Jinsi kuchelewa kwa matokeo ya TRA kunavyochelewesha utumishi kuita interview kwa fani za uhasibu na Manunuzi kwa MDAs na LGAs

NEWSINKP

Member
Joined
Sep 26, 2016
Posts
77
Reaction score
92
Habari wana JF!
Kama mnakumbuka mwezi July 2023 utumishi walitoa nafasi za ajira kwa kada mbalimbali zikiwemo za uhasibu na manunuzi kwa MDAs na LGAs. Mwezi huu tarehe 4 kuna kada waliitwa interview isipokua uhasibu na manunuzi, na sababu inasemekana wanasubiri TRA wamalize mchakato ili candidates wasije pata ajira utumishi na TRA kwa wakati mmoja.

Hivyo utumishi wanasubiri mpaka TRA wamalize mchakato ndipo waite watu kwa ajili ya written interview. Kwa hyo TRA kuchelewa ni athari kubwa mno kwa michakato mingine.
Nawasilisha.
 
Kama ni ndio mambo yapo namna hiyo basi si itakuwa changamoto kubwa kwa wale ambao hawa husiki na usaili wa TRA kusubiria muda mrefu kwa jambo lisilo wahusu, au ilikuwa na ulazima gani wao kuajiri wenyewe kama utaratibu ni mpaka wao wamalize shuhuli zao then ndipo taasisi nyingine ziendelee na shuhuli za kuajiri watu ili kupisha msongamano usio kuwa wa ulazima..[emoji847]
 
MDAs- Ministries and Independent Departments Authorities.
LGAs- Local Government Authorities.
 
Hili ni sahihi kabisa, TRA in short mchakato wa ajira hawauwezi ni bora warudishe utumishi
 
Wewe umetolea wapi hizi habari?
Kwani mbona watu huwa wanafanya interview mbili hadi tatu at once hapo utumishi, kisha mtu anapata post mbili na zaidi?
 
Wewe umetolea wapi hizi habari?
Kwani mbona watu huwa wanafanya interview mbili hadi tatu at once hapo utumishi, kisha mtu anapata post mbili na zaidi?
Sasa ndugu yangu kila siku taasisi zinaboresha. Hata kwa ufahamu wako tuu huoni kwamba mtu mmoja kuchaguliwa posts zaidi ya moja tena zote serikalini ni lack of seriousness na pia ni matumizi mabaya ya fedha za umma kuendesha usahili hovyo hovyo kiasi hicho. Na Rais aliwahi kusema mifumo ya serikali isomane, kusomana maana yake ndo kama hii
 
Hahahaa bro ni vizuri sana kama ungeiweka sawa coz kuna mtu alitaka kujua. Ila hicho nlichokiandika ndo sahihi kasome Public Procurement utaikuta.
Labda lina maana zaidi ya moja
 
Nimeangalia andiko hili ila ninachokiona tatizo siyo kuwa ajira imetoka wapi au nani angeajiri. Shida ninayoiona ni walioomba nafasi tra ni wengi sana. Hivo inaonyesha kabisa mchujo ndiyo unaendelea fanyika maana nafasi zilizotoka na walioomba ni tofauti kubwa waombaji ni wengi. Tusiwalaumu sana watoza kodi hofu wakitoa haraka inaweza sababisha kuchukua wasio na sifa. Mimi kuomba tu niliona shida nikaamua niendelee na vibiashara vyangu maana si kwa nyomi lile.Labda tuwaombe ndugu zeetu tra wajitahidi ili kuepuka shutuma
 
naona tangazo limetoka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…