Jinsi Tanzania ilivyogeuzwa shamba la bibi

Jinsi Tanzania ilivyogeuzwa shamba la bibi

Ikiwa mtanzania mwenye asili ya kiasia anaitwa Mhindi, Je mtanzania mwenye asili kwa mfano ya kibantu ataiwa nani ?

Sababu wote ni watanzania na wote ni waafrika.

Punguzeni chuki zenu za kibaguzi, hawa watu wanafanikiwa kwa juhudi zao. Hicho kiwanda kikifungwa leo watu wangapi watakosa ajira ?
Kwa hii inaonekana wewe ni mnyapara katika viwanda vyao wahindi?ama haujawatembalea hawa jamaa ukaona jinsi walivyo na ubaguzi wa hali juu
 
Mkuu andika Article kwenye gazeti. Anza na yale ya kiingereza. Wahusika wote (wizara, uhamiaji) watayaona wenyewe.

Soma na Utekeleze Signature yangu hapo chini
nimekupata mkuu nitajitahidi kufanya hivyo
 
Vikwazo, hata avator yako inatosha kuwakilisha hii mada. Nchi yetu inatafunwa sana na hawa wageni, kwa kazi ambazo hata kijana aliyehitimu drs la saba anaweza kuzifanya. Ukifuatilia vibali vyao vya kufanya kazi nchini utakuta ni tofauti kabisa na kazi anayoifanya. Lakini haya yanafanyika kwa kusaidia na Ma-HR kwenye makampuni kwa kuwaita ni wataalam wenye fani zisizo hapa nchini.
Ni aibu na inatia hasira sana, leo hii ukienda kwenye makampuni ya migodi, walinzi na wapelezi wake ni weupe kutoka bondeni. Wagawa vyumba vya kulala ni hao hao. Ukikaa nao ukawauliza hivi inakuwaje mnapata vibali vya kazi hata hizi; wanakujibu "kwenye nchi yenu kama una pesa, kila kitu kinawezekana" Hili jibu mimi huwa linanitia aibu sana. Kuna mmoja anasema wakati anaitwa kuja hapa nchini kufanya kazi anayoifanya, alikuja lakini kwa mashaka sana kwa kuhofia angerudishiwa uwanja wa ndege, kwani alijua kzai hiyo kuna wazawa wanaweza kuifanya. Lakini alistaajabu, hadi leo ana miaka minne anafanya kazi hiyo bila bughudha yoyote.
Kuna hawa wenzetu wa bondeni SA, ni wanyanysaji sana. Lakini ndio viongozi wetu wanawaleta kila siku kama wataalam na wawekezaji. Enzi za nyuma waliitwa makaburu lakini sasa ni wawekezaji. Hivi huwezi kuwekeza, na kazi zikafanywa na wazawa?
 
Tofauti ya mishahara katika sekta binafsi ni jambo la kawaida hapa Tanzania tukiwa bado watoto wadogo mzee wetu mwl Nyerere alitwambia kuwa ubepari ni unyama hatukuelewa sasa wengi wetu tunaelewa tafsiri ya maneno hayo.Kuondokana na matatizo hayo na mengineyo watanzania tufanye uamuzi kubadili mfumo uliopo.
 
Kwa kweli inasikitisha, wageni ndo wanafaidi matunda ya nchi hii,watanzania tunakandamizwa tu, hii ni laana au nini?maisha haya mpaka lini?
 
Ikiwa mtanzania mwenye asili ya kiasia anaitwa Mhindi, Je mtanzania mwenye asili kwa mfano ya kibantu ataiwa nani ?

Sababu wote ni watanzania na wote ni waafrika.

Punguzeni chuki zenu za kibaguzi, hawa watu wanafanikiwa kwa juhudi zao. Hicho kiwanda kikifungwa leo watu wangapi watakosa ajira ?

Kila mfanya biashara anataka kazi yake ifanikiwe maana kuna mashindano makubwa huko kwenye jukwaa la biashara. Na watanzania hatuna sifa ya kufanya kazi kwa ufanisi , uvivu na ufisadi ndio sifa yetu kubwa leo.


Hawa ndio wafanyakazi wa ndani wa wahindi, wafua chupi na waosha vyombo na mayaya!
 
Back
Top Bottom