Jinsi uhamiaji Kenya wanatuponza, Watanzania wanaingia ingia tu watakavyo


Watatuletea balaa sana hawa, kwao wamegoma kuchukua tahadhari, halafu nchi yote wanategemea maabara moja tu, hivyo hata kupima kwenyewe wanafanya tu ili wafanye lakini hawachukulii serious, bado wanasongamana kwenye madaladala na kila sehemu, halafu hawataki kutulia kwao, kwa njaa zao wanang'ang'ania kuja huku.
 
126 vs 20. Tunasubiri kesho igonge 135.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Appeal to those propagating hate towards Tanzania in here, come out and help to brind order

 
Nani aje kufa huko?

Ndugu zako waganga njaa, wameshindwa kuvumilia wiki hizi mbili huko kwenu.....wanatuponza maana nyie testing zimewashinda hamfanyi kwa kasi, sasa mkiachia achia ndugu zenu kwa njaa zao kuruka ruka huku na kule mtattutia kwenye matatizo.
 
Ndugu zako waganga njaa, wameshindwa kuvumilia wiki hizi mbili huko kwenu.....wanatuponza maana nyie testing zimewashinda hamfanyi kwa kasi, sasa mkiachia achia ndugu zenu kwa njaa zao kuruka ruka huku na kule mtattutia kwenye matatizo.
Tuonyeshe impact yao kwenye maambukizi mkuu
 
Tuonyeshe impact yao kwenye maambukizi mkuu

Sasa hivi hiki kirusi hakuna anayejua kichwa chake wala mkia, kimeshtukiza dunia na kusababisha mataifa yote kufanya kitu ambacho hakijawahi kufanyika kwenye historia ya dunia hii, hivyo ukiambiwa kaa kwako, basi tulia vumilia mpaka tuelewe upepo wa hiki kitu. Kimetukosa kosa Afrika, bado hatujui kama kiliandaliwa kwenye maabara kwa ajili ya wazungu au kiliibuka chenyewe.
Hadi sasa hakuna anaye taarifa za jinsi gani Afrika hatujanasa vizuri, aidha kinatokota ndani yetu kikisubri kutufuta duniani au nini nyuma ya pazia, hivyo watu waache kiherehere, baki ndani kwako, binafsi hapa nina kamradi nimeagizwa kwenda kutia saini mkataba kule Ethiopia, ila nimegoma siendi hata kwa dawa, nazihitaji sana hizo hela zao lakini kwa sasa bora niziskie tu lakini sitasafiri.
 
Sawa braza nimekuelewa.. Ila unavyotushusha kana kwamba watz ni njaa njaa tunawategemea ninyi ili tuishi... I'm sure bado kuna wakenya wanavuka kuja tz kwa sasa ikichangiwa pia na hali ya covid baina ya haya mataifa mawili.... Hapa cha kufanya ni kuhakikisha hakuna movement yoyote baina ya haya mataifa mawili na pande zote mbili zitekeleze hili ipasavyo... Kutupiana mpira hivi sijui ikiletwa case humu ya ninyi kuvuka boda itakuwaje.
 

Nyie kwenu hamjafunga mpaka, hivyo Mkenya anayekuja huko hana haja ya kujificha, mkifunga na itokee kunao wanaokuja kinyemela kama wanavyofanya ndugu zenu, hapo mtakua na haki ya kutusema. Sisi tumefunga, ila tunashtukizwa na ndugu zenu wamefika mpaka Kenya ndani, juzi wamekamatwa sita na kuwekwa karantini, tena wamekamatwa maeneo ya Kenya kati.

Ingekua nchi yenu mnachukua tahadhari hamsongamaani na kufanya mambo ya hatari, wala hatungekua na wasiwasi wa ujio wa ndugu zenu, maana tungekua tunajua wanatokea kwenye nchi ambayo wako serious. Kwa mfano leo Waganda au Wanyarwanda wakitushtukiza, wala siwezi kuwa na wasiwasi sana maana kule kwao marais wao wamelichulia hili suala kwa kumaanisha sana, wanajiahidi sana, hawana utani, hairuhusiwi kukusanyika au misongamano.
 
Sawa mkuu,ila ninavyojua ukifunga mipaka umefunga kweli;hakuna kuingia hakuna kutoka.., unavyosema ninyi kuingia huku ni ruksa basi mmeifunga kimajina tu na si ajabu kuna wanaoingia huko bila kuwa noticed... Najua ikifika point hii ngoma imewazidia utaanza kuilaumu pia tz, lakn nikwambie tu sie hatuna impact yoyote hapo... ungewashauri pia wenzio wasiotekeleza amri ya kufunga mipaka kwa kuja huku waache;ningekuona wa maana zaidi... Tofauti na hapo hiyo amri ya mpakani mnaivunja wenyewe... Halafu sisi hatujalala usingizi kihivyo kwenye hili janga kama unavyojaribu kuaminisha umma.... Kuna measures mtafanana nchi na nchi ila kuna zingine mtatofautiana.
 
Ndugu zako waganga njaa, wameshindwa kuvumilia wiki hizi mbili huko kwenu.....wanatuponza maana nyie testing zimewashinda hamfanyi kwa kasi, sasa mkiachia achia ndugu zenu kwa njaa zao kuruka ruka huku na kule mtattutia kwenye matatizo.
Hili gonjwa halifichiki , fanya testing usifanye testing kama upo utawachapa vizuri na idadi ya wagonjwa mahospitalini itasema , hali za watu mtaani zitasema , ni kama pembe la ng'ombe halifichiki

Mlipokosea ni kuruhusu wale wachina waingie mtaani , hapo tu

sisi Huku kwetu hakuna kitu kama hicho

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Ndio maana uzi nilianza kwa kulaumu maafisa wa uhamiaji kwetu, tunaposhtukizwa na Watanzania huku Kenya kati ina maana wamelala hapo mpakani wanaachia kila mtu aingie atakavyo.
Sawa mtasema kwenu huko hamjalala ila tunayoyaona kwenye mitandao inaonyesha mumeendana kinyume na dunia, tunaona mkuu wa mkoa bwana Makonda amekusanya umati anahutubia, tunaona rais wenu akihutubia kwenye kanisa lililojaa waumini, ni wazi suala la msongamano hamjalichukulia kwa umakini.
Duniani mapolisi wanaingia mpaka kwenye nyumba za ibada na kushurutisha utiifu wa sheria, kule Nigeria polisi wanaingia kanisa na Biblia na kufungua maandiko kabisa na kuwasomea wachungaji haswa sehemu inayosema Mkristo atii uongozi na sheria za nchi.
 

Corona bado ni gonjwa jipya, hakuna anaayejua hata utalificha vipi, kwenu huko sijasema mnaficha, nimesema hamna uwezo hata wa kupima, mnapima watu 300 kwa wiki tatu wakati sisi tunapima hao 300 kwa siku moja.
Sema ni kwamba hili gonjwa halionekani kuwa na makali yoyote kwa Mwafrika, maana hata huku kwetu tunakopima watu wengi kwa mkupuo, bado vifo ni vichache, na hata idadi kubwa ya wanaogundulika nacho wanadunda tu ndani ya karantini, yaani hawapo kwenye ventilators wala nini, wengi hata wanatamani watoroke maana mtu anajihisi mzima ila kipimo kimeonysha anacho kirusi.
Hivyo kwa Mwafrika utakuta wengi wanadunda mtaani wanatamba tu nacho mwilini, akikohoa kidogo anchukulia poa kama mafua ya kawaida, na hadi anapona bila kujua lilikua Likorona limemtembelea bila ya yeye kujua. Hili limewashangaza wazungu maana walitegemea tufe kama milioni kumi hivi, ila Afrika yote vifo bado vichache na kirusi kinazagaa kimya kimya.

Wasiwasi wangu ni kisije kubadilika na kuanza kuzamisha watu huku, tuombe mzungu awe ameshapata dawa maana kawaida Miafrika hadi mzungu agundue hatuna uwezo huo.
 
my friend it's a two way traffic, hata wakenya wanaingia kiholela sana tanzania na mamlaka inajua ila nadhani kwa kwasababu ya issue ya ujirani na ku-share baadhi ya mila na desturi, authority imeamua kutokuwa serious.

ukitaka kuliamini hili, zungumza na watanzania waishio mpakani namanga na holoholo au tembelea arusha, dar na mwanza ukutane na wakenya wanaoishi kiholela wakifanya kazi zao bila kusumbuliwa na mtu.

imefika wakati, wengine hujitambulisha kama watanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…