Jinsi nilivyonusurika kupata virusi vya UKIMWI

Jinsi nilivyonusurika kupata virusi vya UKIMWI

Nisamehe tu

Member
Joined
Mar 9, 2019
Posts
29
Reaction score
70
Habari za wakati huu Ndugu,

Natumai mu wazima wa afya ,Nawasalimu katika jina la ( JAMHURI YA MUUNGANO )Wakubwa shikamooni wadogo habari za mida,,pasipo kupoteza muda hii ni historia halisi ya maisha yangu ,lengo ni kumtaka aliye tayari awe Ndugu yangu ila nina uhitaji wa mtu kama baba au mama ,au dada ,nitatoa sababu mbele

Mimi ni kijana wa miaka 23 sasa ,nilizaliwa mkoani kagera na pia katika familia yangu tulizàliwa watoto wawili ,yaani Mimi na Mdogo wangu wa kike ,ni katika familia ya kati maana mama alikuwa na duka na baba alikuwa akimiliki gereji hivyo maisha ya nyumbani hayakuwa ya kukosa mlo ,ni mwaka 2002 mama angu alianza kuumwa sana kwa ugonjwa ambao Mimi sikuujua ilibidi ahamie kwa bibi ambaye ni mama yake.

Utokana na ule udogo nilokuwa nao basi hakika sikujua ni nini hasa ,kilimsumbua mama angu mzazi ,kutokana na udhaifu ule wa mama angu ilinibidi Mimi na Mdogo angu tuamie kwa bibi ili tuwe chini ya malezi ya ujombani ambako mama alikuwa hakiuguzwa kwa mda ule ,japo katika kuishi kwetu ujombani ilikuwa ni Mara chache sana kumuona baba yetu kuja hata kumjulia hali mama yetu ,ndipo mwaka 2004 ,mama angu mzazi alifariki (PUMZIKA KWA AMANI MAMA) basi baada ya msiba kukatokea mgogoro ni wapi sisi tunaenda kulelewa ni ujombani au kwao baba mzazi.

Mgogoro huu ulitokana na Ndugu upande wa baba kutuhitaji sana ila Ndugu upande wa mama hawakuwa tayari kwasababu ya uwepo wa migogoro ya muda mrefu kuhusu masuala ya ushirikina ,ya kuwa upande wa baba yangu ni wachawi hivyo hawataweza kutuacha tuishi ,Hakika kilikuwa kipindi kigumu katika umri wangu Mdogo sana ,mwisho tulisalia upande wa mama yaani ujombani ,ni katika kipindi hicho nilishaanza darasa la kwanza ,nikiwa niko chini ya uangalizi wa bibi yangu.

KUGUNDUA UWEPO WA GONJWA LA UKIMWI KATIKA FAMILIA YANGU.

Niliendelea kusoma katika shule ya msingi iitwayo rwemishasha A ,nikiwa darasa la tano ,nilianza kushuhudia Mdogo wangu akipewa dawa alfajili na jioni japo zilikuwa dawa za hospitalini ila sikujua zilikuwa ni za nini ,dawa zile alikuwa anapimiwa anapewa na bibi zilikuwa ni za kunywa ,nikizikumbuka dawa zile kwa jina la ZINOVIDININE ,MENOVIC na majina mengine ambayo sikuyajua ,Ni wakati mmoja jioni Sana nilimsikia mdogo wangu akilalamika ya kuwa ni lini ataacha kunywa hizo dawa ,nikagundua kuwa basi ni mda atakuwa kaanza kutumia sawa zile ,Bahati mbaya ujio na huduma za baba yetu nyumbani pale vilikuwa adimu sana maana mda mwingi bibi alilalamika sana kuzidiwa na majukumu ya kutulea na baba kutotujulia hali ,Nimeishi na bibi kwa tabu sana maana naye hakuwa na kazi yoyote zaidi ya kutegemea kodi ya vyumba viwili alovyokuwa navyo pale

Hakika tuliishi kwa kubangaiza ila bibi alitukatza kuonesha shida kwa watu ,maana siku zote aliniambia "kidogo nikipata tutakula mwanangu nikikosa mridhike" watoto wake yaani wajomba zangu na mama wadogo zangu hawakuwa na msaada bado kwa bibi .Nikiwa niko darasa la saba ndipo baba yangu alifariki ,tukiwa msibani ndipo nilijua baba yangu alikuwa muathirika wa gonjwa la UKIMWI ,maana watu waliongea wazi na kuongeza pia ni ugonjwa huo huo ulimuuua mama yangu lakini ,wakaeleza kinagaubaga ya kuwa hata Mimi na Mdogo wangu tulizaliwa na ugonjwa huo pia ,nilipoyasikia haya na kuzikumbuka dawa Mdogo wangu anatumia niliumia sana na kujua ni kweli nikawa mwingi wa huzuni ila huzuni ule uliongezwa na fujo zilizotokea siku ya mirathi ya baba kuonekana kila kitu eti ni mali aliziwaachia Ndugu zake kwa maandishi ya kusema hakuwa na imani kama sisi tulikuwa wanae ,hakika niliumia sana na hali ya Mdogo wangu haikuwa sawa maana alisumbuliwa na magonjwa nyemelezi sana.

Baada ya msiba maisha yaliendelea sasa nikiwa yatima kamili ,mwaka 2010 nilifanya mtihani wa darasa la saba ,nikafauli vizuri kwa kuchaguliwa shule ya mkoa ,BUKOBA SECONDARY ,Ni pale nilisoma mpaka kidato cha nne ,japo kutokana na changamoto za kutohudhuria shule Mara kwa Mara kuifuatilia afya ya Mdogo wangu maana mda mwingi alikuwa akilazwa hivyo nilijikuta nakuwa na ufaulu wa wastani sana toka form 1mpaka 4 japo nilitokea kuwa kipenzi cha walimu wa masomo ya sanaa kwa uwezo wangu wa kujieleza na kujenga hoja na ushawishi ,japo walipenda kuniuliza kkwanini Mimi ni mtoro wa Mara kwa Mara sikuwahi waambia maana bibi alinikanya kupenda kueleza mambo binafsi kipindi hicho ,hivyo niliendelea kupewa adhabu kila niwapo mtoro sikujali sana ,

Baada ya matokeo ya form two kutoka niliffanikiwa kufaulu vizuri nikiwa mwanafunzi niliyeongoza kwa masomo ya sanaa katika ufaulu wa juu ,hivyo kutokana na shida nilizokuwa napitia ilinibidi form three niende ambako ni rahisi kwangu kwa hali yangu hivyo rasmi nikasoma mchepuo wa sanaa ,hivy matokeo ya form four nikafanikiwa kuwa na matokeo mazuri ya kuniruhusu kuendelea mbele kwa kiasi Fulani hali ya Mdogo wangu kipindi hiki iliimarika kidogo ,akaweza endelea na masomo yake pia ,nikawa nimechaguliwa kujiunga na kidato cha tano ,shule ya wavulana KAHORORO iliyoko mkoani kagera ,ila usisahau kuwa ninakumbuka msibani watu walisema mimi na Mdogo wangu ni waathirika wa UKIMWI, Hivyo nilikata shauri kuwa naenda kupima nikijikuta ni muathirika basi sitaendelea na mambo ya elimu ,

Baada ya kupima niliambiwa Mimi ni mzima wa afya ,ni hapo nikaanza kumtafuta mtu anidhamini katika masomo yangu hayo maana kwa hali ya bibi asingeweza Mimi kupata hela ya kununua vifaa na ada ,nilienda kwenye mashirika ya kidini mengi sikupata msaada zaidi niliambiwa nisubili ,nikiwa katika kuhangaika huko nikapata mfadhiri ambaye aliamua kunipeleka shule ya binafsi iliyoko dar ea salaam ,huyu aliitwa mchungaji samweli huyu aliniahidi kunisomesha huko dar es sala kwa makubaliano ,nikimaliza itanibidi nisome theology maana alisema ananiona nikiwa mchungaji na kiongozi ,hivyo alifanya maandalizi yote ikiwemo kutumia mda mwingi kumshawishi bibi kukibali Mimi kwenda kusoma huko hatimaye nilisafir na mchungaji mpaka dar ,na tulifikia ubungo riverside ambako alikuwa na wenyeji wake ,baada ya siku kadhaa alinipeleka katika shule iliyoko chini ya kanisa la Lutheran iliyoko kimara -bonyokwa ndipo nikaanza shule yangu ya upili yaani (advance) shule iliitwa Midlands high school.

ITAENDELEA
 
Mkuu fungua kurasa hizo, leo nipo lindo mpaka kuchee. Ila pole sana
 
Polee ndugu, naelewa uliyopitia, polee sana aisee.
 
Ikiendelea kumbuka kuweka vituo ili ambao tumeshwindwa kusoma tujaribu... Unaaandika kama uliruka shule ya msingi na kwenda sekondari moja kwa moja!
Habari za wakati huu Ndugu ,natumai mu wazima wa afya ,Nawasalimu katika jina la ( JAMHURI YA MUUNGANO )Wakubwa shikamooni wadogo habari za mida,,pasipo kupoteza muda hii ni historia halisi ya maisha yangu ,lengo ni kumtaka aliye tayari awe Ndugu yangu ila nina uhitaji wa mtu kama baba au mama ,au dada ,nitatoa sababu mbele Mimi ni kijana wa miaka 23 sasa ,nilizaliwa mkoani kagera na pia katika familia yangu tulizàliwa watoto wawili ,yaani Mimi na Mdogo wangu wa kike ,ni katika familia ya kati maana mama alikuwa na duka na baba alikuwa akimiliki gereji
 
Ndefu sana haina mpangilio wa aya nimeshindwa kusoma ila pole kwa yote!
 
Ndefu sana haina mpangilio wa aya nimeshindwa kusoma ila pole kwa yote!

Ndio mimi siku hizi sisomi za hv. Naangalia kwanza chini nikikuta tu "itaendelea", naahirisha kusoma.

Yani post ndeeefu na bila hata mpangilio wala haya, halafu uniambie inaendelea? Like i am not bored enough already...
 
Pole kiongozi

Tunapenda kujiita majina yenye taswira mbaya kwa wanaotuzunguza,
Make yourself a badass licha ya kuwa na matatizo

All of these Mpauko shivo Unyayo Nisamehe tu ni baadhi ya majina ya washiriki wenye mada zinazo narrate changamoto zao.

I dont think that's a good idea
 
Inaendelea .....
Samahani kwa uandishi mbaya ,simu inasumbua kidogo ,nivumilie tumalize
Basi masomo yangu ya kidato cha tano yaliendelea vizuri kabisa ,nikiwa ni mwanafunzi bora kwa mchepuo wa HGL kwa wakati wote .Katika mwaka wangu wote wa kidato cha tano ni Mara moja tu ,mfadhiri wangu alinitembelea na hapo alinieleza kuwa nabaki pale shuleni wakati wote wa likizo
.Hivyo nilikuwa nabaki pale pamoja na walimu maana wengi waliishi pale ,nilijitaidi kufanya shughuli ndogo za pale kipindi cha likizo ,hivyo walimu walinipenda sana na kutamani niwaeleze kinagaubaga juu ya maisha yangu ,ila kwa wakati ule sikuwa tayari hivyo sikuwahi eleza historia yangu , Katika likizo ya mwisho ya kidato cha tano ili niingie kidato cha sita ,siku moja siku ya ijumaa nilistuka ghafra naitwa na Mkuu wa shule ya kuwa kuna mgeni wangu ,Nilienda ofisini kumsikiliza mgeni husika .Alikuwa ni dada aliyejitambulisha kwa jina la Linah na kusema kaagizwa na mchungaji samwel ili anijulishe ya kuwa Mdogo wangu amefariki na amekuwa akiumwa kwa majuma kadhaa. Niliumia sana siku ile nakujutia kuzaliwa .Yule dada alinieleza ni safari tu ndiyo iliyo mbele yetu kwenda msibani .Basi alisema nitaondoka naye mpaka kwake na kesho tutakuwa safarini kwenda bukoba /kagera ,na tuliondoka mpaka kwake upanga. Tulilala pale japo usiku mzima sikulala nilikuwa mwingi wa machozi na mawazo mengi .Alfajili alikuja yule dada linah na kunieleza niendelee kulala tutakuwa na safari saa nne ,hivyo nijitaidi angalau saa moja na nusu ndiyo niamke ,niliwaza na kuwazua vipi kwetu kulivyo mbali vile nianze safari saa nne ,Ila baada ya mda kadhaa muda wa saa mbili kuelekea saa tatu tulikuwa njiani kuelekea airport tukiwa tunaendeshwa na mmewe ,hiyo ilikuwa baada ya kifungua kinywa pale nyumbani ,Baada ya taratibu zote pale airport za ukaguzi ,tuliweza kusafiri mpaka nyumbani Kagera baada ya kufika airport ilibidi Mimi ndiye niwe muongozaji maana yule dada alikuwa ni mgeni kule ,Tulifika msibani nikawakuta Ndugu zangu upande wa mama wapo ila ndugu upande wa baba hata mmoja sikumtia machoni ,hilo liliniongezea uchungu ,basi mazishi yalifanyika na baada ya siku nne ,.Yule dada aliniqmbia mchungaji samwel anahitaji kuzungumza na mimi kwa simu maana kwa maelezo ya dada ni kuwa mchungaji mda huo hakuwepo Tanzania ,nilizungumza naye alinitia moyo sana na kunisihi sasa rasmi nirudi shule ,yeye yuko pamoja na Mimi ,wakati wa kurudi haikuwa kama tulivyokuja kwani tulipanda ndege tukashushwa mwanza ,hapo mwanza dada alikuwa na shughuli zake alienda kuzifuatilia baada ya siku mbili tena ndiyo safari ya dar es salaam ilifana ,baada ya kufika dar alinipa laki moja na nusu na akanirudisha shule na kudai ataendelea kuja kuniona nijitaidi sana ,.Hivyo akawa ameondoka nikaendelea na masomo ila ile laki na nusu nilitoa elfu ishirini na iliyobaki nikamkabidhi mhasibu maana alikuwa akinitunzia hela ya matumizi ambayo mchungaji alinitumia ni Mara nyingi ile hela sikuitoa hata kidogo
Basi niliendelea na masomo kwa nguvu huku nikiwa namkumbuka bibi yangu aliyeniaga nikiwa narudi dar kwa machozi akiwa analia huku akinitamkia maneno haya ya lugha ya kihaya (GENDA MWANAWANGE OSHOME OYEKAZA ,NANYE KOLAMALA KUSHOMA BASI MUKAMA ANTWALE ,MUKAMA AKWEMBEMBELE),Kwa taafsiri ya nenda mwanangu jikaze usome ,ukimaliza na Mimi Mungu anichukue ,Mungu akutangulie
ITAENDELEA.
 
Inaendelea .....
Samahani kwa uandishi mbaya ,simu inasumbua kidogo ,nivumilie tumalize
Basi masomo yangu ya kidato cha tano yaliendelea vizuri kabisa ,nikiwa ni mwanafunzi bora kwa mchepuo wa HGL kwa wakati wote .Katika mwaka wangu wote wa kidato cha tano ni Mara moja tu ,mfadhiri wangu alinitembelea na hapo alinieleza kuwa nabaki pale shuleni wakati wote wa likizo
.Hivyo nilikuwa nabaki pale pamoja na walimu maana wengi waliishi pale ,nilijitaidi kufanya shughuli ndogo za pale kipindi cha likizo ,hivyo walimu walinipenda sana na kutamani niwaeleze kinagaubaga juu ya maisha yangu ,ila kwa wakati ule sikuwa tayari hivyo sikuwahi eleza historia yangu , Katika likizo ya mwisho ya kidato cha tano ili niingie kidato cha sita ,siku moja siku ya ijumaa nilistuka ghafra naitwa na Mkuu wa shule ya kuwa kuna mgeni wangu ,Nilienda ofisini kumsikiliza mgeni husika .Alikuwa ni dada aliyejitambulisha kwa jina la Linah na kusema kaagizwa na mchungaji samwel ili anijulishe ya kuwa Mdogo wangu amefariki na amekuwa akiumwa kwa majuma kadhaa. Niliumia sana siku ile nakujutia kuzaliwa .Yule dada alinieleza ni safari tu ndiyo iliyo mbele yetu kwenda msibani .Basi alisema nitaondoka naye mpaka kwake na kesho tutakuwa safarini kwenda bukoba /kagera ,na tuliondoka mpaka kwake upanga. Tulilala pale japo usiku mzima sikulala nilikuwa mwingi wa machozi na mawazo mengi .Alfajili alikuja yule dada linah na kunieleza niendelee kulala tutakuwa na safari saa nne ,hivyo nijitaidi angalau saa moja na nusu ndiyo niamke ,niliwaza na kuwazua vipi kwetu kulivyo mbali vile nianze safari saa nne ,Ila baada ya mda kadhaa muda wa saa mbili kuelekea saa tatu tulikuwa njiani kuelekea airport tukiwa tunaendeshwa na mmewe ,hiyo ilikuwa baada ya kifungua kinywa pale nyumbani ,Baada ya taratibu zote pale airport za ukaguzi ,tuliweza kusafiri mpaka nyumbani Kagera baada ya kufika airport ilibidi Mimi ndiye niwe muongozaji maana yule dada alikuwa ni mgeni kule ,Tulifika msibani nikawakuta Ndugu zangu upande wa mama wapo ila ndugu upande wa baba hata mmoja sikumtia machoni ,hilo liliniongezea uchungu ,basi mazishi yalifanyika na baada ya siku nne ,.Yule dada aliniqmbia mchungaji samwel anahitaji kuzungumza na mimi kwa simu maana kwa maelezo ya dada ni kuwa mchungaji mda huo hakuwepo Tanzania ,nilizungumza naye alinitia moyo sana na kunisihi sasa rasmi nirudi shule ,yeye yuko pamoja na Mimi ,wakati wa kurudi haikuwa kama tulivyokuja kwani tulipanda ndege tukashushwa mwanza ,hapo mwanza dada alikuwa na shughuli zake alienda kuzifuatilia baada ya siku mbili tena ndiyo safari ya dar es salaam ilifana ,baada ya kufika dar alinipa laki moja na nusu na akanirudisha shule na kudai ataendelea kuja kuniona nijitaidi sana ,.Hivyo akawa ameondoka nikaendelea na masomo ila ile laki na nusu nilitoa elfu ishirini na iliyobaki nikamkabidhi mhasibu maana alikuwa akinitunzia hela ya matumizi ambayo mchungaji alinitumia ni Mara nyingi ile hela sikuitoa hata kidogo
Basi niliendelea na masomo kwa nguvu huku nikiwa namkumbuka bibi yangu aliyeniaga nikiwa narudi dar kwa machozi akiwa analia huku akinitamkia maneno haya ya lugha ya kihaya (GENDA MWANAWANGE OSHOME OYEKAZA ,NANYE KOLAMALA KUSHOMA BASI MUKAMA ANTWALE ,MUKAMA AKWEMBEMBELE),Kwa taafsiri ya nenda mwanangu jikaze usome ,ukimaliza na Mimi Mungu anichukue ,Mungu akutangulie
ITAENDELEA.
Pole ndgu.
 
Maisha ni ya hovyo sana ,
Na ni safar ya kuhuzunisha sana,
 
Andika yote mahali, halafu huku uwe unapaste tu
 
(tarehe 20 Feb 2021)
(Wiki iliyopita Jumanne)
 
Maisha ninsafari ngumu inahitaji ujasiri kuvuka!! Mitihani ni migumu sana! Wazazi na walezi tujitahidi kuwapunguzia magumu ya maisha watoto wetu!
 
Back
Top Bottom