Jinsi nilivyofanikiwa kutengeneza Sh. Milioni 19.9 ndani ya siku 35 kwa kutumia Milioni 3.8

Jinsi nilivyofanikiwa kutengeneza Sh. Milioni 19.9 ndani ya siku 35 kwa kutumia Milioni 3.8

uzi safi sana, umekaa ki JF na unajenga ukakamavu ktk kutafuta maisha. asante kwa kuutupia hapa.
 
Safi sana kaka,
Nimejifunza mengi mnoo
1. Kujiamini kwa kila unachotaka kukifanya
2. Kujituma na kufanya kazi kwa moyo
3. Utii na juhudi katika kazi
4. Elimu si kitu,mchongo ni kutafuta fursa na kuangalia namna gani zitakupa pesa.
5. Kumpenda anayekutumikia,kutamfanya afanye kazi kwa moyo na faida inakuwa kwako, "ukila na kipofu usimshike mkono"
6. Kuwa tayari kufanya kazi katka mazingira yeyote yale, yakini kuna maslahi au laa,ipo siku utafanikiwa.
7. Hakuna uchawi wala uganga katika kazi,ni umakini tu katka kazi ndio unahtajika.
AHSANTE KAKA ONTORIO.
 
Safi sana kiongozi - hongera kwa uthubutu. Ni vizuri tukaonyeshana dira, muda wa kuwa 'financial independent' ndio huu. Vijana wanashinda kumtukana Bashite as if uwepo wa bashite unawaondolea ugali mezani. Period!!!
Mengine yote nipo na wewe Sana tu, Tatizo ni kwenye avatar yako tu, tafuta avatar inayojitambua, ktk ulimwengu wa roho, hiyo avatar ndo inabeba nafsi yako, Kama umemwogopa siro hadi hutaki pm na wakati huna kosa lolote ulilotenda, sasa hiyo avatar unaipendaje?
Nakutabiria kufilisika endapo hutaitoa hiyo avatar Yako.
 
Wabongo hua n rahisi sana kuhamasika ila tukipigwa na ugumu na shuruba kidogo tu tunarun away
 
mkuu ONTARIO ni kweli kwenye hiyo shughuli kuna mambo mengi ya kishirikina, nilishaifanya hiyo kazi ila nikakimbizwa na hayo mambo...ilifika mahali dereva anavimba miguu walipoona bado wabishi wakaliloga na trekta lenyewe likawa haliwaki, nikapoteza pesa nyingi sana kwenye matengenezo lakini haliponi wenyeji wakatuambia tuligeuze kama tunaondoka litawaka, tukafanya hivo likawaka...wakatuambia huo uchawi upo common sana huko mashambani....

umebahatika kupata client wasio na hizo mambo so mshukuru Mungu, ila hao watu ni wasumbufu mno. mtu akikuita mswahili aisee pigana....ni watu wa husda na wivu wa kiwango cha lami.

ila all in all big up sana na mshukuru sana Mungu kwa hayo mafanikio sio kila mtu anafanikiwa, God has a plan for you.
 
mkuu ONTARIO ni kweli kwenye hiyo shughuli kuna mambo mengi ya kishirikina, nilishaifanya hiyo kazi ila nikakimbizwa na hayo mambo...ilifika mahali dereva anavimba miguu walipoona bado wabishi wakaliloga na trekta lenyewe likawa haliwaki, nikapoteza pesa nyingi sana kwenye matengenezo lakini haliponi wenyeji wakatuambia tuligeuze kama tunaondoka litawaka, tukafanya hivo likawaka...wakatuambia huo uchawi upo common sana huko mashambani....

umebahatika kupata client wasio na hizo mambo so mshukuru Mungu, ila hao watu ni wasumbufu mno. mtu akikuita mswahili aisee pigana....ni watu wa husda na wivu wa kiwango cha lami.

ila all in all big up sana na mshukuru sana Mungu kwa hayo mafanikio sio kila mtu anafanikiwa, God has a plan for you.
Ni kweli inabidi ashukuru tu mungu........siyo rahisi kama Ontario anavyoeleza.....Hata mimi naamini sana Mungu lakini yaliyonikutaga katika maisha yangu ya kuhangaika zaidi ya miaka ishirini duh nilipiga saluti malimwengu.....Wote tunaamini mungu ila hata biblia inatambua uwepo wa ulimwengu wa giza....kama hayajakukuta huwezi elewa....
 
Ukiwa unasoma na kusikiliza hizi stori za waliofanikiwa kwenye kilimo utatamani hata kesho uende shamba.

Kwa mleta mada alivyoelezea unaweza ukajidharau kwa nini umechelewa kuwa tajiri.

Kwa kifupi kilimo sio virahisi hivyo kama tunavyoaminishwa. Ndio maana watu wengine wakiingia shamba msimu wa kwanza tu anakimbia huku akilia kutokana na faida alizopigiwa kwenye daftari kabla hajakanyaga shamba.

Ingekuwa ukiwa na trekta ndio unatengeza faida kiasi hicho kwa mwezi mmoja kuna watu wangekuwa na pesa sana.

Kuna jamaa nipo nao wanamiliki trekta mbili wengine hadi nne, lakini hawatengenezi kiasi hicho cha pesa sio tu kwa mwezi hadi hata mwaka kwa kupitia kulima tu mashamba ya watu.
 
Afterthought 1:

Niwe tu muwazi - sijibu PM yoyote ile, I mean YOYOTE. Sitoi mawasiliano ya aina yoyote ile, PM kumejaa uhuni, utapeli na kujikamatisha kwa kamansa Xirro.

Maswali yote najibu hapa, maelezo yote nafafanua hapo. Kila mtu ajifunze, wote tugawane darasa huru. Wote tupanuane fikra.
Du. Umenigonga sana akili yangu. Hongera sana sana
 
Dah!!! Kama hata na mie nshaanza kumfahamu huyu jamaa kuna article kuhusu yeye pia nilishawahigi kusoma kwenye gazeti fulani. Inahusiana na issue hiyo hiyo ya Kuku... Hongera sana Ontario
Naaam,jamaa ana guts and audacity..ambayo ni key to success popote duniani..
 
Ukiwa unasoma na kusikiliza hizi stori za waliofanikiwa kwenye kilimo utatamani hata kesho uende shamba.

Kwa mleta mada alivyoelezea unaweza ukajidharau kwa nini umechelewa kuwa tajiri.

Kwa kifupi kilimo sio virahisi hivyo kama tunavyoaminishwa. Ndio maana watu wengine wakiingia shamba msimu wa kwanza tu anakimbia huku akilia kutokana na faida alizopigiwa kwenye daftari kabla hajakanyaga shamba.

Ingekuwa ukiwa na trekta ndio unatengeza faida kiasi hicho kwa mwezi mmoja kuna watu wangekuwa na pesa sana.

Kuna jamaa nipo nao wanamiliki trekta mbili wengine hadi nne, lakini hawatengenezi kiasi hicho cha pesa sio tu kwa mwezi hadi hata mwaka kwa kupitia kulima tu mashamba ya watu.
ni kweli Ontario ni motivation speaker mzuri sana inaonekana kuna NGO anafanya kazi inayojihusisha na mambo ya kuwa motivate na kuinspire watu mbali mbali shunguli za kilimo..story yake iko kinadharia sana kuliko ukweli halisi ulioko shambani........kutengeneza hizo faida ndani ya siku 35 ni jambo ambalo halipo kiuhalisia....kilimo nakijua sana na wenye matrekta nawajua wengi hawajawahi kutengeneza hiyo faida kwa muda mfupi hivyo....wakulima wengi wa kijijini ni masikini hawategemei sana kulimiwa na matrekta lada jembe la Plau na wenye mashamba makubwa wana wengi wana matrekta yao .
 
Back
Top Bottom