BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
Jinsi wakili msomi Dickson Matata alivyompeleka puta mtoto wa IGP Mahita.
MATATA: Nikumbushe Majina yako.
SHAHIDI: Naitwa Inspector Mahita Omary Mahita.
MATATA: nitakuwa Sahihi nikisema wewe ni Mtoto wa IGP mstaafu Omary Mahita.
SHAHIDI: Upo sahihi
MATATA: Wakati Baba yako akiwa IGP wewe Ulikuwa wapi?
SHAHIDI: Nilikuwa Chuo kikuu
MATATA: Wakati Baba yako akiwa IGP ulikuwa na akili timamu?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Unakumbuka madai ya baba yako kuwakuta CUF na visu akadai wamekusudia kufanya ugaidi.
WAKILI WA JAMHURI: Objection Mheshimiwa Jaji. Naomba swali hilo liondolewe.
MATATA: Wakati mnawakamata watuhumiwa mlikuwa na Kikosi Maalum?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Kikosi chote kilitokea Arusha?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Na kikosi hicho kilikuwa chini ya RPC Kingai ambaye wakati huo alikua RCO Arusha?
SHAHIDI: Sahihi kabisa
MATATA: Unapotoka kwenye kituo unapaswa kuwa na Movement Order?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Ulipotoka Arusha kwenda Moshi hukueleza kuwa na movement order.
SHAHIDI: Nilikua nayo.
MATATA: Ulimweleza nani?
SHAHIDI: Sikueleza lakini nilikua nayo
MATATA: Maelezo yako ya awali hayaelezi hivyo.
SHAHIDI: Kimya.
MATATA: Je unajua kwamba unapofika mkoa mwingine unapaswa uriporti kwanza kwa Mlmamlaka za Mkoa huo?
SHAHIDI: Ni kweli.
MATATA: Katika maelezo yako hakuna popote uliposema umeripoti kwa mamlaka za polisi Moshi.
SHAHIDI: Ni kweli lakini?
MATATA: Hakuna lakini, jibu NDIYO au HAPANA.
SHAHIDI: Niliripoti lakini labda kwenye maelezo nilisahau kuandika.
MATATA: sasa kama hukuandika ulitegemea mahakama iote?
SHAHIDI: Kimya
MATATA: Una ushahidi wowote unaoonesha mliripoti mamlaka za polisi Moshi kabla ya operesheni yenu?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Uko wapi?
SHAHIDI: sijaja nao
MATATA: mlipowakamata watuhumiwa mliwasafirisha kuja Dar?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: walipofika Dar mliwatoa central na kuwapeleka Mbweni?
SHAHIDI: Ni kweli.
MATATA: Kwanini mliwapeleka Mbweni?
SHAHIDI: Kwa sababu ya usalama.
MATATA: Kati ya Cetral na Mbweni wapi kuna usalama zaidi?
SHAHIDI: Lakini..
MATATA: Jibu, acha lakini.
SHAHIDI: Mbweni.
MATATA: Kati ya Central na Mbweni wapi kuna askari wengi?
SHAHIDI: Central.
MATATA: Kati ya central na Mbweni wapi kuna silaha nyingi zaidi?
SHAHIDI: Central.
MATATA: Kati ya central na Mbweni wapi panaweza kupatikana msaada wa haraka ikitokea dharura?
SHAHIDI: Central.
MATATA: Sasa unasemaje Mbweni kuna usalama kuliko central?
SHAHIDI: ili watuhumiwa wasiweze kutoroka.
MATATA: Umewahi kusikia pale central kuna watuhumiwa wametoroka?
SHAHIDI: kimya
MATATA: Jibu swali, umewahi kusikia watuhumiwa kutoroka central?
SHAHIDI: wangeweza kutoroka.
JAJI: Mbona swali rahisi, jibu kama umeshawahi kusikia wametoroka?
SHAHIDI: Mheshimiwa Jaji mimi sijui.
MATATA: Kwanini mliwapeleka watuhumiwa Mbweni?
SHAHIDI: Ni kwa maelekezo ya viongozi wangu.
MATATA: Nakuuliza wewe, sio viongozi wako.
SHAHIDI: Kama nilivyosema ni sababu za kiusalama.
MATATA: Utakubaliana na mimi kwamba mlipowaleta watuhumiwa Dar hujasema mliripoti kwa nani?
SHAHIDI: Tuliripoti kwa mamlaka za polisi kanda maalumu na mkoa wa kipolisi Kinondoni.
MATATA: Kwenye taarifa yako kuna mahali umeeleza hayo?
SHAHIDI: Hapana.
MATATA: Unaelewa kabla ya kuwasachi watuhumiwa, ilibidi nyie mlisachiwe kwanza?
shahidi ni kweli sijazungumza hilo.
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Lakini kwenye maelezo yako hujaeleza ka mlisachiwa kwanza kabla ya kuwasachi watuhumiwa.
SHAHIDI: Tulisachiwa japo sijaeleza.
MATATA: Kwa kuwa hujaeleza nitakosea nikisema hamkusachiwa.
SHAHIDI: Kimya.
MATATA: Umeeeleza kuwa watuhumiwa ni Makomandoo wa JWTZ?
SHAHIDI: Ni kweli.
MATATA: Utakubaliana na mimi kwamba Makomandoo ni watu ambao wanahitaji ulinzi zaidi?
SHAHIDI: Sahihi.
MATATA: Lakini katika maelezo yako hakuna popote umesema mliwasifirisha kwa pingu? Je utakubaliana na mimi nikisema mliwasafirisha makomandoo wa jeshi kizembe bila kuwafunga pingu?
SHAHIDI: Tuliwafunga
MATATA: Lakini maelezo yako uliyoandika hayaelezi hivyo.
SHAHIDI: Itakua nilisahau tu.
MATATA: Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.!
Malisa GJ
MATATA: Nikumbushe Majina yako.
SHAHIDI: Naitwa Inspector Mahita Omary Mahita.
MATATA: nitakuwa Sahihi nikisema wewe ni Mtoto wa IGP mstaafu Omary Mahita.
SHAHIDI: Upo sahihi
MATATA: Wakati Baba yako akiwa IGP wewe Ulikuwa wapi?
SHAHIDI: Nilikuwa Chuo kikuu
MATATA: Wakati Baba yako akiwa IGP ulikuwa na akili timamu?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Unakumbuka madai ya baba yako kuwakuta CUF na visu akadai wamekusudia kufanya ugaidi.
WAKILI WA JAMHURI: Objection Mheshimiwa Jaji. Naomba swali hilo liondolewe.
MATATA: Wakati mnawakamata watuhumiwa mlikuwa na Kikosi Maalum?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Kikosi chote kilitokea Arusha?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Na kikosi hicho kilikuwa chini ya RPC Kingai ambaye wakati huo alikua RCO Arusha?
SHAHIDI: Sahihi kabisa
MATATA: Unapotoka kwenye kituo unapaswa kuwa na Movement Order?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Ulipotoka Arusha kwenda Moshi hukueleza kuwa na movement order.
SHAHIDI: Nilikua nayo.
MATATA: Ulimweleza nani?
SHAHIDI: Sikueleza lakini nilikua nayo
MATATA: Maelezo yako ya awali hayaelezi hivyo.
SHAHIDI: Kimya.
MATATA: Je unajua kwamba unapofika mkoa mwingine unapaswa uriporti kwanza kwa Mlmamlaka za Mkoa huo?
SHAHIDI: Ni kweli.
MATATA: Katika maelezo yako hakuna popote uliposema umeripoti kwa mamlaka za polisi Moshi.
SHAHIDI: Ni kweli lakini?
MATATA: Hakuna lakini, jibu NDIYO au HAPANA.
SHAHIDI: Niliripoti lakini labda kwenye maelezo nilisahau kuandika.
MATATA: sasa kama hukuandika ulitegemea mahakama iote?
SHAHIDI: Kimya
MATATA: Una ushahidi wowote unaoonesha mliripoti mamlaka za polisi Moshi kabla ya operesheni yenu?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Uko wapi?
SHAHIDI: sijaja nao
MATATA: mlipowakamata watuhumiwa mliwasafirisha kuja Dar?
SHAHIDI: Ndio
MATATA: walipofika Dar mliwatoa central na kuwapeleka Mbweni?
SHAHIDI: Ni kweli.
MATATA: Kwanini mliwapeleka Mbweni?
SHAHIDI: Kwa sababu ya usalama.
MATATA: Kati ya Cetral na Mbweni wapi kuna usalama zaidi?
SHAHIDI: Lakini..
MATATA: Jibu, acha lakini.
SHAHIDI: Mbweni.
MATATA: Kati ya Central na Mbweni wapi kuna askari wengi?
SHAHIDI: Central.
MATATA: Kati ya central na Mbweni wapi kuna silaha nyingi zaidi?
SHAHIDI: Central.
MATATA: Kati ya central na Mbweni wapi panaweza kupatikana msaada wa haraka ikitokea dharura?
SHAHIDI: Central.
MATATA: Sasa unasemaje Mbweni kuna usalama kuliko central?
SHAHIDI: ili watuhumiwa wasiweze kutoroka.
MATATA: Umewahi kusikia pale central kuna watuhumiwa wametoroka?
SHAHIDI: kimya
MATATA: Jibu swali, umewahi kusikia watuhumiwa kutoroka central?
SHAHIDI: wangeweza kutoroka.
JAJI: Mbona swali rahisi, jibu kama umeshawahi kusikia wametoroka?
SHAHIDI: Mheshimiwa Jaji mimi sijui.
MATATA: Kwanini mliwapeleka watuhumiwa Mbweni?
SHAHIDI: Ni kwa maelekezo ya viongozi wangu.
MATATA: Nakuuliza wewe, sio viongozi wako.
SHAHIDI: Kama nilivyosema ni sababu za kiusalama.
MATATA: Utakubaliana na mimi kwamba mlipowaleta watuhumiwa Dar hujasema mliripoti kwa nani?
SHAHIDI: Tuliripoti kwa mamlaka za polisi kanda maalumu na mkoa wa kipolisi Kinondoni.
MATATA: Kwenye taarifa yako kuna mahali umeeleza hayo?
SHAHIDI: Hapana.
MATATA: Unaelewa kabla ya kuwasachi watuhumiwa, ilibidi nyie mlisachiwe kwanza?
shahidi ni kweli sijazungumza hilo.
SHAHIDI: Ndio
MATATA: Lakini kwenye maelezo yako hujaeleza ka mlisachiwa kwanza kabla ya kuwasachi watuhumiwa.
SHAHIDI: Tulisachiwa japo sijaeleza.
MATATA: Kwa kuwa hujaeleza nitakosea nikisema hamkusachiwa.
SHAHIDI: Kimya.
MATATA: Umeeeleza kuwa watuhumiwa ni Makomandoo wa JWTZ?
SHAHIDI: Ni kweli.
MATATA: Utakubaliana na mimi kwamba Makomandoo ni watu ambao wanahitaji ulinzi zaidi?
SHAHIDI: Sahihi.
MATATA: Lakini katika maelezo yako hakuna popote umesema mliwasifirisha kwa pingu? Je utakubaliana na mimi nikisema mliwasafirisha makomandoo wa jeshi kizembe bila kuwafunga pingu?
SHAHIDI: Tuliwafunga
MATATA: Lakini maelezo yako uliyoandika hayaelezi hivyo.
SHAHIDI: Itakua nilisahau tu.
MATATA: Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.!
Malisa GJ