Jinsi nilivyougua miaka mingi na kunusurika kifo baada ya kurogewa uchawi wa bundi

Pia tumia muda kujipanga zaidi ili kutoka kiutu cha Uhakika zaidi.

Unaposema shughuli ilikuwa mwaka 1975 kwenye shughuli ya kumtoa Mwali ambaye alikuwa Dada yako na ambaye sasa ana miaka 75, ina maana wakati wa Shughuli yake ya 'Kumtoa Mwali' alikuwa na miaka 30!

Huyo alikuwa ni Mwali ama Mke wa MTU?

Jipange
 
Basi sisomi tena kumbe ni chai tu kama chai zingine😆😆
 
Sasa hivi huyo dada ana miaka kama 75, ina maana ametolewa mwali akiwa na miaka 30 [emoji849]. Kwa kawaida mwali wanatolewa na miaka 13-18

Halafu huu mtindo wa itaendelea mmeutoa wapi? Bongo movie?

Kuna yule jamaa wa "Visa Mikasa vya Kusaka Utajiri", hajaendelea mpaka leo ... Ni Chizi Maarifa sijui
 
Hili hata mimi nililiona
 
watu wa zamani sana wengi wao hawajui miaka yao halisi ,hususa wale ambao hawakuenda shule .Huwa wanaweza kukutajia tu kipindi ,msimu au matukio ww ndio utang'amua umri wa makadilio wa mtu huyo kama haufahamu kuhusu matukio au vipindi hivyo vilitokea lini unaweza kushindwa hata kukadiria umri halisi.

Mtu anaweza kukwambia mm nilizaliwa wakati karibu na yale Mafuriko yaliyouwa watu wengi ndio ilivyo.
Mfano dada ukimuuliza umri wake atakwambia "Mimi nilizaliwa kabla kipindi cha Muumiani,yaani kipindi cha muumiani ndio maarufu Morogoro nilipata mtoto wa kwanza".

Ndio maana sijaandika kwamba ana miaka 75 neno lililotumika ni kama 75.

Tukumbuke nyakati zetu watu wengi hatukuwa na vyeti vya kuzaliwa wala mambo ya birthday kuhusu umri unajipimia tu mwenyewe.

Kiufupi ukimuuliza dada mwenyewe umri wa mtu hatokwambia kwa mwaka atakupa matukio tu.

Mfano nikimuuliza mm na mdogo wa mwisho tunatofautiana umri gani atakujibu "mdogo wa mwisho ulikuwa hauwezi kumbeba mgongoni mpaka umpandishe kitandani ndio unambeba".-Hapa kila mtu atakuja na jibu tofauti kwa kweli kuhusu tofauti y umri kati yangu na mdogo wa mwisho.
 
Ngoja hii comment niiweke kumbukumbu 😂😂😂😂
 
@Chizimaarifa katuacha na Alosto
 
Hii ya jina ilimsumbua dadangu yaani kila wiki analazwa na kuongezwa maji, akikanyaga shule basi hali mbaya. Tulitumia gharama nyingi mno wakati huo yupo Boarding school, akiripoti tu basi haipiti siku 2 tunaambiwa mgonjwa tunamsafirisha kurudi nyumbani. Lakini baada ya kurekebisha jina hakusumbua tena mpaka leo
 
Ebu fafanua vizuri, unasema Dada yako kwa Sasa Ana Kama miaka 75, na mwaka aliotolewa ni 1975 ina maana alikuwa na miaka 30 hivi unasema chuchu msumali kweli?
 
ahahahahaahahha chai ya Leo chumvi imezidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…