Jinsi kanisa lilivyovunja ndoa ya binamu yangu na kumfuja mali za talaka, wanawake wanaoabudu manabii wa mchongo wamechotwa akili huwaambii kitu

Jinsi kanisa lilivyovunja ndoa ya binamu yangu na kumfuja mali za talaka, wanawake wanaoabudu manabii wa mchongo wamechotwa akili huwaambii kitu

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Ni kisa cha miaka 10 iliyopita lakini mhusika anapitia kipindi kigumu mpaka sasa

Ilifikia kipindi anashinda sana kanisani mpaka anaacha watoto nyumbani, hapiki analipa kanisa kipaumbele, kuchukua pesa za savings kwajili ya zaka na sadaka za kitapeli, anaweza kesha kanisani, n.k. Mume wake alimuacha na yeye alikuwa brainwashed kwamba ni sawa tu kulipa kanisa kipaumbele akajazwa maneno mme ni pepo.

Baada ya ndoa kuvunjika kukawa na mgao, Aliambulia nyumba moja ndogo na mali kadhaa zenye thamani ya milioni 10 hivi, alizidiwa akili kizembe akaanza kupeleka mafungu ya sadaka na misaada huko kanisani, ndani ya miaka miwili hana mbele wala nyuma imebidi ajenge duka dogo pale nyumbani kwake, sidhani kama anaingiza faida zaidi ya elf 5 kwa siku maana imekuwa ni kawaida baadhi ya siku nyumba yake pekee ipo gizani wakati majirani kuna umeme.

Akili zimekuja kumfunguka mwishoni kabisa kwamba wachungaji wake ni matapeli.

Pia soma:Hofu ya kuongezewa mke mwenza, wepesi wa kutoa talaka na kuachana bila kugawana mali inachangia wanawake waislam kuwa na adabu kuzidi wakristo?
 
Ni kisa cha miaka 10 iliyopita lakini mhusika anapitia kipindi kigumu mpaka sasa

Ilifikia kipindi anashinda sana kanisani mpaka anaacha watoto nyumbani, hapiki analipa kanisa kipaumbele, kuchukua pesa za savings kwajili ya zaka na sadaka za kitapeli, anaweza kesha kanisani, n.k. Mume wake alimuacha na yeye alikuwa brainwashed kwamba ni sawa tu kulipa kanisa kipaumbele akajazwa maneno mme ni pepo.

Baada ya ndoa kuvunjika kukawa na mgao, Aliambulia nyumba moja ndogo na mali kadhaa zenye thamani ya milioni 10 hivi, alizidiwa akili kizembe akaanza kupeleka mafungu ya sadaka na misaada huko kanisani, ndani ya miaka miwili hana mbele wala nyuma imebidi ajenge duka dogo pale nyumbani kwake, sidhani kama anaingiza faida zaidi ya elf 5 kwa siku maana imekuwa ni kawaida baadhi ya siku nyumba yake pekee ipo gizani wakati majirani kuna umeme.

Akili zimekuja kumfunguka mwishoni kabisa kwamba wachungaji wake ni matapeli.
Akina Mwamposi hawana huruma kabisa kwa mtu mjinga.
 

Attachments

  • 5809407-b5f938c1728b0c773ef86cb6f9fbd76b.mp4
    9.8 MB
Ni kisa cha miaka 10 iliyopita lakini mhusika anapitia kipindi kigumu mpaka sasa

Ilifikia kipindi anashinda sana kanisani mpaka anaacha watoto nyumbani, hapiki analipa kanisa kipaumbele, kuchukua pesa za savings kwajili ya zaka na sadaka za kitapeli, anaweza kesha kanisani, n.k. Mume wake alimuacha na yeye alikuwa brainwashed kwamba ni sawa tu kulipa kanisa kipaumbele akajazwa maneno mme ni pepo.

Baada ya ndoa kuvunjika kukawa na mgao, Aliambulia nyumba moja ndogo na mali kadhaa zenye thamani ya milioni 10 hivi, alizidiwa akili kizembe akaanza kupeleka mafungu ya sadaka na misaada huko kanisani, ndani ya miaka miwili hana mbele wala nyuma imebidi ajenge duka dogo pale nyumbani kwake, sidhani kama anaingiza faida zaidi ya elf 5 kwa siku maana imekuwa ni kawaida baadhi ya siku nyumba yake pekee ipo gizani wakati majirani kuna umeme.

Akili zimekuja kumfunguka mwishoni kabisa kwamba wachungaji wake ni matapeli.

Pia soma:Hofu ya kuongezewa mke mwenza, wepesi wa kutoa talaka na kuachana bila kugawana mali inachangia wanawake waislam kuwa na adabu kuzidi wakristo?
Akili zimekuja kumfunguka mwishoni kabisa kwamba wachungaji wake ni matapeli.
 
Sasa mbona sijaina namna kanisa lilivyovunja hiyo ndoa? Mmekuwa na mmeingia kwenye mfumo wa kulichafua kanisa bila sababu.

Elezea namna gani kanisa limevunja ndoa yake na namna lilivyomfirisi.
 
  • Thanks
Reactions: I M
Akina Mwamposi hawana huruma kabisa kwa mtu mjinga.
Mkuu hili tatizo linatakiwa kuangaliwa kwa makini sana. Victims wanakuwa wamekuwa brainwashed kiasi cha kutojitambua. Mimi nashauri mtu mwenye mwenza au ndugu ambaye ni victim wa hawa ''mitume'' asidharau na kusema ni ''shauri yake''. Tujitahidi kuwaondoa kwenye haya matatizo kwani wanakuwa wameingia kwenye hali ya ukichaa na kichaa siku zote anataka msaada. Najua ni ngumu sana kuwakomboa watu wa aina hiyo ila ikiwezekana deal na huyo mtume fake moja kwa moja. Kuna ile kanuni inayosema tapeli anatakiwa kushughulikiwa nje ya mifumo ya sheria, ikiwezekana apply hii kanuni na mshikishe adabu huyo ''mtume''.
 
Akina Mwamposi hawana huruma kabisa kwa mtu mjinga.
Sio mwamposa tu, makanisa na dini yote ni utapeli. Mungu hayupo n wala hajawahi kuwepo

Dini inavyopumbaza watu, ni mkatoliki kuona muumini wa mwamposa anaibiwa na muumini wa mwamposa kuona mkatoliki anaibiwa, yaani wote wamepumbazwa kuona kwamba mwenzie ndie anaeibiwa ila sio yeye ingawa uhalisia ni kwamba wote wanaibiwa, huyu anaibiwa na mwamposa na huyu anaibiwa na papa Francis nk nk.

Dini ni utapeli mkubwa kuwahi kutokea Duniani.
 
Mkuu hili tatizo linatakiwa kuangaliwa kwa makini sana. Victims wanakuwa wamekuwa brainwashed kiasi cha kutojitambua. Mimi nashauri mtu mwenye mwenza au ndugu ambaye ni victim wa hawa ''mitume'' asidharau na kusema ni ''shauri yake''. Tujitahidi kuwaondoa kwenye haya matatizo kwani wanakuwa wameingia kwenye hali ya ukichaa na kichaa siku zote anataka msaada. Najua ni ngumu sana kuwakomboa watu wa aina hiyo ila ikiwezekana deal na huyo mtume fake moja kwa moja. Kuna ile kanuni inayosema tapeli anatakiwa kushughulikiwa nje ya mifumo ya sheria, ikiwezekana apply hii kanuni na mshikishe adabu huyo ''mtume''.
Uko sahihi. Anko wangu alienda na panga kanisani na kumchomoa mkewe katikati ya ibada za hawa matapeli.
 
Kanisa limevunja sababu ya huyo kiongozi wa kanisa kusababisha mgogoro wa huyo dada na mumewe, hata ingekua shehe wa msikiti amefanya hayo aliyofanya tungesema msikiti umevunja ndoa kwasababu kanisa/msikiti unawakilishwa na hao viongozi
Sasa kanisa limevunjaje hapo mkuu? Mbona uelewa wako ni finyu sana we dogo?

Mfano shehe akibaka msikiti au waislam ndio wamebaka? Je Padri akilawiti kanisa ndio limelawiti? Mwalimu mkuu akiiba shule ndio imeiba? Baba yako akifumaniwa, nyumba yenu ndio imefumaniwa? Kwa umri wako hadi upo JF unashindwa kutofautisha kati ya mtu binafsi na taasisi?

Haya hongera kwa kucomment 👋👋👋 maana naona najadiliana na mwehu.
 
Wajanja wamegundua watu ni wepesi kuaminiamini tu. Ndio maana wanabuni namna ya kuonesha miujiza. Mtu kafufuliwa, mtu kapona, shuhuda mbalimbali za utajiri nk.

Pia wamegundua wanawake ni wepesi kukamatika, kiasi ya kwamba yupo tayari kuvunja ndoa lakini muda mwingi awe kanisani au mali zote apeleke huko.

Wanaume tuwe makini katika mtego huu. Yule mwamba aliye mchomoa mkewe ndani ya kanisa akiwa na panga ana stahili tuzo.

Mambo ya kusema mke atajijua mwenyewe kila mtu atahukumiwa mwenyewe hayapo. Kabla na wakati wa kufunga ndoa, waliridhika na imani walizo nazo. Bila shaka wasinge ridhika wasinge oana. Inakuwaje iwe ni sawa mmoja wao achepuke peke yake halafu iwe ni sawa.

Na hao wanao sajili waumini wana ndoa wapya katika madhehebu yao wasisajili majina tu, wajiridhishe mtu katoka wapi na vipi ana mwenza aliyeridhia. Isiwe kama mteja na duka.

Namna nyingine mtu akigundua mke anapewa jeuri huko kanisani akichukua hatua za kumrudisha mtekwaji wake atakuwa sahihi.

Maana mimi muoaji najua nilivyo mpata mke wangu, huenda niliwekeza kwelikweli au nilosotea, halafu waje watu janjajanja wamlaghai, vumbi lazima litimke.
 
Sasa kanisa limevunjaje hapo mkuu? Mbona uelewa wako ni finyu sana we dogo?

Mfano shehe akibaka msikiti au waislam ndio wamebaka? Je Padri akilawiti kanisa ndio limelawiti? Mwalimu mkuu akiiba shule ndio imeiba? Baba yako akifumaniwa, nyumba yenu ndio imefumaniwa? Kwa umri wako hadi upo JF unashindwa kutofautisha kati ya mtu binafsi na taasisi?

Haya hongera kwa kucomment 👋👋👋 maana naona najadiliana na mwehu.
Achana kubishana na hizo mbuzi mkuu, zinakaza mafuvu tu. At least angesema mchungaji alivyovunja ndoa angeeleweka, ila kutumia neno kanisa ni mshamba mmoja tu achana naye, ujue kanisa linahusisha na waumini kwa pamoja!
 
Sio mwamposa tu, makanisa na dini yote ni utapeli. Mungu hayupo n wala hajawahi kuwepo

Dini inavyopumbaza watu, ni mkatoliki kuona muumini wa mwamposa anaibiwa na muumini wa mwamposa kuona mkatoliki anaibiwa, yaani wote wamepumbazwa kuona kwamba mwenzie ndie anaeibiwa ila sio yeye ingawa uhalisia ni kwamba wote wanaibiwa, huyu anaibiwa na mwamposa na huyu anaibiwa na papa Francis nk nk.

Dini ni utapeli mkubwa kuwahi kutokea Duniani.
We acha bla bla Wakatoliki hawana wizi
 
Wajanja wamegundua watu ni wepesi kuaminiamini tu. Ndio maana wanabuni namna ya kuonesha miujiza. Mtu kafufuliwa, mtu kapona, shuhuda mbalimbali za utajiri nk.
Hiwezi amini kwamba Kaniaa kwa Buza wa Lulenge alikuwa anatoa Miujiza ya uongo redioni na kwenye tv.
 
Back
Top Bottom