utam wa upadre uliisha pale maaskofu walipoanza kubana mafrater na mapdre kuwa na wafadhiri wa nje. pia ruzuku ya jimbo kuminywa, padre anaishi kwa uchumi wa parokia aliyopo. hakuna asiyependa kula bata hata kama kwa modes tofaut dunian. au kusaidia ndugu na wazaz. sasa unasoma miaka kibao unaishia maisha magum. tusisahau ukisomea sana dini na makando kando yake sana unaelewa kuwa mambo mengi dunian hayako kama yanavyosadikishwa! furaha ndo tunu pekee Mungu katupatia. ukiikosa manake kusudio la uhai kwako halipo. hata sifa pekee ya kuwa na uelewa wa kipekee ukipitia seminarin kama kujua kiingereza fasaha na kuishi responsibly ( kwa utaratib) imemezwa na shule za kisasa zenye mitaala bora zaid. ndo maana seminary zinapigwa chini matokeo vidato siku hizi. pia tusisahau utandawazi na kupungua kwa ushawishi wa dini dunian( sabab Mungu ameshindwa kujidhihiri kumpambania mwanadam kimiujiza kwa dhiki na tabu hizi kias kwamba majibu ya kisayansi yanaonekana ya uhakika zaid kutatua). kwa hali ya mapadre ilivyo leo na mienenndo yao walio wengi, kanisa katoliki linaelekea kudhalilika sana na zaidi labda waziangalie upya sheria na kanuni za ukasisi hasa kuoa. siku hizi shetan afsa mwandamizi wa ngono kahamishia majukum yake kwa kanisa na viongoz wake. au bas utandawaz umepevuka kuwaweka hadharan mambo yao ya siri.