Jinsi nilivyothibitisha Uchawi, hutoamini nakwambia!

Jinsi nilivyothibitisha Uchawi, hutoamini nakwambia!

I had this experience....

Nyumba yetu ilikuwa iko karibu na bahari ... wakati wa usiku mwingi ninapenda kupanda balcony ghorofani kuvuta fegi.....mbele ya uzio wa nyumba ni barabara kubwa ,niliona washkaji wawili wamesimamisha pikipiki (250 XLR)...pembeni yao kulikuwa na demu wanamuongelesha....mara nikaona pikipiki imeondolewa kasi huku yule aliyekuwa ameshuka chini kuongea na Cutie akamdandia mwenzake mgongoni wkt pikipiki inaondoka hapo....nikawa ninamuangalia yule demu na barabarani taa zilikuwa ni kali tu ....ghafla demu akapotea...ilihali pembeni yake kulikuwa na kuta za nyumba pande zote....nilitupa kichungi nikakimbilia chumbani kujifunika mashuka....

Hizo mbanga zipo wakuu....
 
Ndugu zangu wa JamiiForums, napenda kushiriki nanyi tukio la kushangaza lililotokea maishani mwangu, ambalo lilinionyesha wazi kuwa uchawi upo! Mpaka leo nikikumbuka usiku ule, mwili hunisisimka na maswali hayaishi kichwani mwangu.

Usiku wa Ajabu

Ilikuwa ni usiku wa manane, saa nane hivi. Nyumba ilikuwa kimya kabisa, kila mtu amelala, lakini ghafla niliamka nikiwa na hisia ngeni. Kulikuwa na ukimya wa ajabu, ukimya ambao hukufanya usikie hata sauti ya mapigo ya moyo wako. Nilihisi kama kuna mtu au kitu ndani ya chumba changu, ingawa mlango ulikuwa umefungwa na madirisha yakiwa salama.

Niliinama kidogo nikatazama chini ya kitanda—hakukuwa na kitu. Nikanyanyuka taratibu na kuwasha taa ya simu yangu, kisha nikapeleka macho dirishani. Ndipo nikamuona mtu akisimama nje ya nyumba yangu, umbali wa kama mita tano, akiwa hana kiatu na amevalia mavazi meupe yaliyochafuka. Uso wake haukuwa wazi, lakini mwili wake ulikuwa umetulia kimya bila hata kusogea.

Nilihisi hofu ikianza kunizidia, lakini nikajipa ujasiri. “Labda ni mwizi,” nilijiambia, nikachukua fimbo yangu ndogo niliyokuwa nayo chumbani. Nikaamua kumfuata taratibu ili nione kama kweli ni mtu wa kawaida au kuna jambo lingine.

Tukio Lisiloeleweka

Nilipofungua mlango na kutoka nje, cha kushangaza ni kuwa mtu yule alionekana kama vile anateleza ardhini badala ya kutembea! Hakutembea kwa miguu kama binadamu wa kawaida. Niliendelea kumfuata kwa tahadhari, lakini kila nilipomsogelea, alionekana kusogea mbali zaidi bila hata kukimbia.

Nilipojaribu kupiga kelele ili majirani wasikie, sauti yangu haikutoka! Nilihisi kama koo langu limefungwa ghafla, kama mtu aliyebanwa na mkono wa ajabu! Hofu ilinizidi, nikaanza kurudi nyuma haraka kuelekea ndani. Nilipofika mlangoni na kugeuka kutazama tena, yule mtu alikuwa ametoweka ghafla—kana kwamba hakuwahi kuwepo!

Ushahidi wa Ajabu

Siku iliyofuata asubuhi, nilipowaeleza majirani kuhusu tukio hilo, baadhi yao waliniambia kuwa jirani yetu mmoja alifariki usiku huo huo nikiwa napambana na kiumbe kisichoeleweka! Inasemekana mtu huyo alikuwa anahusishwa na vitendo vya ushirikina na alishawahi kushukiwa kuwa mchawi wa mtaa.

Kwa hakika, tangu siku hiyo, niliamini kuwa kuna vitu ambavyo akili ya kawaida haiwezi kuelewa. Mpaka leo, sijui yule mtu alikuwa nani hasa, wala alitowekaje bila hata kusikika. Uchawi upo ndugu zangu, na mimi nimeshuhudia kwa macho yangu!

Je, umewahi kukutana na tukio kama hili? Niambie!
Hili tukio bado halitoshi kusema kuwa umemshuhudia mchawi. Bado haileti picha ya muujiza wa kichawi kwa haya matukio umesema hapa.

Na sijui kwanini unahusisha kifo cha huyo jirani na tukio la kuona hicho unachosema umeona? Na sijui kwanini umeita 'kupambania naye' wakati uliona tu na ukakimbilia ndani.

Labda kuna maelezo umesahau kuyaeleza hapa. Yaani kwa kukabwa koo lako sauti isisikike ndiyo uwe umepambana na mchawi hadi akafa? Kweli?

Na kiukweli tukio la kukabwa koo lako lilifanya nihisi ulikuwa kwenye ndoto ndefu ukadhani ni tukio halisi baada ya kuzinduka usingizi.

Ova
 
Hili tukio bado halitoshi kusema kuwa umemshuhudia mchawi. Bado haileti picha ya muujiza wa kichawi kwa haya matukio umesema hapa.

Na sijui kwanini unahusisha kifo cha huyo jirani na tukio la kuona hicho unachosema umeona? Na sijui kwanini umeita 'kupambania naye' wakati uliona tu na ukakimbilia ndani.

Labda kuna maelezo umesahau kuyaeleza hapa. Yaani kwa kukabwa koo lako sauti isisikike ndiyo uwe umepambana na mchawi hadi akafa? Kweli?

Na kiukweli tukio la kukabwa koo lako lilifanya nihisi ulikuwa kwenye ndoto ndefu ukadhani ni tukio halisi baada ya kuzinduka usingizi.

Ova
Nice !
 
Huamini kama Kuna uchawi?

Kuamini is one thing to show proof is another. Hakuna proof ya uchawi mahala popote pale zaid ya hearsay stories kama yako zinazosimuliwa na kuaminiwa na watu wajinga.

Kuna watu wanaamini wao ni mbwa, wengine wanaamini wao ni malaika na wengine mizimu. Mimi naamini nimewahi kwenda zanzibar kwa mguu toka DSM, mimi binafsi naamini na nataka na wewe uniamini. Ukiwa zwazwa utaamini.
 
Hili tukio bado halitoshi kusema kuwa umemshuhudia mchawi. Bado haileti picha ya muujiza wa kichawi kwa haya matukio umesema hapa.

Na sijui kwanini unahusisha kifo cha huyo jirani na tukio la kuona hicho unachosema umeona? Na sijui kwanini umeita 'kupambania naye' wakati uliona tu na ukakimbilia ndani.

Labda kuna maelezo umesahau kuyaeleza hapa. Yaani kwa kukabwa koo lako sauti isisikike ndiyo uwe umepambana na mchawi hadi akafa? Kweli?

Na kiukweli tukio la kukabwa koo lako lilifanya nihisi ulikuwa kwenye ndoto ndefu ukadhani ni tukio halisi baada ya kuzinduka usingizi.

Ova
Una vituko sana, nimechekaaaa.

Sijasoma hata post ya jamaa ila hii reply yako imenifanya nicheke kila aya!
 
Mwaka 2012 nilikuwa na geto chumba changu kipo usawa wa barabarani. Siku moja nimelala nikasikia sauti ya mkwaruzo kule barabarani wa ile watu kama wanafagia nikajiuliza inamaana ndio kumekucha?
chap nikainuka kuchukua sim niangalie saa nikakuta ni saa nane dk mbili nikajiuliza nani anafagia sasa muda huu? nikainuka kuelekea upande wa dirisha nikafunua pazia..
aisee nilichokishuhudia macho hayakuamin mpaka leo!
niliona watu wanafagia barabarani kilichonishangaza ni kwamba watu wanafagia barabarani halafu namna ya mjongeo wao wanatembea kinyume nyume!
niliwaza sana nini nakiona ama naota nikafikicha macho kuona vizuri.. ni watoto wamama na wanaume wachache kilikuwa kama kikundi cha watu zaidi ya 10 wanafagia wanatembea kinyume nyume kwenda kuzoa taka.
nikasema ngoja niende sebleni nicheki kwa engo nyingine.. nhee! si nikajigonga kwenye mavyombo nikasikia pametulia tulii! kwenda kufungua pazia nione tena nakuta peupe hamna mtu yani ndan za sekunde chache watu wamepotea. nikalala zangu huku nimejawa na hofu
 
Watu hawaamini kama uchawi upo mara nyingi nasema watu wenye mapepo wakiombewa kanisani na kupiga Yale makelele sio wajinga it's real na ni uthibitisho wa nguvu za giza
Mwaka 2012 nilikuwa na geto chumba changu kipo usawa wa barabarani. Siku moja nimelala nikasikia sauti ya mkwaruzo kule barabarani wa ile watu kama wanafagia nikajiuliza inamaana ndio kumekucha?
chap nikainuka kuchukua sim niangalie saa nikakuta ni saa nane dk mbili nikajiuliza nani anafagia sasa muda huu? nikainuka kuelekea upande wa dirisha nikafunua pazia..
aisee nilichokishuhudia macho hayakuamin mpaka leo!
niliona watu wanafagia barabarani kilichonishangaza ni kwamba watu wanafagia barabarani halafu namna ya mjongeo wao wanatembea kinyume nyume!
niliwaza sana nini nakiona ama naota nikafikicha macho kuona vizuri.. ni watoto wamama na wanaume wachache kilikuwa kama kikundi cha watu zaidi ya 10 wanafagia wanatembea kinyume nyume kwenda kuzoa taka.
nikasema ngoja niende sebleni nicheki kwa engo nyingine.. nhee! si nikajigonga kwenye mavyombo nikasikia pametulia tulii! kwenda kufungua pazia nione tena nakuta peupe hamna mtu yani ndan za sekunde chache watu wamepotea. nikalala zangu huku nimejawa na hofu
 
Kuamini is one thing to show proof is another. Hakuna proof ya uchawi mahala popote pale zaid ya hearsay stories kama yako zinazosimuliwa na kuaminiwa na watu wajinga.

Kuna watu wanaamini wao ni mbwa, wengine wanaamini wao ni malaika na wengine mizimu. Mimi naamini nimewahi kwenda zanzibar kwa mguu toka DSM, mimi binafsi naamini na nataka na wewe uniamini. Ukiwa zwazwa utaamini.
Unataka ku prove uchawi upo?
 
Mwaka 2012 nilikuwa na geto chumba changu kipo usawa wa barabarani. Siku moja nimelala nikasikia sauti ya mkwaruzo kule barabarani wa ile watu kama wanafagia nikajiuliza inamaana ndio kumekucha?
chap nikainuka kuchukua sim niangalie saa nikakuta ni saa nane dk mbili nikajiuliza nani anafagia sasa muda huu? nikainuka kuelekea upande wa dirisha nikafunua pazia..
aisee nilichokishuhudia macho hayakuamin mpaka leo!
niliona watu wanafagia barabarani kilichonishangaza ni kwamba watu wanafagia barabarani halafu namna ya mjongeo wao wanatembea kinyume nyume!
niliwaza sana nini nakiona ama naota nikafikicha macho kuona vizuri.. ni watoto wamama na wanaume wachache kilikuwa kama kikundi cha watu zaidi ya 10 wanafagia wanatembea kinyume nyume kwenda kuzoa taka.
nikasema ngoja niende sebleni nicheki kwa engo nyingine.. nhee! si nikajigonga kwenye mavyombo nikasikia pametulia tulii! kwenda kufungua pazia nione tena nakuta peupe hamna mtu yani ndan za sekunde chache watu wamepotea. nikalala zangu huku nimejawa na hofu
Tatizo uliparamia karai la vyombo 🤣🤣
 
N
I had this experience....

Nyumba yetu ilikuwa iko karibu na bahari ... wakati wa usiku mwingi ninapenda kupanda balcony ghorofani kuvuta fegi.....mbele ya uzio wa nyumba ni barabara kubwa ,niliona washkaji wawili wamesimamisha pikipiki (250 XLR)...pembeni yao kulikuwa na demu wanamuongelesha....mara nikaona pikipiki imeondolewa kasi huku yule aliyekuwa ameshuka chini kuongea na Cutie akamdandia mwenzake mgongoni wkt pikipiki inaondoka hapo....nikawa ninamuangalia yule demu na barabarani taa zilikuwa ni kali tu ....ghafla demu akapotea...ilihali pembeni yake kulikuwa na kuta za nyumba pande zote....nilitupa kichungi nikakimbilia chumbani kujifunika mashuka....

Hizo mbanga zipo wakuu....
Ngoja baadae nita andika Uzi mwingine apa wa jamaa yangu mmoja alikutana na jini porini
 
Ndugu zangu wa JamiiForums, napenda kushiriki nanyi tukio la kushangaza lililotokea maishani mwangu, ambalo lilinionyesha wazi kuwa uchawi upo! Mpaka leo nikikumbuka usiku ule, mwili hunisisimka na maswali hayaishi kichwani mwangu.

Usiku wa Ajabu

Ilikuwa ni usiku wa manane, saa nane hivi. Nyumba ilikuwa kimya kabisa, kila mtu amelala, lakini ghafla niliamka nikiwa na hisia ngeni. Kulikuwa na ukimya wa ajabu, ukimya ambao hukufanya usikie hata sauti ya mapigo ya moyo wako. Nilihisi kama kuna mtu au kitu ndani ya chumba changu, ingawa mlango ulikuwa umefungwa na madirisha yakiwa salama.

Niliinama kidogo nikatazama chini ya kitanda—hakukuwa na kitu. Nikanyanyuka taratibu na kuwasha taa ya simu yangu, kisha nikapeleka macho dirishani. Ndipo nikamuona mtu akisimama nje ya nyumba yangu, umbali wa kama mita tano, akiwa hana kiatu na amevalia mavazi meupe yaliyochafuka. Uso wake haukuwa wazi, lakini mwili wake ulikuwa umetulia kimya bila hata kusogea.

Nilihisi hofu ikianza kunizidia, lakini nikajipa ujasiri. “Labda ni mwizi,” nilijiambia, nikachukua fimbo yangu ndogo niliyokuwa nayo chumbani. Nikaamua kumfuata taratibu ili nione kama kweli ni mtu wa kawaida au kuna jambo lingine.

Tukio Lisiloeleweka

Nilipofungua mlango na kutoka nje, cha kushangaza ni kuwa mtu yule alionekana kama vile anateleza ardhini badala ya kutembea! Hakutembea kwa miguu kama binadamu wa kawaida. Niliendelea kumfuata kwa tahadhari, lakini kila nilipomsogelea, alionekana kusogea mbali zaidi bila hata kukimbia.

Nilipojaribu kupiga kelele ili majirani wasikie, sauti yangu haikutoka! Nilihisi kama koo langu limefungwa ghafla, kama mtu aliyebanwa na mkono wa ajabu! Hofu ilinizidi, nikaanza kurudi nyuma haraka kuelekea ndani. Nilipofika mlangoni na kugeuka kutazama tena, yule mtu alikuwa ametoweka ghafla—kana kwamba hakuwahi kuwepo!

Ushahidi wa Ajabu

Siku iliyofuata asubuhi, nilipowaeleza majirani kuhusu tukio hilo, baadhi yao waliniambia kuwa jirani yetu mmoja alifariki usiku huo huo nikiwa napambana na kiumbe kisichoeleweka! Inasemekana mtu huyo alikuwa anahusishwa na vitendo vya ushirikina na alishawahi kushukiwa kuwa mchawi wa mtaa.

Kwa hakika, tangu siku hiyo, niliamini kuwa kuna vitu ambavyo akili ya kawaida haiwezi kuelewa. Mpaka leo, sijui yule mtu alikuwa nani hasa, wala alitowekaje bila hata kusikika. Uchawi upo ndugu zangu, na mimi nimeshuhudia kwa macho yangu!

Je, umewahi kukutana na tukio kama hili? Niambie!

Mkuu upo vizuri sana kwa UTUNZI unafaa kuwaandikia bongo movie story.
 
Back
Top Bottom