Jinsi nilivyoibiwa gari kizembe bar

Jinsi nilivyoibiwa gari kizembe bar

Ila kuna jamaa hapa jirani kwangu aliibiwa 2017,kapiga tungi wakati wa kurudi home akapaki pembeni kwenda kukojoa ,kurudi ndani ya gari mambo yamemzidi akapiga usingizi hata milango ipo wazi ,wakaja wahuni wakamsukuma tu nje wakawasha gari Harrier ikaenda kirahisi hadi leo hajapata
 
Maisha ya mwanadamu yamejaliwa nankumbukumbu nyingi sana, nyingi na mbaya, zenye kutufundisha na zenye kuburudisha. Al mradi ni matukio yalitokea na yakapita.

Nakumbuka mwaka 2018, tarehe kama ya leo, na mwezi huu huu, nikiwa na gari ndio lina siku nne tu tangu lipite pale gati namba mbili na kutua mikononi mwangu, mzee nikajitoma nalo Bar, Maryland Mwenge.

Kilichonipeleka hapo bar, niweze kukutana na mrembo mantashahu, chotara wa Kigiriki na Kichaga, mtoto mwenye urefu wake wa futi tano point kumi na moja, chuchu mkuki, viwango vya kimataifa.

Kabla sijafika Maryland nilikuwa Break Point ya mjini, kisha nikaingia The Governors Kinondoni, lakini cha kustaajabisha nilikuwa nikikutana na sura zilezile.

Nilipofika Mwenge nikampigia bibie kwamba niko ndani ya nyumba namsubiri yeye ili tuanze safari ya kwenda Morogoro kula raha za dunia.

Kabla hajafika, wakaingia jamaa ambao nimekuwa nikiwaona tangu Break Point, na The Governors.

Moja kwa moja wakaja kwangu, mmoja akatoa bastola na kuniwekea kidevuni, wakati ubaridi wa mtutu wa bastola ukikikera kidevu changu, mara nikaona mwingine naye anatoa bastola yake na kupiga risasi tatu hewani, wakasema niwape funguo ya gari.

Nikawapa funguo, wakaondoka huku wakipiga risasi hewani kuwatisha watu wasiwafuate.

Nikabaki hapo bar nimepigwa na bumbuwazi. Nikawapigia simu rafiki zangu mapolisi akiwemo Mentor wa JamiiForums.

Jitihada za kulisaka gari zikaanza mara moja. Mimi na ubwege wangu nikaendelea kubung'aa pale Maryland kama kada wa CCM aliyekosa wali maharage wa kampeni.

Hazikufika dakika kumi, jamaa (majambazi) wakarudi tena na kunikuta pale, wakanibebamsobemsobe hadi kwenye gari yao, wakanitupia humo na wakatoa gari mbio huku wakiendesha kuelekea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Tulipofika maeneo ya Udasa tukakuta gari imezimika, na haiwezi kuwaka mpaka uweze kugusa sehemu fulani.

Ilikuwa kila ikipiga kengele watakiwa kugusa sehemu hiyo. Basi wakaniambia niwaonyeshe sehemuya kugusa ili gari isizime.

Nikapagusa nikawaambia wawashe,wakaiwasha, wakanissukumia huko chini wakatoka nduki na kuniacha kwenye viwanja vya chuo.

Nilitoka nduki hadi nilipopata daladala la kwenda Makumbusho nikapanda huku nikitweta, nikarudi nyumbani Kijitonyama.

Usiku mida ya saa tatu nikapigiwa simu kuwa gari yangu imepatikana mitaa ya Kimara Baruti ilizimika barabarani.

Kile kitufe kilikuwa kina sense fingerprint walishindwa kuendelea kuliendesha gari lile na hawakuwa na sehemu nyingine ya kunipata.

Tangu siku hiyo nikajifunza kwamba sitakiwi kuonana na mtu mara mbili sehemu mbili tofauti.

Pia nikajifunza nikipatwa na jambo lolote ni lazima nihame eneo la tukio.

Kingine nilichojifunza ni umuhimu wa mifumo ya usalama kwenye gari, gps for vehicle tracking nk.

Pia nilijifunza umuhimu wa kuwa na bima kubwa kwa chombo chako.

Hiyo ndiyo kumbukizi yangu ya alhamis ya leo
sasa mm niliibiwa simu na pesa kwa mtindo uo uo
 
Ila kuna jamaa hapa jirani kwangu aliibiwa 2017,kapiga tungi wakati wa kurudi home akapaki pembeni kwenda kukojoa ,kurudi ndani ya gari mambo yamemzidi akapiga usingizi hata milango ipo wazi ,wakaja wahuni wakamsukuma tu nje wakawasha gari Harrier ikaenda kirahisi hadi leo hajapata
Yuko mwingine Sinza, enzi zile unatoa gari bandarini bila namba, namba unaifuatilia kesho yake. Jamaa kaja home na mark two mayai haina namba Wala bima. Kufika home waif Yuko jikoni, jamaa kwa Raha alizokua nazo kamchukua binti yake wskaenda duka la jirani kununua vitu ili ajipongeze. Wahuni nao kumbe wanamfuata, alipotoka kwenye gari hakufunga milango na lok. Ile anatoka na kibinti wakati wanaagizwa vitu dukani wahuni wakaingia kwa gari na spare key ambayo waliuziwa na walinzi bandarini kwa Bei ndogo tu. Wakawasha gari ikiwa na dokoment zote na kutokomea kusikojulikana.
 
Maisha ya mwanadamu yamejaliwa nankumbukumbu nyingi sana, nyingi na mbaya, zenye kutufundisha na zenye kuburudisha. Al mradi ni matukio yalitokea na yakapita.

Nakumbuka mwaka 2018, tarehe kama ya leo, na mwezi huu huu, nikiwa na gari ndio lina siku nne tu tangu lipite pale gati namba mbili na kutua mikononi mwangu, mzee nikajitoma nalo Bar, Maryland Mwenge.

Kilichonipeleka hapo bar, niweze kukutana na mrembo mantashahu, chotara wa Kigiriki na Kichaga, mtoto mwenye urefu wake wa futi tano point kumi na moja, chuchu mkuki, viwango vya kimataifa.

Kabla sijafika Maryland nilikuwa Break Point ya mjini, kisha nikaingia The Governors Kinondoni, lakini cha kustaajabisha nilikuwa nikikutana na sura zilezile.

Nilipofika Mwenge nikampigia bibie kwamba niko ndani ya nyumba namsubiri yeye ili tuanze safari ya kwenda Morogoro kula raha za dunia.

Kabla hajafika, wakaingia jamaa ambao nimekuwa nikiwaona tangu Break Point, na The Governors.

Moja kwa moja wakaja kwangu, mmoja akatoa bastola na kuniwekea kidevuni, wakati ubaridi wa mtutu wa bastola ukikikera kidevu changu, mara nikaona mwingine naye anatoa bastola yake na kupiga risasi tatu hewani, wakasema niwape funguo ya gari.

Nikawapa funguo, wakaondoka huku wakipiga risasi hewani kuwatisha watu wasiwafuate.

Nikabaki hapo bar nimepigwa na bumbuwazi. Nikawapigia simu rafiki zangu mapolisi akiwemo Mentor wa JamiiForums.

Jitihada za kulisaka gari zikaanza mara moja. Mimi na ubwege wangu nikaendelea kubung'aa pale Maryland kama kada wa CCM aliyekosa wali maharage wa kampeni.

Hazikufika dakika kumi, jamaa (majambazi) wakarudi tena na kunikuta pale, wakanibebamsobemsobe hadi kwenye gari yao, wakanitupia humo na wakatoa gari mbio huku wakiendesha kuelekea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Tulipofika maeneo ya Udasa tukakuta gari imezimika, na haiwezi kuwaka mpaka uweze kugusa sehemu fulani.

Ilikuwa kila ikipiga kengele watakiwa kugusa sehemu hiyo. Basi wakaniambia niwaonyeshe sehemuya kugusa ili gari isizime.

Nikapagusa nikawaambia wawashe,wakaiwasha, wakanissukumia huko chini wakatoka nduki na kuniacha kwenye viwanja vya chuo.

Nilitoka nduki hadi nilipopata daladala la kwenda Makumbusho nikapanda huku nikitweta, nikarudi nyumbani Kijitonyama.

Usiku mida ya saa tatu nikapigiwa simu kuwa gari yangu imepatikana mitaa ya Kimara Baruti ilizimika barabarani.

Kile kitufe kilikuwa kina sense fingerprint walishindwa kuendelea kuliendesha gari lile na hawakuwa na sehemu nyingine ya kunipata.

Tangu siku hiyo nikajifunza kwamba sitakiwi kuonana na mtu mara mbili sehemu mbili tofauti.

Pia nikajifunza nikipatwa na jambo lolote ni lazima nihame eneo la tukio.

Kingine nilichojifunza ni umuhimu wa mifumo ya usalama kwenye gari, gps for vehicle tracking nk.

Pia nilijifunza umuhimu wa kuwa na bima kubwa kwa chombo chako.

Hiyo ndiyo kumbukizi yangu ya alhamis ya leo

Ha ha 2018, umefuata mrembo Maryland huyo mrembo hawezi kuwa mrembo haswa haswa Kama unavyosema asababishe wewe kuibiwa gari...mrembo wa hizo sifa umkute Maryland Bora hata governors
 
Yuko mwingine Sinza, enzi zile unatoa gari bandarini bila namba, namba unaifuatilia kesho yake. Jamaa kaja home na mark two mayai haina namba Wala bima. Kufika home waif Yuko jikoni, jamaa kwa Raha alizokua nazo kamchukua binti yake wskaenda duka la jirani kununua vitu ili ajipongeze. Wahuni nao kumbe wanamfuata, alipotoka kwenye gari hakufunga milango na lok. Ile anatoka na kibinti wakati wanaagizwa vitu dukani wahuni wakaingia kwa gari na spare key ambayo waliuziwa na walinzi bandarini kwa Bei ndogo tu. Wakawasha gari ikiwa na dokoment zote na kutokomea kusikojulikana.
wahuni walishasoma mchezo vizuri , aisee inaumiza lakini
 
wahuni walishasoma mchezo vizuri , aisee inaumiza lakini
Walinzi wa bandari hua wanawauzia zile funguo za akiba majambazi na siku gari inatoka bandari wanawatonya kwamba Ile Subaru tuliyokupa ufunguo wake Leo inatoka. Basi ukitoka geti 2 unakua unafuatiliwa tu. Fanya kosa ingia bar.
 
Bujibuji mi ningependa tu kujua huyu[emoji116][emoji116]ni ww?
JamiiForums-2068367120.jpg
 
Stori imejaa chumvi nyingi na ichanganywa na unga wa mhogo.

Majambazi wapige risasi hewani kwenye umma, wakimbie, wafike huko warudi tena eneo lile lile tena mwenge.

Sawa bwana.
kweli aisee maaana kuna risk ya polisi kuwa tayari wamefika eneo la tukio. Jamaa katupiga chai bila sukari
 
Kwahyo somo la uzinzi hukulipata eee? Maana hilo ndo chanzo. Sasa na kuambia uzinzi na divai mpya ninoma.
 
Ila kuna jamaa hapa jirani kwangu aliibiwa 2017,kapiga tungi wakati wa kurudi home akapaki pembeni kwenda kukojoa ,kurudi ndani ya gari mambo yamemzidi akapiga usingizi hata milango ipo wazi ,wakaja wahuni wakamsukuma tu nje wakawasha gari Harrier ikaenda kirahisi hadi leo hajapata
Mambo ya kulewa kizembe hayo😀
 
Back
Top Bottom