Jinsi nilivyomuokoa mzee mmoja na njama za kutaka kuuawa na kijana wake

Jinsi nilivyomuokoa mzee mmoja na njama za kutaka kuuawa na kijana wake

Miaka kama 13 imepita wakati huo tukiwa Ilboru sekondari nilikuwa na rafiki yangu mmoja ambaye tulikuwa tunaishi jirani kwenye jiji moja la kanda ya ziwa

Tulikuwa hatufahamiani kabla, tulifahamiana wakati tunaanza kidato cha kwanza tulipokuwa shule na urafiki ukaanzia hapo

Siku moja tumerudi nyumbani likizo alinikaribisha nyumbani kwao nami nikafika

Tukiwa pale nyumbani aliniambia kuwa mama yake mzazi aliondoka yaani waliachana na baba na hivyo baba yake akaoa mke mwingine ambaye hakuwa na umri mkubwa sana kama 24 hivi

Familia hiyo yenye asili ya kaskazini mzee alikuwa na gereji kubwa hapo jijini, maduka mawili ya vifaa vya ujenzi na spea za magari

Pia alikuwa na uwekezaji wa madini huko kahama sasa siku hiyo tunaondoka kutoka nyumbani kwao alinisindikiza ,alichukua ufunguo wa gari akanambia panda humu nikusindikize ,nilishangaa sana kwamba kwa umri miaka 15 anajua kuendesha gari

Basi akaendesha tulipofika mjini akanambia kwanza tupige misele mjini mara tunaenda kuwatafuta mademu waliokuwa wanasoma nao huko seminary primary

Katika urafiki wangu na yule kijana alipenda starehe sana kuliko kusoma na likizo nzima nikimwambia tuanze kusoma anakwambia yupo bize mara aende dukani kumsadia mfanyakazi wao, mara aendeshe gari mpaka kahama, Geita na hakuwa na leseni ila pesa kila kitu njiani

Hata tulipokuwa shuleni dogo yeye hana muda wa kusoma stories zake ni pesa, madem na magari

Tukiwa kidato cha tatu dogo walivurugana na walimu na wakamuita mzazi wake kama hamhamishi watamfukuza shule hivyo mzazi wake akaamua kumhamishia private moja huko Bukoba

Urafiki uliendelea na tulikuwa tunakutana nyumbani kipindi cha likizo na maisha yake ni kudrive magari ya baba yake

Baada ya matokeo ya kidato cha nne kutoka aliscore 0 wakati huo mimi nikiwa na 3 pia alichangia mimi kupata hizo alama kwa misele na stories zake

Baba yake alipopata habari kuwa mwanae aliscore 0 alimgombeza sana na wala kijana hakushtuka yeye aliendelea kula maisha na magari ya baba yake na pikipiki muda mwingine

Baba yake akamtaka amrudishe shule kijana akagoma baba yake akampeleka gereji yake afundishwe ufundi ,kijana akagoma mzazi akamtishia kumfukuza nyumbani lakini baadae kijana akakubali

Siku moja alichukua gari la baba yake akaondoka kusikojulikana na baada ya wiki moja akajikuta yupo lockup Dodoma kituo cha polisi kwa kuendesha gari bila leseni,mzazi wake aliambiwa akaenda akamtoa akamrudisha nyumbani na akamwambia mzazi wake hataki ufundi wala kitu chochote anahitaji akae nyumbani tu na hata kukaa dukani hataki

Basi mzazi wake akamuacha,kijana ni kudrive magari ya mzee mjini na kama hana hela ya mafuta anamuomba mama mdogo hela anaenda kujaza ,akaanza mazoea na mama mdogo wakaingia kwenye mahusiano ya kimapenzi

Baba yake akaanza kuwa na mashaka kati ya kijana wake na mkewe ,baada ya baba kuwatia mashakani,kijana na mama mdogo wakaanza kuandaa mikakati ya kumuondoa uhai

Wakapanga kuwa wakisha muondoa huyo mzee wanauza kila kitu wanahamia Mbeya au Tunduma lakini kabla ya hayo ili kuwarahisishia kuchukua mali zote lazima watumie mbinu ili mzee aandike wosia wa kuwagawia mali kijana na mama mdogo ,cha kukuongezea ni kwamba mama mdogo alikuwa amezaa na mzee watoto wawili wa kike na kijana alikuwa na mdogo wake mmoja wa kike ambaye muda mwingi anasomea Uganda

Mipango ya kutaka kuandaa wosia inaanza kufanyika na lengo la wosia ni kuwa baada ya kumuondoa uhai ndugu wa marehemu wasiwe na nguvu ya kuongelea mali na sasa na mimi nadokezewa hili dili kwa posho ya milioni 5 nikifanikiwa kufanya yafuatayo

Itaendelea................Nilienda kunywa maji sasa naendelea

Baada ya kupewa hilo dili la milioni 5 Dada(mama mdogo wa jamaa) aliniita hotel moja maeneo ya Ghana ilikuwa saa 12 jioni akaanza kunitaka nifanye yafuatayo

Kwanza ataniletea documents za mzee vitambulisho,leseni na vitu vingine niende nimtafute mwanasheria tuandike wosia kisha tutumie mbinu na huyo mwanasheria zipate muhuri wa mahakama na akanipa orodha ya mali kwenye karatasi na picha ya saini ya mzee ,passport za mzee,huyo mwanamke,passport za watoto wote ,akanipa na akanipa barua ya serikali za mitaa iliyogushiwa na vyeti vya kuzaliwa na cheti cha ndoa

Akanipa milioni moja kwa kuanzia na nikimpata mwanasheria aliyetayari tutampa kitu kidogo na mwanasheria asiwe wa Mwanza wala Shinyanga

Nikaingia kazini kumsaka mwanasheria, nilipokuwa nawahusisha wanasheria kama watatu hivi walikataa ,wakawa wanashauri kwa nini tusitumie mbinu za ushawishi wa kawaida yeye mzee aandike wosie kwa kigezo cha kuhofia ukoo kuwanyang'anya mali lolote likitokea kwa mzee?

Iliposhindana kwa hao watatu nikaamua kwenda chuoni SAUT nikampata kijana mmoja akawasiliana na ndugu yake akakubali kufanya hiyo kazi alikuwepo Tabora na akawataka hao wanafamilia ndo waende Tabora na nyaraka zote zinazohitajika na kiasi cha milioni 7

Nikamwambia mdada akakubali nikampa nyaraka zake zote akamwambia msela wake wakapanga tarehe ya kwenda Tabora

Kweli zoezi lilifanikiwa na cha kwangu wakanipa milioni mbili na nusu ikabaki milioni mbili na nusu ambayo wangenipa baadae baada ya Dada kudai hela ametumia yote nisubiri akusanye

Baada ya miezi kadhaa mdada alinipigia simu akinihitaji mara moja hotel moja maeneo Bwiru ,nikataka kujua kulikoni akanambia niende tu kuna mazungumzo,nikataka nijue mzee alipo kwanza akanambia yupo nje ya nchi basi nikaondoa wasiwasi nikaenda

Alikuwa na msela wake wanakunywa pombe basi nami nikajumuika pale mezani ,siku hiyo ndo nilijua malengo ya kutaka kujimilikisha mali hii ni baada ya kulewa kijana akawa anatamka wazi wazi kuwa ile mali ni yake na muda wowote atamuua mzee apishe ,asiwe kizingiti

Basi mwanamke akachukua laki tano akanipa ila akanionya kuwa nililosikia pale hata siku moja asije akalisikia sehemu nyingine na wakisikia nitakufa mara moja

Ilipofika saa 5 hivi dreva wao akawafuata na mimi nikachukua tax nikasepa zangu home

Asubuhi nilikuwa na mawazo sana kutokana na vitisho nilivyopewa ,nikataka niwareport polisi ila nikasema moyoni acha tu wakishanipa million 2 zangu zilizobaki naweza kuchukua hatua

Siku moja nipo zangu mjini nilipigiwa sim na mzee (baba yake msela) akanambia niende mahala fulani mtaa Fulani anambie,kwanza nilishangaa amepataje namba yangu ila nikawaza au deal limebuma au kuna nini ngoja nikamsikilizie

Alikuwepo Vila park kwa nje uwanja wa furahisha amepark gari lake pembezoni akanambia ingia ndani ,nikaingia nikakaa na yeye siti ya mbele

Mazungumzo yaakaanza,"Wewe ni rafiki yake sana R na tangu mkiwa sekondari,na pale kwangu nina mwanamke na unamjua vizuri ,hebu nambie nini kinachoendelea kati yako na yeye?

Nikapigwa na butwaa,nikanyamaza kidogo nikamwambia mzee yule mama J alikuwa ananiita maeneo mbalimbali hapa mjini kwa mambo kadha wa kadha ila naendelea kufanya uchunguzi yakikamilika nitakutafuta nikwambie"

Mzee akafyumu "Mambo gani,sema mambo gani hayo,yaani ujue kabisa nina abc zako kuhusu mke wangu,awali nilikuwa namuwazia R lakini nilipoongea na R kwa kirefu alikutaja wewe kuwa unatembea na mama J '"

Nikamwambia mzee siyo kweli,akanizaba makofi mawili akanambia nishuke na akaniambia nisipoachana na mke wake atanifanyia mbaya

Wakati narudi zangu R akanipigia sim kwamba amebanwa na mzee kuwa huenda mimi natembea na mama J ,nilivyoona yamefika shingoni nikaamua kukutaja ila cool down kesho nitakupa laki mbili ukapoze mikikimikiki "Nikamwambia poa

Kesho yake nikatumiwa hiyo laki mbili na ghafla mama yangu ananiita nyumbani ,kufika ananiambia kuna polisi wamekuja kukutafuta wamesema leo ufike kituoni kuna kitu wanataka kujua kutoka kwangu"

Awali mama alikuwa amenigombeza na akiwa anataka kujua nimefanya kosa gani basi nikamwambia hamna kitu

Nikaenda polisi kituo nilichoelekezwa nikaanza kuhojiwa kwa nini natembea na mke wa mtu

Nitaendele baadae.............

Basi polisi mmoja akaanza kunihoji kuwa natembea na mke wa mtu nikamuuliza "mke wa nani afande mbona simjui" Afande akaniambia "Bwana mdogo usijifanye hujui ,unamtesa mzee wa watu na tamaa ya pesa,na inasemekana yule mwanamke anakuhonga ,uongo kweli?" Nikawaza kidogo nikamwambia afande ngoja nikwambie ukweli "Mimi stembei na yule mama, yule mama anatembea na kijana wa yule mzee sijui kama unamfahamu?" Afande akajibu "Hapana simfahamu" nikaendelea kueleza ,"Yule mama si unamuona siyo aged siye mama yake mzazi wa huyo mama bali ,yule mzee walizinguana na mke wake akafukuza " Afande akasema "Mimi siwafahamu familia ya yule mzee ,tofauti na mzee mwenyewe siwafahamu wengine"

Basi mwishowe afande akanionya kuhusu kuwa na ukaribu na huyo mwanamke ila sikumdokezea swala la familia ya mzee kutaka kumfanyia unyama nilipiga kimya nikaondoka

Ilikuwa imefika saa 12 inaelekea saa moja nikiwa natembea barabarani gari haice ikaja ikasimama pembezoni barabarani ,akapiga honi dreva akaniita ,nikajiuliza labda ananifahamu,ile nafika mlangoni kwa dreva kumsikiliza,nikashtukia mlango unafunguliwa upande wa abiria narushwa ndani mlango unafungwa gari linaanza kukimbia

Mle kulikuwa na watu watatu wote sura ngeni,wakaninyang'anya sim yangu ,mle ndani kuna sit moja tu,nikapigwa makofi nikalazwa chini,nikafungwa na kamba mikono ,wakanifunika uso kwa kitambaa,ndo nikaanza kusikia mmoja ananiambia "Yule mwanamke ulishatembea naye mara ngapi na mpaka sasa alishakupa sh ngapi?

Nikawajibu huku nimelazwa kifudifudi kuwa" Mbona hakuna mwanamke ambaye nimewahi kutembea naye" Nikashushiwa fimbo matakoni kama 20 hivi nikiambiwa dogo usiposema unaenda kufa

Nikawambia "Jamani mimi stembei na mwanamke yeyote hapa mjini ,ila kuna mwanamke wa tajiri mmoja anaitwa mama j ndo mme wake ananituhumu "

Ndo mwingine akadakia "Tayari amekiri kuwa anatembea naye kwa hiyo tuache kumpiga huyo dogo"

Wakaacha kunipiga ,gari likakimbia muda mrefu kweli na sijui ninapoenda

Baada ya masaa mengi tu,gari likasimama ,nikasikia kalipe kivukoni",Nikawauliza sasa mnanipeleka wapi jamani ,"mmoja akanambia "Dogo kaa tulia la sivyo utapotezwa"

Nikanyamaza ,gari likazidi kuchanja mbuga sijui tunaenda wapi,nikawaza sasa hapo kuwa lipia kakate ticket kivukoni ni wapi hapa,kwa masaa yote kweli hapa ni Busisi kweli

Gari likaenda masafa kweli kweli ,baadae wakanifungua kama na kitambaa wakaniambia shuka upesi,kufika nje wakasema hilo ni onyo ukirudia hiki utakachokutana nacho hapa ni kidogo

Gari likaondoka wakaniacha ,kuangalia naona mistu tu,giza kali kweli na hata sijui nilipo ni wapi ,

Nikaaa pembezoni mwa njia ndogo sijui hata ni saa ngapi ,nasikia tu kelele za wadudu wapiga kelele vichakani nyakati za usiku

Nikawaza acha nitembee nielekee popote liwalo na liwe kama nitakutana na wanyama wakali humu hamna shida

Kadri nilivyokuwa natembea nikawa nasikia mlio wa mashine kama jenereta kwa mbali,nikawaza ngoja nifuate hiyo mashine ilipo ,mstu mnene kweli kweli

Nikasogea nikakuta majengo mengi na umeme umewaka hilo eneo,nikawaza ngoja niende hapa niombe msaada ,kufika nikaanza kubisha hodi kwa sauti kubwa sana,mlinzi akajitokeza akaniamrisha kaa chini,nikaaa akaniambia tembelea magoti uje mpaka huku muda huo tochi ipo usoni kwangu

Nitaendelea
Nitag
 
Inaendelea...... Basi baada ya kuona yule bwana mdogo amenisababishia zengwe, na Mimi nikaona sasa ni bora niwalipue yeye na hawara yake.
Baada ya kupokewa na maswali mazito mazito na wale walinzi wa yale maeneo, maana mwanzoni nilizani yupo mmoja kumbe walikuwa wapo wanne na kumbe siku chache zilizopita eneo hilo walifanyiwa bonge la ambush na majambazi, hivyo walikuwa makini sana na kila kinachokaribia maeneo yao.

Ilikuwa nusura yangu kubwa sana kusogea maeneo hayo huku nikipiga hodi kwa sauti kubwa maana kama ningependa Kama naingia pale nyegezi stand ya mabasi wangenishona shaba wale wazee.
Nashukuru Mungu walinielewa na kuniamini, japokuwa usiku kucha sikulala ilibidi iwe macho macho, mimi siwaamini wao hawaniamini. Kulipokucha Sasa nikapatiwa maelekezo ya jinsi yakuondoka maeneo hayo, kwa sharti la kila nilichokiona yaani mali za pale nifanye Kama sijaona chochote, yaani ni sawa na kuwa kipofu, wewe hauoni lolote lile.

Safari kurudi home ikaanza Sasa, ikumbukwe simu sina, pesa sina muda huo nilikuwa na nguo zangu na kende tu... Itaendelea....

Tusonge mbele Sasa, kichwani nilikuwa na maswali kibao, ikafikia wakati nikajiona mjinga sana, yaani milioni mbili na nusu, mara laki tano na tena laki mbili ya kupozwa baada ya kulambwa makofi na mzee wa mskaji ndio Leo hii zinataka kunitoa roho kweli?? Hapana nikifika tu town nalivuruga chaap..
Aisee nilitembea kinyama, wale mabaunsa walinipeleka mbali sana na viboko kibao nilikula.
WADAU NILIENDELEZE STORY? Nasubili maamuzi yenu hapa.
Mkuu songa mbele, usipoteze muda. Chap kwa haraka
 
Utajiri mwingine aurithiki wa makafara
Ndio utafte vyako hii kurithisha watoto mali ni ujinga watafte zao na hii mentality ndio inawafanya wawe lazy wakuue Ili wapate mali
 
Duuu sijui kwanini story tamu, hazinaga mwendolezo, au utasikia tukutane telegram
 
Kasha potelea kusiko julikana , moja ya mipango yangu ndani ya mwaka huu , ni kwamba nisijisumbue kufuatilia story yoyote ndani humu , ona sasa sijui nini kimenikuta mbaka nikaanza kuifuatilia story hii , natabaki nateska tu na kiu jamaa hata haendelei tujue mwishoe ikawaje .
We ndugu una vituko. Ila ndo jf huwezipata stress.
 
Aisee wadau acha tusonge mbele mbele.....
Inaendelea nilipoishia na hii ndio dawa yao japo na mimi nina kipolo changu huko.
Basi uwezi amini kipindi kile japo watumiaji wa simu hawakuwa wengi sana Ila kumbe ilikuwa muhimu sana kukariri japo namba chache za watu wangu wa Karibu kichwani. Pia napenda kuwakumbusha siku zote za maisha yako hapa duniani hakikisha unazo kichwani namba angalau 5 za watu wako wa Karibu, ili siku likikukuta la kukukuta huko usihangaike sana.

Nilibahatika kufika town kimazabe mazabe hivyo hivyo, kwanza kabla sijaenda home kwa bi mkubwa nikapitia gheto kwa rafiki yangu mmoja hivi ili anipe support ya kuelekea home, maana kwa jinsi bi mkubwa wangu alivyokuwa mtata asingenielewa hata kidogo.
Na sikutaka kumpa pressure kabisa kuhusu huu UTOPOLO uliokuwa unaniandama.
Mshkaji nilimpanga kila kitu kuhusu maujinga yote yanayonisibu, na ikaonekana ni heri zaidi nikatoe taarifa polisi, maana yule mzee alishaanza kuonekana mtu hatari sana kwangu, we jiulize hadi anawakodi watu wa kuniteka na kunipa vitisho?? Sasa siku akiamua kunipokonya namba si atanipokonya kizembe huyu!!? Chakufia mapema nini? eti kisa ushkaji ndio nivumilie maviboko yote Yale ambapo hata kule ilbolu sikuwai kuchapwa hivyo!!

....... Ngoma mpeto mpeto hadi kwa bi mkubwa, aisee kumkuta mother kapanick kinyama, kumbe yule dogo alifika home kuniulizia alafu alienda kiwaki sana kana kwamba anatafuta jambazi na RB mkononi, nikaona isiwe taabu sana acha nianze nao ligi isiyo na mdhamini. Mother nikampa story yote mwanzo mwisho na mwisho akaniwamba kofi eti kwanini wakati nalamba mikwanja ya advance toka kwa mama J sikumpa hata senti moja nyekundu!! Nyie njaa hizi acheni tu.

Itaendelea........

Tunaendelea Sasa, kutokana na kuonekana na bi mkubwa kuwa minoti nilitumia alone, yaani man alone bila kumshirikisha na yeye akajitoa kabisa kunisaidia, kwa ahadi ya siku nikiwekwa lupango atakuwa ananiletea viazi na uji siku moja moja hadi nikome kujifanya mwamba wa mipango mjini.
Ikaisha hiyo, mzee nikaingia ndani nikachange nguo, nikavaa magwanda ya vita sasa, kuna trouser yangu moja hiyo ya kitambaa chata Tokyo, huwa nikiivaa inanifichia umaskini wangu na hiyo huwa inavaliwa mara moja moja, either church kama nikioteshwa kwenda church siku hiyo, au sherehe za kikanisa kanisa.......

Juu nikapiga shati yangu ya mikono mifupi na kiatu kimoja hivi amaizing, ukiniangalia vibaya unaweza kudhani afisa wa TRA anapita mtaani kukagua wakwepa kodi, kumbe ni mbwa kala mbwa hiyo.
Ngoma hiyo na mpambe wangu moja kwa moja hadi kirumba police station, nia na madhumuni ilikuwa kwenda kutoa taarifa za vitisho nilivyotishwa pia kumshtaki yule father kwa kunihisi natembea na mke wake wakati sio kweli, na kuhusu yule dogo ( yaani mtoto wake) huyo sikuwa na shaka nae sana maana nilikuwa najua namna ya kumpata na kumtingisha kisawa sawa.
Nilikutana na yule kamanda wa mwanzo, nikamkumbusha tukio langu, na nikampa taarifa zote za jinsi nilivyovhukuliwa mkuku mkuku na bakora juu Hadi nje kabisa ya mji huko.

Baada ya kuandikisha maelezo, ikabaki issue ya mzee atafutwe ili tukae tuzungumze na sikuona sababu ya kumchukia kwa kitendo cha kunikodia wale wababe, maana nilijua fika uchungu wa mke.
Nilipomalizana na wandewa pale polisi, Sasa kazi ikawa ni kumtafuta yule shwaini muuzia wenzie matatizo. Kwa kuwa sehemu zake zote za kujiongezea dhambi kilazima nazijua, hivyo Mimi na mpambe wangu hatukupata shida sana kumfind huyo dogo.
Aisee nilipomuona nilipandwa na hasira kinyama, ukizingatia hadi muda huo siri zake sijavujisha alafu ndio kwanza yeye anaanza kuniangushia jumba bovu wakati mama ake anamtafuna mwenyewe. Nakajisemea je? wakisha mpunguza yule mzee wao si Mimi ndio nitaonekana muuaji?
Nikaona huu utakuwa ujinga Sasa, nikamsogelea nikamwuliza swali moja dogo tu, unataka nini tena toka kwangu, akajibu akasema, we malaya potea hapa, kima wa kidukuma wewe.

Hivyo nawaambia hadi leo hii nadhani nitakuwa na ufa kwenye fuvu la mbele la kichwa, maana nilimvika ndoo yule fackin hadi bar ikafungwa muda huo huo, ugomvi wake ulikuwa sio mchezo. Niliwasha moto wa kihabeshi siku hiyo na trouser yangu ya kichungaji mwanzo mwisho.
MSIPENDE KULA POP CORN TU, KUANDIKA KUNACHOSHA, NAJUA MTACHONGA SANA MABOTI ILA ITAENDELEA KESHO.
 
Back
Top Bottom