezaji wa Al akhdar muda wote walikuwa katika movements iwe wana mpira au hawana mpira na hivi ndivyo soka la kisasa linahitaji mchezaji awe.
Ni rahisi sana kwa wachezaji kutoka mataifa ya Afrika ya kaskazini kwenda kucheza mpira katika ligi za ulaya ,kutokana wana kasi. Mpira wa kisasa hauhitaji mambo mengi sana uwanjani. Ukiweza kucheza basic football na ukiwa na kasi basi unaweza kucheza ulaya bila ya tabu.
Wachezaji wetu huonesha movements wakiwa na mpira tu tena ni kwa baadhi , ni jambo la kawaida kuona timu inashambulia huku wachezaji wa safu ya kiungo wakiwa wapo nyuma wanatembea badala ya kukimbia. Wanapokuwa hawana mpira ndio tatizo kabisa maana huoni kujituma wala kukimbia kuhakikisha kuwa wanaumiliki mpira ama kuziba mianya .Badala yake wanatembea tu huku wakiruhusu timu pinzani ziongeze presha golini kwao.
Kama tunahitaji kufika mbali kimataifa ni lazima tubadili mfumo wetu wa uchezaji. Na kama inawezekana basi wachezaji wavishwe vifaa ambavyo vitakuwa vikionesha ni kwa umbali gani wamekimbia uwanjani , hii itawasaidia makocha katika kubadili taswira nzima ya mpira wetu.
Wenzetu huko ulaya na afrika kaskazini kwa wastani mchezaji anatakiwa akimbie sio chini ya umbali wa kilometa 9-12 kwa dakika 90 awapo uwanjani. Na viungo wa kati ndio wanaotakiwa wakimbie zaidi kuliko wachezaji wa nafasi yeyote kiwanjani.
Sasa si ajabu kuja kukuta kuwa wachezaji wetu wanakimbia umbali chini ya kilometa 4 wawapo kiwanjani ktk kipindi cha dakika 90.
Natoa pole kwa vilabu vya Tanzania vilivyoumaliza mwendo katika mechi za awali za Mashindano ya Afrika ,nazungumzia Yanga,Azam na Kipanga.
Mara baada ya mechi za jana nilitulia kidogo kufanya tathmini kujua mapungufu ya vilabu vya Tanzania katika soka la Kimataifa, nikagundua tatizo kubwa linalotusumbua ni KASI, jinsi gani tunautembeza au kuukimbiza mpira uwanjani. Ama kwa hakika tupo (very slow) taratibu sana.
Timu za waarabu huwa zinazitesa sana timu za Tanzania kutokana na kucheza mpira wa kasi.Nimekuwa na nitaendelea kuwa muumini wa soka la kasi kwani ndio soka la nchi zilizopo ulimwengu wa kwanza kisoka.
Katika hii mechi ya Al-Akhdar dhidi ya Azam tutakuwa tumejifunza kitu kuwa wenzetu wa Afrika ya kaskazini ambao wamepakana na mataifa ya ulaya kwa kutenganishwa na bahari ya mediterrenia wamefanikiwa sana kupata chembechembe za soka la ulaya.
Kwa jinsi ya hawa Al-akhdar walivyokuwa wakicheza kwa kasi unaweza kujiuliza imekuwaje wakacheza kombe la shirikisho badala ya klabu bingwa Afrika!?
Kama Al-akhdar alimaliza ligi ya nchini Libya akiwa nafasi ya tatu ,vipi hao vinara wa nafasi ya kwanza na ya pili?!
Soka letu limebarikiwa kuwa na wachezaji ambao wana individual skills ila linapokuja suala la kasi uwanjani ,naweza kusema kwa kjnywa kipana kuwa wapo chini sana!! Work rate ya wachezaji wetu wa ligi kuu ya Tanzania ipo chini sana. Wachezaji wa Al akhdar muda wote walikuwa katika movements iwe wana mpira au hawana mpira na hivi ndivyo soka la kisasa linahitaji mchezaji awe.
Ni rahisi sana kwa wachezaji kutoka mataifa ya Afrika ya kaskazini kwenda kucheza mpira katika ligi za ulaya ,kutokana wana kasi. Mpira wa kisasa hauhitaji mambo mengi sana uwanjani. Ukiweza kucheza basic football na ukiwa na kasi basi unaweza kucheza ulaya bila ya tabu.
Wachezaji wetu huonesha movements wakiwa na mpira tu tena ni kwa baadhi , ni jambo la kawaida kuona timu inashambulia huku wachezaji wa safu ya kiungo wakiwa wapo nyuma wanatembea badala ya kukimbia. Wanapokuwa hawana mpira ndio tatizo kabisa maana huoni kujituma wala kukimbia kuhakikisha kuwa wanaumiliki mpira ama kuziba mianya .Badala yake wanatembea tu huku wakiruhusu timu pinzani ziongeze presha golini kwao.
Kama tunahitaji kufika mbali kimataifa ni lazima tubadili mfumo wetu wa uchezaji. Na kama inawezekana basi wachezaji wavishwe vifaa ambavyo vitakuwa vikionesha ni kwa umbali gani wamekimbia uwanjani , hii itawasaidia makocha katika kubadili taswira nzima ya mpira wetu.
Wenzetu huko ulaya na afrika kaskazini kwa wastani mchezaji anatakiwa akimbie sio chini ya umbali wa kilometa 9-12 kwa dakika 90 awapo uwanjani. Na viungo wa kati ndio wanaotakiwa wakimbie zaidi kuliko wachezaji wa nafasi yeyote kiwanjani.
Sasa si ajabu kuja kukuta kuwa wachezaji wetu wanakimbia umbali chini ya kilometa 4 wawapo kiwanjani ktk kipindi cha dakika 90.