Habar wana JF
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo kiuweli nilipatwa na matatizo ya kuvamiwa na majambazi siku ya ijumaa.
Ilikuwa ni saa 5 usiku tukitokea sehemu Moja inaitwa Itigi kuja Manyoni baada ya kumaliza kukusanya pesa kwenye magoli ninayosimamia sijui kuna mtu alichoresha Raman kwamba tumekusanya hela wakaamua kutufatilia.
Tukiwa tumejiachia hatuna habar tulikuwa wa4 kwenye gari mara tukaona mdada akisimamisha gari akiwa amevaa suruali kabeba na begi mgongoni tukaona labda anaenda manyoni wacha tumsaidie kumbe tulikuwa kwenye mpango maalumu.
Mwenzetu akasema ngj nichimbe dawa nyie muulizeni anaenda wapi ile tunashuka tukawekw chini ya ulinzi tukanyang'anywa kila kitu kuanzia simu laptop na pesaa kiasi cha milioni 21 na laki 3.
Namshukuru mungu hakuna aliyeumizwa hata mmoja na kinachoniuma kuliko vyote ni simu yangu tu ndo Ilikuwa na kila kitu na pesaa wamechukua yani sjui nifanyeje.
NB:
Kwa yeyote anayependa mm kuwa hapa kuendeleza mada zetu pendwa za kule mmu unaweza nichangia hata 1000 ili nipate hata kasimu ka promotion wakat nasubiria kujipanga upya karibu pm nikupe namba ya mchango.
Natumia laptop jaman ya kazini huwez kwenda nayo home ndo shida yenyewe.