Mzuka wanajamvi!
Ukiitwa kwenye fursa juwa wee mwenyewe ndio fursa.
"Bado naendesha Ferrari yangu na baadhi yenu hamuwezi hata kununua chakula." Iyo ndio ilikuwa ujumbe wa mwisho wa mwanzilishi wa Crypto currency alivyoandika kwenye group la telegram baada ya kuwatapeli shilingi billion moja za Kenya sawa na dollars million 10.
Bitstream Circle iliyoanzishwa na tapeli mkenya na mchina ilianza kuleta sintofaham ambapo wawekezaji walikuwa wengi wakenya kila wakijaribu kutoa hela zao ilikuwa ikicheleweshwa.
Kampuni iyo ya Bitstream Circle iliyoahidi wawekezaji watakaowekeza hela zao kwenye crypto currency watapata faida asilimia 10 hadi 15 kwa siku. Na ilianza kuonekana mtandaoni kwaanzia December 7 2021.
Iliweza kupata followers elfu 10 kwa muda mfupi kwenye telegram page. Na waliojiunga wakatakiwa kuwekeza kwaanzia dolla 20.
Kila kitu kilienda vizuri hadi march 13 mwaka huu ambapo users walianza kuona ucheleweshaji walipotaka kutoa hela zao.
Hao matapeli walipoulizwa shida ipo wapi wakawa wanadanganya wanaupgrade system. Na kuupgrade system ilikuwsa ikichukua Zaid ya masaa matano.
Ilipofika March 14 habari mbaya ikawafikia wawekezaji. Ujumbe wa matusi dhihaka na kejeli wakatumiwa wawekezaji. Yani hii iliniuma sana. Unatapeli watu na kuwatukana.
“You are a bunch of brainless races, see you on our next plan,” an administrator of the page posted to the 10,914 investors.
“Bye, haha. I am living a luxurious life with your dollars. If you have invited friends, wait to be killed by your recommenders. Idiots. There will be a time to meet.”
Soma zaidi kwa kiingereza kwenye page ya kwanza.
Source dailynation